MWANZA!!! Get ready for the #STEPUP2014.... Kwa mara ya Kwanza Kabisa!!!, Hapa @diamondplatnumz MONDI hapa NAPPY BOY! @Tpain you Better save the Date!..21| 02 |2015
MWANZA!!! Get ready for the #STEPUP2014.... Kwa mara ya Kwanza Kabisa!!!, Hapa @diamondplatnumz MONDI hapa NAPPY BOY! @Tpain you Better save the Date!..21| 02 |2015
Yuskiss kisiba Kiongozi wa kampuni inayo jihusishana mambo mbalimbali mtandaoni na kisanaa KISIBASHARESKY ENTERTAINMENT ambaye CSW tulifanya mahojiano naye baada ya kuanzisha kitengo utengenezaji wa musiki.Yuskiss alisema ameamua kufanya hivyo kutokanana wasanii wengi wamekuwa wakihitaji msaada kutoka katika tasnia ya film na video lakini wanashindwa kutokana na msaada unakuwa mdogo kwa upande wao pia akaongeza kwa kusema kuwa kwa yoyote mtu mwenye kipaji ambaye atakuwa anajiweza na anajiamini hatosita kufanya nae kazi.
kwa sasa kisibasharesky inahusikana Utengenezaji wa video,graphics,photograph katika majarada na mitindo ya mavazi,Utengenezaji wa midundo aina zote (Beat) Matangazo aina zote mtandaoni,Blog design Pamoja na Cover aina zote Cd,dvd n.k.
kiongozi huyo anawakaribisha sana wale wote watakao penda kushirikiana naye.
kwani mpaka sasa kuna baadhi ya vijana tayari wamesha anza kazi
kama masanii Mc saiba na Dobe guy ambapo hivi karibuni kazi zao zitatoka kuanzia mtandaoni na media pia.
==Imeandikwa na Marry kutoka CSW.==
Leo mwenyekiti wa kundi la Cash point jijini mwanza anasherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwake.
Kwakuonesha utofauti wa hali ya juu katika sherehe yake ambapo Ameambatana na wanakikundi wenzie chief Yuskiss kisiba,Jay 4 shizo manizo,Issa dody, simple girl pamoja na mashabiki wanao penda kundi hilo lenye mtazamo tofauti wa kimaisha Ambapo kundi
.Kundi hilo limepiga hatua katika masoko afrika mashariki katika swala la ujasiriamali pia wameweza kumiliki kampuni zao binafsi kama COM,KIDO TZ Vijana hawa wamekuwa wakifanya vitu vya kipekee katika jamii kwa kuwasaidia watu mbalimbali
misaada pia Cash point imekusanya Vipaji mbalimbali kwakila aliyeomo ndani ya kundi kwakuwatembelea wodi ya wazazi kwakutoa misaada mbambali kwa wakina mama walio jifungua siku yaleo.
Huuni mfano wa kuigwa kwa vijana wa kiyanzania ambao wanaopenda kujiinua kiuchumi kwakuhakikisha wana pambana na umaskini hapa nchini bila ya kutegemea ajira serikalini.
==HAPPY BIRTHDAY DERRICK SWAG==
AnaitwaNEEMA PAUL MALIMOni jina analotumia Facebook, amekuwa ndio Tabia yakekuweka picha za kuwatega wanaume na kuwataka wampigie simu ili aweze kuwapa penzihilo kwa maelewano.Huyu inasemekana ni kahaba wa kutupwa kwani amekuwa akiweka picha zake zisizo na maadili na Ni biashara yake anayoifanya na soko lake anategemea FACEBOOK….!!!!EWE MWANANCHI JIHADHARI UKIMWI UNAUA…
Mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu Dodoma – UDOM aliyefahamika kwa jina la KAMUGISHA S/O ISACK, Miaka 24, Mhaya, Mwaka wa Tatu, Kitivo chaSayansi ya Jamii (Social Science) anayeishi Block Namba 11, chumba Namba 62, alijitupa kutoka ghorofa ya pili hadi chini na kusababisha majeraha sehemu za mdomoni, shingoni na pajila uso.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamshna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amesema tukio hili limetokea terehe 18/03/2014 majira ya 20:15 huko maeneo ya chuo kikuu cha Dodoma manispaa na Mkoa wa Dodoma.Kamanda MISIME amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni ulevi. Majeruhi alilazwa katika hospitali ya UDOM na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na kuruhusiwa tarehe 20/03/2014 baada ya kuonekana hali yake inaendelea kuimarika.Aidha Kamanda MISIME amesema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote kujibu shitaka la kujaribu kujiua.Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.
