ads

Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

Thursday, January 15, 2015

WIVU WA MAPENZI WAZUA BALAA MKOANI SHINYANGA

Mkazi  wa mtaa wa Kitwana kata ya Busoka wilayani Kahama mkoani Shinyanga Regina  Shija (55) ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga kichwani  na watu wasiojulikana kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa Kimapenzi.
Afisa mtendaji wa Mataa huo, Bw. Rafael Jumanne ameiambia paparazi kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 5.00 usiku ambao watu wasiofahamika walivamia nyumbani kwa  Regina akiwa  anajiandaa kulala na wajukuu wake wawili.
Amesema baada ya watu hao ambao idadi yao haijafahamika, kuvamia nyumbani hapo walianza kumkatakata mapanga mama huyo kichwani na  mkono wa kulia hali iliyosababisha kuvuja damu kwa wingi baadaye kufariki dunia.
Afisa Mtendaji huyo amedai kuwa chanzo cha  mauji hayo bado hakijafahamika ingawa yanahusishwa na wivu  wa kimapenzi na kwamba   jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu huyo na kuupeleka kuuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya wilaya ya Kahama.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Bw. Justus Kamugisha  amethibitisha kutokea kwa tukio  hilo ambapo amesema hakuana mtu yeyote anayeshikiliwa na kuwa jeshi hilo linaendelea na upelelezi huku akiwaomba wananchi kulisaidia kwa kutoa taarifa za siri zitakazoweza kulisaidia kuwabaini wahusika na hatimaye kuwakamata na kuwafikisha  katika vyombo vya sheria.

Sunday, January 11, 2015

MWANZA!!! Get ready Kwa mara ya Kwanza Kabisa!

MWANZA!!! Get ready for the ‪#‎STEPUP2014‬.... Kwa mara ya Kwanza Kabisa!!!, Hapa @diamondplatnumz MONDI hapa NAPPY BOY! @Tpain you Better save the Date!..21| 02 |2015

Sunday, April 27, 2014

COMING SOON MC SAIBA KUTOKA KISIBASHARESKY SASA AJA NA SONG IKO POA

Msanii wa miondoko ya hip hop kutoka kisibasharesky katika usimamizi wa yuskiss kisiba ambaye kwa sasa yuko kwenye maandalizi ya kutoa nyimbo yake inayokwenda kwa jina la IKO POA
Msanii huyo (MC SAIBA) Amesema ``kwa sasa najiandaa kutoa nyimbo hii pia na nyingine itafuata hivi karibu ambayo tunategemea video yake kufanyia nchini ghana kwa usimamizi wa yuskiss kisiba ambaye ndiye anaye jaribu kutimiza ndoto za watu wengi hasa kwa wasanii kwani ni producer na anaweza mambo mengi sana``Baada ya hapo yuskiss kisiba naye alisema kuwa ameamua kufanya kazi na Mc saiba kwani nikijana anaye jituma pia anakipaji na uandishi mzuri wa mashairi.Pia kisiba aliongezea kwakusema kuwa ana muandaa producer ambaye naye yupo katika lebo yake kwajina anajulikana kama DOBE GUY.
Pia anapenda kuwa karibisha vijana kwaajili yakutimiza ndoto zao popote pale walipo kwani Kisibasharesky entertainment haishughuliki na kitu kimoja ila kuna vitu vingi sana ndani yake.
https://www.facebook.com/pages/Yuskiss-Kisiba
https://www.facebook.com/ykisiba

Tuesday, April 22, 2014

KISIBASHARESKY SASA YAJA KATIKA MTAZAMO MPYA WA TUMAINI ZA KUTIMIZA NDOTO ZA WENYE VIPAJI AINA ZOTE SOMA HAPA KUFAHAMU ZAIDI