Mtukioyakikatili yameendelea kushika kasi wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo mtoto aitwayeSaid Siraji/SaidJoshuaamelazwa katika Hospitali ya wilaya usiku wa kuamkia leo, baada ya kunusurika kifo katika jaribio la kuchinjwa nababayake mzazi aliyejulikana kwa jina laSalvatory.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya-Kahama; DaktaJosephFwoma amesema Siraji amefikishwa hospitalini hapo leo alfajiri baada ya kuokotwa na wasamaria wema akiwa anakimbia huko akivuja damu shingoni.Dakta Fwoma amesema baada ya kufikishwa hospitalini madaktari walimfanyia upasuaji na kumshona sehemu ya koromeo aliyochinjwa na hadi alasiri hii hali yake imeendelea vizuri hasa baada ya kuongezwa damu.Kwa mujibu wamamamzazi wa Mariamu Idd(35) amesema, Mtoto Siraji jana alichukuliwa na baba yake mzazi anayeitwa Siraji Salvatory(45) kwenda naye kwake mitaa ya Majengo kwa kuwa wazazi hao walikwisha achana siku nyingi.Mariam amesema, awali Salvatory alikuwaakimchukua Sirajimarakwa mara na kumpeleka nyumbani kwake na baadaye kumrudisha akidai kuchoshwa na huduma za matibabu kutokana na mtoto huyo kuwa na matatizo ya kiafya.Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema chanzo cha tukio hilo inasadikiwa kuwa mtuhumiwa anaugua ugonjwa wa akili.
Mwanadada Wema Sepetu ambaye
pia aliwahi kuwa Miss Tanzania
2006 ambaye kwa sasa
anaendesha kampuni yake binafsi
iitwayo Endless Fame
inayojishughulisha zaidi na
utengenezaji wa Filamu
mbalimbali.
Kupitia kipindi cha Leo tena
February 28 Wema Sepetu
amekubali kutaja sifa za
mwanaume anayempenda kuwa na
mvuto kwake,swali lililoulizwa na
Watangazaji wa kipindi hicho ni
kuhusu mwanaume wa sifa gani
anayedhani anaweza kuolewa nae
ambapo Wema alijibu “Kuolewa sio
shida je huyo mwanaume
nampenda,maana naweza kuja
kuchumbiwa lakini nisimpende”
“Mimi nampenda Mwanaume
mweusi,wanaume weupe sio
kwamba sijawahi kuwa nao lakini
nakuwa sina mzuka nao”.
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake
na Diamond amekiri kwa
kusema’Kweli niko na Nasib -
Diamond na nadhani muda huu
kutakua na utulivu ndani yake,ule
utoto tuliokua tunafanya nadhani
ulikua utoto na imekua Power
Couple toka mwaka 2010 kwa hiyo
tuna ni miaka 4 sasa,kwa sasa
tumeamua kuwa serious’.
Habari kwa Hisani ya Millard Ayo
Wema Sepetu pia kaandamana na
Ant Ezekiel kwenye interview ya
kipindi hicho kinachorushwa na
Clouds Fm.
Diamond Platnumz
kiukweli, nasikitishwa sana jins
baadhi ya wasanii kutwa
wanavyolazimisha kunitengenezea
ugomvi wa kilazima pasipo kuwa na
sababu, mara wengine wakizusha
eti Nimewatusi kwenye Media,
Mara sjui Nimepost kuwakashif,
yaani ilimradi tu....kwanini
Wanamuziki wa Tanzania
Tunashindwa kubadilika... mbona
mi nahangaika na muziki wangu
kimpango wangu... Mnasema nyie
ndio mnaojua kuimba mie sijui
"sinatatizo"... Mnasema nyie ndio
wenye sauti nzuri yangu mbaya
"Sina tatizo"... sasa mbona tena
bado mnanifatilia na kutokujua
kwangu... Nafkiri ni vyema mkaanza
kutumia ujuzi wenu kukuza sanaa
ya nchi yetu na kuleta heshima na
maendeleo nchini, kuliko kupika
majungu..... Watu wanataka kazi!
Pichani kushoto ni bi mdada
Chanel Tapper akionyesha urefu
wa ulimi wake
Chanel Tapper ni mwanafunzi wa
chuo cha California Marekani,
ndiye mwanamke wa kwanza
anayeshikilia rekodi ya dunia ya
kuwa na ulimi mrefu kupita
wanawake wote, inasemekana
anaulimi wenye urefu wa sentimita
9.7, baada ya kuingia katika kitabu
cha rekodi za dunia maarufu kama
Guiness , amesema anategemea
wahisani pamoja na hela
atakazopata ziweze kumuendeleza
katika kumaliza chuo na masomo
yake.
Baada ya kutimuliwa
MTANASHATI msanii PNC arudi
mikono nyuma akimuomba boss
wake Ostaz Juma arudi tena
katika lebo hiyo. Picha hii
imeonekana katika account ya
facebook ya Ostaz Juma ikisema
“hahaha jamani mziki ni kazi
pnc arudi kuomba msamaha ili
aendelee kufanya kazi
mtanashati”
Na baadae mtu mzima Ostaz
akatupia video clip ikimuonyesha
PNC akiomba msamaha kwa
machungu kabisa hebu bonyez
CREDIT : DJ CHOKA
Nisha amfanyia suprise mama
yake Hemedi PHD katika siku
ya kuzaliwa mama yake Hemedi
PHD ilikuwa kinondoni
barabarani akamwambia
hemedi kapata ajali alivyotoka
nje alikuwa kapagawa mara
waka mwimbia happy birth day
toyuuuuuuuuu...!!!
Ha ha haaa!!! Mama Hemedy
hoi tena kibaya zaidi siku hio
ilikuwa ndio siku ya
kumaliziwa Shooting ya Filamu
ya GUMZO ambayo kwa sasa
ipo mbioni kutoka,
Yani mama kutoka tu nje
akaona msongamano wa
magari watu kibao akaamini
kuwa mwanae kapata ajali
kweli kumbe ilikuwa ni katika
kumalizia kipande cha Filamu
ambapo Hemedi PHD
anatakiwa aonekane katika
ajali ya kugongwa na gari.. Du!
mama almanusura kuzimia.
Mama yake hemedi alifarijika
sana ilikuwa kipindi cha
shooting ya gumzo
MREMBO mmoja ambaye alihu-
dumu kwenye nyumba ya kulala
wageni na baa (jina tunalo)
iliyopo Tengeru, wilayani
Arumeru, mkoani Arusha,
Blandina Michael (33) amekutwa
amekufa kwenye moja ya vyumba
vya nyumba hiyo huku chanzo
cha tukio hilo kikihusishwa na
vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu
mmiliki wa nyumba ya wageni
moja ambaye pia anajihusisha na
biashara za madini (jina tunalo)
kwamba alimtoa kafara
mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa,
kila mwaka mtu mmoja katika
biashara zake hupoteza maisha
ghafla.
Hata hivyo, mfanyabiashara huyo
alipoongea na Uwazi juzikati
alikanusha vikali tuhuma hizo na
kueleza kuwa yeye ni muumini
mzuri wa imani yake.