Yuskiss kisiba Kiongozi wa kampuni inayo jihusishana mambo mbalimbali mtandaoni na kisanaa KISIBASHARESKY ENTERTAINMENT ambaye CSW tulifanya mahojiano naye baada ya kuanzisha kitengo utengenezaji wa musiki.Yuskiss alisema ameamua kufanya hivyo kutokanana wasanii wengi wamekuwa wakihitaji msaada kutoka katika tasnia ya film na video lakini wanashindwa kutokana na msaada unakuwa mdogo kwa upande wao pia akaongeza kwa kusema kuwa kwa yoyote mtu mwenye kipaji ambaye atakuwa anajiweza na anajiamini hatosita kufanya nae kazi.
kwa sasa kisibasharesky inahusikana Utengenezaji wa video,graphics,photograph katika majarada na mitindo ya mavazi,Utengenezaji wa midundo aina zote (Beat) Matangazo aina zote mtandaoni,Blog design Pamoja na Cover aina zote Cd,dvd n.k.
kiongozi huyo anawakaribisha sana wale wote watakao penda kushirikiana naye.
kwani mpaka sasa kuna baadhi ya vijana tayari wamesha anza kazi
kama masanii Mc saiba na Dobe guy ambapo hivi karibuni kazi zao zitatoka kuanzia mtandaoni na media pia.

==Imeandikwa na Marry kutoka CSW.==

Friday, April 4, 2014

HAPPY BIRTHDAY DERRICK SWAG

Leo mwenyekiti wa kundi la Cash point jijini mwanza anasherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwake.
Kwakuonesha utofauti wa hali ya juu katika sherehe yake ambapo Ameambatana na wanakikundi wenzie chief Yuskiss kisiba,Jay 4 shizo manizo,Issa dody, simple girl pamoja na mashabiki wanao penda kundi hilo lenye mtazamo tofauti wa kimaisha Ambapo kundi
.Kundi hilo limepiga hatua katika masoko afrika mashariki katika swala la ujasiriamali  pia wameweza kumiliki kampuni zao binafsi kama COM,KIDO TZ Vijana hawa wamekuwa wakifanya vitu vya kipekee katika jamii kwa kuwasaidia watu mbalimbali
misaada pia Cash point imekusanya Vipaji mbalimbali kwakila aliyeomo ndani ya kundi kwakuwatembelea wodi ya wazazi kwakutoa misaada mbambali kwa wakina mama walio jifungua siku yaleo.
Huuni mfano wa kuigwa kwa vijana wa kiyanzania ambao wanaopenda kujiinua kiuchumi kwakuhakikisha wana pambana na umaskini hapa nchini bila ya kutegemea ajira serikalini.

==HAPPY BIRTHDAY DERRICK SWAG==

Tuesday, March 25, 2014

Mwanafunzi wa kidato cha nne, Shule ya Sekondari Makongo afariki dunia katika ajali mbaya ya Bajaji naLori jijini Dar

Mwanafunzi wa kidato cha nne, Shule ya Sekondari Makongo, PriscusMallya, amefariki dunia katika ajali iliyolihusisha lori na Bajaj katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi eneo la Bamaga, Dar. Kwa mujibu wa watuwaliokuwa eneo la tukio wakati ajali hiyo ikitokea, wamesema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ndani ya Bajaj pamoja na wenzake wawili wakielekea shuleni Makongo ambapo walikutana uso kwa uso na lori kisha kumrusha na kutokea upande wa pili marehemu.

DIAMOND ATOA YAKE YA MOYONI KUHUSU KUFUNGIWA KWA NYIMBO ZA WASANII WA HAPA BONGO..!! SOMA KAULI ALIYOITOA HAPA

Diamond Platnumz ndiye msanii aliyetajwa sana kuwania tuzo za KTM2014 katika vipengere kama 6 lakini ameamua kufunguka mtazamowake juu ya BASATA kuhusu kufungiwa kwa baadhi ya nyimbo za wasanii , kupitia katika akaunti yake ya instagram Diamond amefunguka na kuandika maneno mengi ya Busara zaidi kuhusu BASATA.Tazama hii picha uone alichofungukaNANUKUU"ikiwa kweli tunalengo la kutoipotosha kimaadili jamii yetu na vizazi vyetu pendwa, nafikiri ni vyema tungeanza kuzuia Video na nyimbo za kutoka nje, kuliko kuzuia nyimbo na video za nyumbani ambazo uchafu wake Haufikii hata robo ya uliopo kwenye Nyimbo zinazopewa kipaumbele toka nje... Hii ni sawa na kuzidi kuukuza mziki wa nje huku tukiudidimiza na kuua mziki wetu... Will the target of reaching our goals ever be achieved?? #Ni_Mtazamo_tu"MWISHO WA KUNUKUU