‘’Hao watu wanapotosha sana,
unajua kuna mwaka mwanaume
mmoja alikufa ghafla kwenye
nyumba yangu ya kulala wageni,
alikuja na mpenzi wake ila
alimeza Viagra ambazo hata
polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na
mimi tukio hilo wanaliunganisha
na hili kwamba nawatoa kafara,”
alisema.
Kifo cha Blandina kilitokea ndani
ya chumba huku mtu mmoja
anayedaiwa kuwa mpenzi wake
aliyejulikana kwa jina moja la
Timo, mkazi wa eneo hilo
akihojiwa na polisi.
Marehemu Blandina ambaye ni
mzaliwa wa mkoa wa Tanga,
anaelezwa na bosi wake huyo
kwamba alikuwa kama mtoto wa
familia yake kwa vile alimwamini
sana. Alifanya kazi hapo kwa
miaka 8 na hakuwa na tatilo la
kiafya.
Bosi huyo alisema mwili wa
marehemu uligundulika baada ya
mfanyakazi mwenzake wa kiume
kumpigia simu saa 2 asubuhi
ambapo simu yake ilikuwa ikiita
bila kupokelewa ndipo alipoamua
kwenda kumgongea katika
chumba hicho.
Alisema baada ya kufika
alishangaa kukuta mlango wa
chumba chake uko wazi na
alipochungulia alibaini kwamba
Blandina alikuwa amefariki dunia.
Hata hivyo, polisi baada ya kufika
na kuufanyia uchunguzi wa awali
mwili huo hawakugundua
kuwepo kwa jeraha lolote
linaloashiria kuuawa, ingawa
mwili huo ulipelekwa kufanyiwa
uchunguzi wa kitaalam katika
Hospitali ya Mkoa ya Mount
Meru.
Mwandishi Wetu
AMA kweli dunia hadaa,
ulimwengu shujaa! Kumeibuka
mchezo mchafu,
kuna Watanzania wanawachukua
warembo nchini na kuwapeleka
China kwa ahadi kwamba
wanakwenda kufanya kazi saluni,
wakifika kule wanawanyang’anya
paspoti na kuwauza kwa
wanaume (ukahaba), sasa
yamemkuta Mbongo aitwaye
Sabrina au Habiba, Ijumaa
Wikienda lina mkasa wa
kusikitisha.
Habari za uhakika kutoka kwa
chanzo chetu nchini humo
zilisema kuwa, Sabrina (24),
alifariki dunia Alhamisi iliyopita
kufuatia kubakwa na wanaume
watano, raia wa Nigeria ambao
wamo nchini humo kibiashara.
Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli
moja iliyopo kwenye Mji wa
Guangzhou ambao umejaa
wageni wengi, wakiwemo
Watanzania.
SIKU YA TUKIO
Rafiki wa karibu wa Sabrina,
Saada alisema siku ya tukio,
marehemu akiwa katika harakati
zake za kutafuta wateja alikutana
na Mnigeria mmoja ambaye
walipatana kulala wote kwa usiku
mzima.
“Kumbe yule Mnaigeria alikuwa
na wenzake wanne. Usiku
walimwingilia wote kwa nguvu
kwa kumbaka mpaka akapoteza
maisha palepale. Ni ukatili
mkubwa.
“Wale watu walipogundua
Sabrina amekufa waliuchukua
mwili wake na kuutupa chini
kutoka ghorofa ya tano,” alisema
rafiki huyo.
MAITI YAKUTWA HAINA FIGO,
MOYO
Habari zaidi zilidai kuwa mpaka
juzi (Jumamosi) madaktari
waliokuwa wakiuchunguza mwili
wa Sabrina waligundua hauna
figo na moyo, jambo linalozidi
kuzua hofu juu ya muaji yake.
NI BIASHARA ILIYOIBUKA CHINA?