MDADA HUYU AJIUZA KUPITIA FACEBOOK, AKESHA AKIPOST PICHA ZA UTUPU

AnaitwaNEEMA PAUL MALIMOni jina analotumia Facebook, amekuwa ndio Tabia yakekuweka picha za kuwatega wanaume na kuwataka wampigie simu ili aweze kuwapa penzihilo kwa maelewano.Huyu inasemekana ni kahaba wa kutupwa kwani amekuwa akiweka picha zake zisizo na maadili na Ni biashara yake anayoifanya na soko lake anategemea FACEBOOK….!!!!EWE MWANANCHI JIHADHARI UKIMWI UNAUA…

HUYU NDYO MWANAFUNZI ALIYEJIRUSHA KUTOKEA GHOLIFANI MPAKA CHINI UDOM KISA SOMA HAPA

Mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu Dodoma – UDOM aliyefahamika kwa jina la KAMUGISHA S/O ISACK, Miaka 24, Mhaya, Mwaka wa Tatu, Kitivo chaSayansi ya Jamii (Social Science) anayeishi Block Namba 11, chumba Namba 62, alijitupa kutoka ghorofa ya pili hadi chini na kusababisha majeraha sehemu za mdomoni, shingoni na pajila uso.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamshna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amesema tukio hili limetokea terehe 18/03/2014 majira ya 20:15 huko maeneo ya chuo kikuu cha Dodoma manispaa na Mkoa wa Dodoma.Kamanda MISIME amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni ulevi. Majeruhi alilazwa katika hospitali ya UDOM na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na kuruhusiwa tarehe 20/03/2014 baada ya kuonekana hali yake inaendelea kuimarika.Aidha Kamanda MISIME amesema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote  kujibu shitaka la kujaribu kujiua.Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Sunday, March 16, 2014

MASKINI MTOTOANUSURIKA KUCHINJWA NA BABA YAKE KISA....

Mtukioyakikatili yameendelea kushika kasi wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo mtoto aitwayeSaid Siraji/SaidJoshuaamelazwa katika Hospitali ya wilaya usiku wa kuamkia leo, baada ya kunusurika kifo katika jaribio la kuchinjwa nababayake mzazi aliyejulikana kwa jina laSalvatory.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya-Kahama; DaktaJosephFwoma amesema Siraji amefikishwa hospitalini hapo leo alfajiri baada ya kuokotwa na wasamaria wema akiwa anakimbia huko akivuja damu shingoni.Dakta Fwoma amesema baada ya kufikishwa hospitalini madaktari walimfanyia upasuaji na kumshona sehemu ya koromeo aliyochinjwa na hadi alasiri hii hali yake imeendelea vizuri hasa baada ya kuongezwa damu.Kwa mujibu wamamamzazi wa Mariamu Idd(35) amesema, Mtoto Siraji jana alichukuliwa na baba yake mzazi anayeitwa Siraji Salvatory(45) kwenda naye kwake mitaa ya Majengo kwa kuwa wazazi hao walikwisha achana siku nyingi.Mariam amesema, awali Salvatory alikuwaakimchukua Sirajimarakwa mara na kumpeleka nyumbani kwake na baadaye kumrudisha akidai kuchoshwa na huduma za matibabu kutokana na mtoto huyo kuwa na matatizo ya kiafya.Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema chanzo cha tukio hilo inasadikiwa kuwa mtuhumiwa anaugua ugonjwa wa akili.