Ilidaiwa kuwa nchini China
imeibuka biashara ya viungo
mbalimbali vya binadamu
ambapo ili vipatikane ni lazima
mwenye viungo hivyo auawe kwa
njia yoyote.
SABRINA AFA, MGANDA APOTEA
Mtoa habari wetu alisema wakati
Wabongo wakiwa kwenye
maombolezo ya kifo cha
Mtanzania huyo, mrembo
mwingine raia wa Uganda, nchi
ambayo imo ndani ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki amepotea katika
mazingira ya kutatanisha nchini
humo.
Baadhi ya watu wana wasiwasi
kuwa kupotea kwa msichana
huyo kunahusiana na kushamiri
kwa biashara ya viungo vya
binadamu.
SABRINA ALIKWENDAJE CHINA?
Mwezi Julai, mwaka jana, Sabrina
alikwenda nchini humo
akidanganywa na mwanamke
mmoja kwamba atapata kazi
kwenye saluni ya wanawake lakini
baada ya kufika alijikuta
akiingizwa kwenye biashara ya
ukahaba bila ridhaa yake mpaka
alipokutwa na mkasa huo
uliopoteza maisha yake.
TAHADHARI KWA WAREMBO
WANAOKWENDA CHINA KUFANYA
KAZI SALUNI
Imebainika kuwa, kumeibuka
wimbi la Wabongo wanaofanya
‘uwakala’ wa kuwachukua
wasichana wa Kitanzania kwa
kuwadanganya kwamba
wanakwenda kufanya kazi za
saluni nchini humo.
Mara baada ya kufika, wasichana
hao hunyang’anywa paspoti ili
washindwe kuondoka nchini
humo na kushinikizwa kujiuza
(ukahaba) huku waliowapeleka
wakipokea fedha kutoka kwa
wateja.
KUIKOMBOA PASPOTI
Habari zilisema kuwa mhusika
hurejeshewa paspoti yake baada
ya malipo yake kwa ‘wakala’
kufikia dola za Marekani 8,000
(kama shilingi milioni 12), ndipo
huachiwa ‘huru’ kuendelea na
maisha yake.
Wengi wakishaachiwa hushindwa
kurejea Bongo na kujikuta
wakiendelea kuuza miili katika
mahoteli na klabu huku
wakikutana na majanga
mbalimbali.
MASOGANGE, KAJALA NA DIDA
Watanzania waishio nchini humo
wamewatahadharisha mastaa wa
Bongo, wakiwemo Mtangazaji wa
Radio TimesFM, Khadija Shaibu
‘Dida’, msanii wa filamu Kajala
Masanja na Video Queen Agnes
Gerald ‘Masogange’ ambao
hupenda kwenda nchini humo
kwa shughuli zao, kutokubali
kuwa karibu na mawakala wa
kuchukua wasichana Bongo kwa
kuwadanganyia kazi ya saluni
kwani wanaweza kujikuta pabaya
siku moja.
DIDA
Ijumaa Wikienda lilimsaka Dida
siku ya Jumamosi iliyopita na
kumuuliza kuhusu kuwepo kwa
mawakala hao ambapo alikiri
kusikia huku akisema warembo
wenyewe wanapaswa kuwa
macho na udanganyifu huo.
“Najua wapo Wabongo
wanaofanya shughuli hiyo, si
China tu hata India, unapelekwa
kwa ahadi ya kazi ya saluni,
ukifika hamna cha saluni wala
nini? Warembo wawe makini
jamani, nenda China kama una
uwezo wako mwenyewe kufanya
‘shoping’ lakini si kupelekwa,”
alisema Dida.
BALOZI WA TANZANIA-CHINA
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta
Balozi wa Tanzania nchini China,
Luteni Jenerali Mstaafu
Abdulrahman Shimbo ili
azungumze lolote kuhusu tukio la
Sabrina, lakini simu yake
ilionekana kutokuwa hewani kwa
muda mrefu.