Thursday, March 6, 2014

HATARII..MFUNGWA AMBAKA MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI HUKO GEITA...!!!


MFUNGWA aliyekuwa
akitumikia kifungo cha miezi
sita katika Gereza la Butundwe
wilayani Geita amembaka
mwanafunzi wa Shule ya
Msingi Luhuha iliyoko Tarafa
ya Butundwe na kumuumiza
sehemu zake za siri, shingoni
na kwenye jicho la kulia.
Mwanafunzi huyo mwenye
umri wa miaka 15 (jina
linahifadhiwa) alitendewa
unyama huo na mfungwa
aliyejulikana kwa jina la
Godfrey Seleman (19) Februari
26, mwaka huu majira ya saa
9:00 alasiri wakati
mwanafunzi huyo alipokuwa
akichanja kuni na wanafunzi
wenzake.
Akieleza jinsi alivyofanyiwa
unyama huo, mwanafunzi
huyo alisema alipotoka shuleni
akiwa na wasichana wenzake
watano walikwenda kuchanja
kuni ndipo walipomuona
mfungwa huyo akiwa amevaa
sare, lakini baadaye alitoweka
ghafla na kurudi akiwa
amejipaka masizi usoni, akiwa
uchi kisha kuanza kumfukuza
yeye huku wenzake wengine
wakifanikiwa kukimbia huku
wakipiga kelele.
Alisema alizidiwa mbio na
mfungwa huyo ambapo
alimshika kisha kumkaba
shingoni na kumwangusha
chini na kuanza kumtendea
unyama na kumsababishia
maumivu makali sehemu zake
za siri.
“Baada ya kutendewa unyama
huo nilitoka eneo hilo ambapo
njiani nikutana na mama
mmoja nikamwelezea mkasa
ulionipata alinionea huruma
ambapo alinipeleka ofisi ya
kijiji ambako niliandikiwa
barua kuwahi polisi,
nikapelekwa hospitali ambako
walinifanyia vipimo,” alisema
binti huyo.
Aliendelea kusema kuwa
mfungwa huyo alimpiga na
kumuumiza katika jicho lake la
kulia ambalo limevimba na
kuwa bado anasikia maumivu
makali jichoni na
shingoni.Kamanda wa polisi
mkoani hapa amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo ambalo
ameliita la kinyama
lisilopaswa kutendwa na mtu
mwenye akili timamu.Alisema
mfungwa huyo mweye na
namba 244/2013 alikuwa atoke
kifungoni mwezi ujao, tayari
ametiwa mbaroni na
atafikishwa mahakamani
upelelezi utakapokamilika

Saturday, March 1, 2014

Whatsapp YAJA NA KASHESHE HIVI KARIBUNI LA KUWAUMBUA WAONGO

Kasheshe tena bonge la
kasheshe laja. Kwa kutumia
maspy wake wa kimataifa,
blog yenu mzigo imekuja na
taarifa ambayo italeta
usumbufu mkubwa katika
jamii ya watumia whatsapp
hapa Bongoland. Najua
mnajiuliza ni nini? Hata sisi
wakurugenzi, waandishi,
wafagizi wa hii blog ya
chekanakitime tuliduwaa
hivihivi kama wewe
ulivyoduwaa wakati tunasubiri
kuelezwa na spy wetu wa
kimataifa ni nini alichogundua
kuhusu watumiaji wa
Whatsapp.
Baada ya Whatsapp kuwa na
kale kamtindo kabaya ka
kuumbua watu kakusema 'Last
seen 2:00'na hivyo kuua kale
kakisingizio kuwa simu ilikuwa
imezima kwa kukosa chaji sasa
wanakuja na mpya zaidi. Kale
kakipengele katakuwa
kanataja hata ulipo, hivyo
katakuwa kakisomeka
mfano,'Last seen 2:00 Sokoni
Kariakoo'.
Sasa hii ni mbaya sana wakati
mtu kakutumia mesej...Baby
tumekusanyika hospitali
mamake rafiki yangu yu
mahututi' Huku Whatsapp
inakuonyesha 'Last seen 2:00
Coco Beach'... Kamtindo haka
kanategemea kuua mapenzi na
ndoa kadhaa ambazo mpaka
sasa zinaonekana kuwa imara
sana.

Thursday, February 27, 2014

Polisi wa Uganda wamezuia kundi la wanawake waliopanga kuandamana kupinga sheria inayopiga marufuku picha chafu.

Polisi wa Uganda wamezuia
kundi la wanawake waliopanga
kuandamana kupinga sheria
inayopiga marufuku picha
chafu.
Chini ya sheria hiyo ni marufuku
kwa wanawake kuvalia mavazi
mafupi, yenye kubana mwilini
kiasi cha kuonekana mapaja na
makalio na sheti inayoonyesha
matiti.
Wanawake hao waliopanga
kuandamana mjini Kampala
walibeba mabano kupinga sheria
mpya baadhi wakuvalia mavazi
mafupi. Baadaye walikubaliwa
kukusanyika katika uwanja nje ya
ukumbi wa kitaifa.

Tuesday, February 25, 2014

Daktari FEKI akamatwa hospitali ya Muhimbili......Hili ni tukio la tatu kutokea

Hospitali ya taifa ya Muhimbili imemkamata mtu mmoja anae sadikiwa kuwa daktari feki ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akitapeli wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika hospitali hiyo ya taifa kwa namna  mbalimbali  Daktari huyo aliyejulikana kwa jina la Kitano Mustafa Kitani mwenye umri miaka 51 anadaiwa kuwa alikuwa anajitambulisha kama daktari upande wa akina mama katika hospitali ya Muhimbili.Hospitali ya taifa ya Muhimbili mbali na utaratibu wa kutumia vitambulisho kwa wafanyakazi ili kuondoa tatizo kama hili, bado tatizo hili limeendelea kujitokeza.Hospitali ya Muhimbili inawataka wafanyakazi wake wanaoshirikiana na madaktari vishoka kuacha tabia hiyo yenye athari kwa wagonjwa na taifa.Chama cha Madaktari nchini kimewataka wananchi kuwa  macho na madaktari wanaojitokeza kutaka kusaidia wagonjwa.Wakati daktari huyo akidai yeye ni daktari kitaaluma, Afisa Usalama hakubaliani nae kutokana na taarifaza kiuchunguzi kuthibitisha kuwa ni feki.Hili ni tukio la tatu kutokea katika hospitali ya Muhimbili.

Monday, February 24, 2014

MWANA DADA MREMBO AFIA GEST JIJINI ARUSHA

MREMBO mmoja ambaye alihu-
dumu kwenye nyumba ya kulala
wageni na baa (jina tunalo)
iliyopo Tengeru, wilayani
Arumeru, mkoani Arusha,
Blandina Michael (33) amekutwa
amekufa kwenye moja ya vyumba
vya nyumba hiyo huku chanzo
cha tukio hilo kikihusishwa na
vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu
mmiliki wa nyumba ya wageni
moja ambaye pia anajihusisha na
biashara za madini (jina tunalo)
kwamba alimtoa kafara
mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa,
kila mwaka mtu mmoja katika
biashara zake hupoteza maisha
ghafla.
Hata hivyo, mfanyabiashara huyo
alipoongea na Uwazi juzikati
alikanusha vikali tuhuma hizo na
kueleza kuwa yeye ni muumini
mzuri wa imani yake.
‘’Hao watu wanapotosha sana,
unajua kuna mwaka mwanaume
mmoja alikufa ghafla kwenye
nyumba yangu ya kulala wageni,
alikuja na mpenzi wake ila
alimeza Viagra ambazo hata
polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na
mimi tukio hilo wanaliunganisha
na hili kwamba nawatoa kafara,”
alisema.
Kifo cha Blandina kilitokea ndani
ya chumba huku mtu mmoja
anayedaiwa kuwa mpenzi wake
aliyejulikana kwa jina moja la
Timo, mkazi wa eneo hilo
akihojiwa na polisi.
Marehemu Blandina ambaye ni
mzaliwa wa mkoa wa Tanga,
anaelezwa na bosi wake huyo
kwamba alikuwa kama mtoto wa
familia yake kwa vile alimwamini
sana. Alifanya kazi hapo kwa
miaka 8 na hakuwa na tatilo la
kiafya.
Bosi huyo alisema mwili wa
marehemu uligundulika baada ya
mfanyakazi mwenzake wa kiume
kumpigia simu saa 2 asubuhi
ambapo simu yake ilikuwa ikiita
bila kupokelewa ndipo alipoamua
kwenda kumgongea katika
chumba hicho.
Alisema baada ya kufika
alishangaa kukuta mlango wa
chumba chake uko wazi na
alipochungulia alibaini kwamba
Blandina alikuwa amefariki dunia.
Hata hivyo, polisi baada ya kufika
na kuufanyia uchunguzi wa awali
mwili huo hawakugundua
kuwepo kwa jeraha lolote
linaloashiria kuuawa, ingawa
mwili huo ulipelekwa kufanyiwa
uchunguzi wa kitaalam katika
Hospitali ya Mkoa ya Mount
Meru.