NI kweli ukistaajabu ya Musa
utayaona ya Firauni! Fumanizi la
aina yake lilitokea juzikati
asubuhi ya saa 2, Mtaa wa
Mbwela, Tandika jijini Dar
ambapo mjamzito aliyejulikana
kwa jina la Semeni alipata
‘kichaa’ cha muda baada ya
kumfumania mumewe, Dullah
akiwa na mwanamke mwingine
chumbani kwao, Risasi Jumamosi
lina kisa kizima.Akisimulia mkasa
huo, Semeni mwenye ujauzito wa
miezi 6 alisema kabla ya tukio
aligombana na mumewe akarudi
kwao kwa muda wa siku mbili
lakini walikuwa wakiwasiliana
mpaka asubuhi ya tukio ambapo
alimpigia simu kumwambia
anafuata nguo kwa vile
anakwenda kliniki.
“Nilipokuwa njiani nilimpigia simu
mume wangu, nikamwambia
nimekaribia, lakini akasema yeye
amekwenda Posta.
“Pamoja na majibu hayo,
niliamua kwenda. Nilipofika
nilikuta mlango umefungwa kwa
ndani, nikampigia simu mume
wangu, akasisitiza hakuna mtu,
yeye yupo Posta.
“Nilichungulia na kuona funguo,
nikajua kuna mtu ila hataki
kunifungulia, hapo wasiwasi
ukazidi kwamba huenda kuna
jambo linaloendelea,” alisema
Semeni.
Mwanamke huyo aliendelea
kuanika kwamba kufuatia hali
hiyo aliwaita majirani ambao
ilibidi wamtishe mtu aliye ndani
kwamba asipofungua watavunja
mlango, ndipo mlango
ukafunguliwa na kumkuta Dullah
akiwa na mwanamke mwingine
chumbani, lakini mumewe huyo
alichoropoka na kukimbia.
“Nilishtuka, nikapiga kelele ya
mshangao kutokana na kitendo
alichokifanya mume wangu,
kumleta hawara mpaka kwenye
chumba tunacholala!
“Sijaamini kilichotokea! Yule ni
mume wangu, amewezaje
kumleta mwanamke ndani ya
chumba tunacholala tena kuna
wapangaji wenzangu
wameshuhudia,” alisema
mwanamke huyo huku akilia
machozi.
Akaendelea: “Mimi hapa
nyumbani siachiwi hela ya kula,
kila siku nakula nyumbani kwetu,
nikijua labda mume wangu hana,
kumbe anamalizia kwa hawara!
Jamani inaniuma sana, kama
hivyo bora amuoe basi tuje tuishi
wote au aniache akae yeye.”
Akizungumza na gazeti hili kwa
uso ‘uliochunwa’, mwanamke
aliyedaiwa kufumaniwa,
Mwanaidi huku akiwa
‘ametaitiwa’ ndani, alijitetea
kuwa hakufahamu kama Dulla
ana mke.
“Mimi aliniambia hana mke wala
mtoto na ndiyo maana nilikubali
kuanzisha uhusiano wa kimapenzi
na yeye si vinginevyo, kama
ningejua nisingekubali kuja, kwa
hiyo siyo kosa langu,” alisema
Mwanaidi.
Baada ya hali kutulia, baba mzazi
wa Dullah ambaye anaishi jirani
aliitwa kuamua ugomvi huo na
kuamuru wote waende nyumbani
kwake ambapo aliagizia gari.
Wawili hao walipofika nyumbani
kwa mzazi huyo walimshusha
Semeni na kumtaka atangulie
ndani, alipoingia tu, nyuma
dereva alitakiwa kuondoka gari
hilo kwa kasi huku Mwanaidi
akiwemo ndani ili kumnusuru.
Baada ya kubaini ‘triki’ hiyo,
Semeni alijirusha chini kwa
hasira na kujigalagaza kisha
kulikimbiza gari hilo bila
mafanikio.
Copyright © 2013 Clickshareworld. All rights reserved.
Designed by Templateism.