COVER YA FILAMU YA MPONZA DR.CHENI

Msanii wa filamu hapa nchini
anayefahamika kwa jina la Dr.
amejikuta katika wakati mgumu
baada ya bodi ya filamu Tanzania
kuzuia filamu yake mpya inayoitwa
'Nimekubali Kuolewa' kwa madai
ya cover iliyotumika katika kasha
la filamu hiyo inachochea ushoga.
Kufuatia madai hayo msanii huyo
amesema kuwa
bodi hiyo haikumtendea haki kwa
kuwa filamu yake ina lengo zuri la
kupinga ushoga na sio kuchochea.
Ameela bodi hiyo haikuangalia
maudhui na badala yake
imeangalia zaidi cover la filamu
hiyo
“Eti ushoga wangu uko kwenye
kujiremba sana, wamenionea,
lengo letu ni kukemea na kupinga
vikali vitendo vya ushoga na ndoa
za jinsia moja, huwezi kuelimisha
bila kuonesha madhara yake kwa
vitendo kama ilivyo kwenye filamu
hiyo. Amesema Dk Cheni.
Msanii huyu amekumbwa na hali
hiyo ikiwa ni muendelezo wa bodi
ya filamu kuzuia filamu ambazo
inazitilia mashaka.
Hata hivyo bodi hii imekuwa
ikilalamikiwa na baadhi ya wasanii
wakidai haitendi haki.

VIFO VYA WATOTO KUONGEZEKA KILA MWAKA KUTOKANA NA VITA VINAVYO ENDELEA DUNIA


Shirika la Misaada kwa watoto,
Save the Children, linasema
kuwa watoto milioni moja
hufariki dunia kila mwaka
katika siku yao ya kwanza ya
maisha.
Katika ripoti mpya ya shirika hilo
la misaada kwa watoto linasema
vifo vya watoto wachanga
vimesalia kuwa moja ya aibu za
dunia ya sasa.
Hali ya watoto ni mbaya zaidi
hasa katika mataifa
yanayokabiliwa na mizozo.
Mwandishi wa BBC aliye Sudan
Kusini, Anne Soy, amesema kuwa
katika mazingira ya sasa ya Sudan
Kusini, watoto na wanawake, hasa
wale waja
wazito wanaokabiliwa na athari
nyingi za vita vinavyoendelea
nchini humo.
Amesema kuwa kutokana na vita
watoto, walioandamana na wazazi
wengine wakiwa pekee,
wanaungana na akina mama
kutembelea mwendo
mrefu ili kujiepusha na vita vya
kikabila vinavyoendelea nchini.
Miundo msingi katika Sudan
Kusini, kama vile hospitali ni
chache sana jambo ambalo
linatatiza maisha ya wanawake na
watoto.
Katika hospitali ya mji wa Nimule
kwenye mpaka wa Sudan Kusini
na Uganda Kuna vitanda 174
pekee hospitalini idadi ambayo
haiafikiana kamwe
na maelfu ya wagonjwa na
wahasiriwa wa vita .
Save the children inasema kuwa
vita vinawaathiri zaidi watoto
huko Syria, Jamhuri ya Afrika ya
Kati CAR na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la Save the Children
linasema kuwa vifo hivi vingi
vinaweza kuzuiliwa.

VIJIMAMBO KATIKA JAMII NIPE NIKUPE SAMAKI NA NGONO KENYA

Inakadiriwa takriban watu milioni
moja na nusu wanaishi na virusi
vya HIV na maradhi ya UKIMWI
nchini Kenya.
Wavuvi vijijini huwapa wauza
samaki wanawake samaki kama
malipo kwa kufanya nao ngono
badala ya pesa.
Lakini sasa mashirika ya misaada
yanajaribu kubadilisha tabia hii,
ijulikanayo kama 'kubadilisha
ngono na samaki'.
Wanawahimiza wanawake
wanunue mashua zao wenyewe.
Mariam Omar ana zaidi toka
magharibi mwa Kenya.

MTANZANIA SABRINA ABAKWA NA WANIGERIA WATANO CHINA, APOTEZA MAISHA

Mwandishi Wetu
AMA kweli dunia hadaa,
ulimwengu shujaa! Kumeibuka
mchezo mchafu,
kuna Watanzania wanawachukua
warembo nchini na kuwapeleka
China kwa ahadi kwamba
wanakwenda kufanya kazi saluni,
wakifika kule wanawanyang’anya
paspoti na kuwauza kwa
wanaume (ukahaba), sasa
yamemkuta Mbongo aitwaye
Sabrina au Habiba, Ijumaa
Wikienda lina mkasa wa
kusikitisha.
Habari za uhakika kutoka kwa
chanzo chetu nchini humo
zilisema kuwa, Sabrina (24),
alifariki dunia Alhamisi iliyopita
kufuatia kubakwa na wanaume
watano, raia wa Nigeria ambao
wamo nchini humo kibiashara.
Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli
moja iliyopo kwenye Mji wa
Guangzhou ambao umejaa
wageni wengi, wakiwemo
Watanzania.
SIKU YA TUKIO
Rafiki wa karibu wa Sabrina,
Saada alisema siku ya tukio,
marehemu akiwa katika harakati
zake za kutafuta wateja alikutana
na Mnigeria mmoja ambaye
walipatana kulala wote kwa usiku
mzima.
“Kumbe yule Mnaigeria alikuwa
na wenzake wanne. Usiku
walimwingilia wote kwa nguvu
kwa kumbaka mpaka akapoteza
maisha palepale. Ni ukatili
mkubwa.
“Wale watu walipogundua
Sabrina amekufa waliuchukua
mwili wake na kuutupa chini
kutoka ghorofa ya tano,” alisema
rafiki huyo.
MAITI YAKUTWA HAINA FIGO,
MOYO
Habari zaidi zilidai kuwa mpaka
juzi (Jumamosi) madaktari
waliokuwa wakiuchunguza mwili
wa Sabrina waligundua hauna
figo na moyo, jambo linalozidi
kuzua hofu juu ya muaji yake.
NI BIASHARA ILIYOIBUKA CHINA?
Ilidaiwa kuwa nchini China
imeibuka biashara ya viungo
mbalimbali vya binadamu
ambapo ili vipatikane ni lazima
mwenye viungo hivyo auawe kwa
njia yoyote.
SABRINA AFA, MGANDA APOTEA
Mtoa habari wetu alisema wakati
Wabongo wakiwa kwenye
maombolezo ya kifo cha
Mtanzania huyo, mrembo
mwingine raia wa Uganda, nchi
ambayo imo ndani ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki amepotea katika
mazingira ya kutatanisha nchini
humo.
Baadhi ya watu wana wasiwasi
kuwa kupotea kwa msichana
huyo kunahusiana na kushamiri
kwa biashara ya viungo vya
binadamu.
SABRINA ALIKWENDAJE CHINA?
Mwezi Julai, mwaka jana, Sabrina
alikwenda nchini humo
akidanganywa na mwanamke
mmoja kwamba atapata kazi
kwenye saluni ya wanawake lakini
baada ya kufika alijikuta
akiingizwa kwenye biashara ya
ukahaba bila ridhaa yake mpaka
alipokutwa na mkasa huo
uliopoteza maisha yake.
TAHADHARI KWA WAREMBO
WANAOKWENDA CHINA KUFANYA
KAZI SALUNI
Imebainika kuwa, kumeibuka
wimbi la Wabongo wanaofanya
‘uwakala’ wa kuwachukua
wasichana wa Kitanzania kwa
kuwadanganya kwamba
wanakwenda kufanya kazi za
saluni nchini humo.
Mara baada ya kufika, wasichana
hao hunyang’anywa paspoti ili
washindwe kuondoka nchini
humo na kushinikizwa kujiuza
(ukahaba) huku waliowapeleka
wakipokea fedha kutoka kwa
wateja.
KUIKOMBOA PASPOTI
Habari zilisema kuwa mhusika
hurejeshewa paspoti yake baada
ya malipo yake kwa ‘wakala’
kufikia dola za Marekani 8,000
(kama shilingi milioni 12), ndipo
huachiwa ‘huru’ kuendelea na
maisha yake.
Wengi wakishaachiwa hushindwa
kurejea Bongo na kujikuta
wakiendelea kuuza miili katika
mahoteli na klabu huku
wakikutana na majanga
mbalimbali.
MASOGANGE, KAJALA NA DIDA
Watanzania waishio nchini humo
wamewatahadharisha mastaa wa
Bongo, wakiwemo Mtangazaji wa
Radio TimesFM, Khadija Shaibu
‘Dida’, msanii wa filamu Kajala
Masanja na Video Queen Agnes
Gerald ‘Masogange’ ambao
hupenda kwenda nchini humo
kwa shughuli zao, kutokubali
kuwa karibu na mawakala wa
kuchukua wasichana Bongo kwa
kuwadanganyia kazi ya saluni
kwani wanaweza kujikuta pabaya
siku moja.
DIDA
Ijumaa Wikienda lilimsaka Dida
siku ya Jumamosi iliyopita na
kumuuliza kuhusu kuwepo kwa
mawakala hao ambapo alikiri
kusikia huku akisema warembo
wenyewe wanapaswa kuwa
macho na udanganyifu huo.
“Najua wapo Wabongo
wanaofanya shughuli hiyo, si
China tu hata India, unapelekwa
kwa ahadi ya kazi ya saluni,
ukifika hamna cha saluni wala
nini? Warembo wawe makini
jamani, nenda China kama una
uwezo wako mwenyewe kufanya
‘shoping’ lakini si kupelekwa,”
alisema Dida.
BALOZI WA TANZANIA-CHINA
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta
Balozi wa Tanzania nchini China,
Luteni Jenerali Mstaafu
Abdulrahman Shimbo ili
azungumze lolote kuhusu tukio la
Sabrina, lakini simu yake
ilionekana kutokuwa hewani kwa
muda mrefu.

Sunday, February 23, 2014

HUU NDIO UJIO MPYA WA MDADA RAY C...!!!SOMA ZAIDI HAPA...

Anaitwa Rehema Chalamila kwenye stage ya muziki tunamjua kama Ray C. Kitu kikubwa kinachosubiriwa kutoka kwake hivi sasa kazi zake mpya kwenye muziki baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu. Kitu cha kusubiria sio hicho tu bali Ray C Foundation ni kitu kingine kitakacho kuja kutoka kwa Ray C. Ameshare ujio wa foundation hii kwenye ukurasa
wake wa instagram na
kudokeza kwa maneno
“Coming soon stay tuned!!!!!”
japokuwa hakuweka wazi kazi
ambayo itafanywa na
foundation hiyo.