ads

Friday, February 7, 2014

KISANUKO CHA MNUKO WA LEO AUNT EZEKIEL AKUTWA KATIKA FOLENI YA MAKAHABA JIJINI DAR

Muigizaji maarufu wa filam Tanzania anaejulikana kwajina la Aunt Ezekiel akutwa katika
foleni ya makahaba wa
kujiuza jijini dar…Akimbia
kumkwepa PAPARAZI kwa aibu asipigwe picha.
Lakini imekuwa ngumzo kwa watu wengi na wamekuwa wakijiuliza maswali me sana kwanini nyota huyo kuinekana katika eneo hilo tena akiwa katika vivazi vya utata.

MPIGIE KURA KISURA HAWA 13 MODEL COMPETITION

Mpagie kura mwadada huyu kisura aweze kuiwakilisha nchi yako kimataifa kwa uzuri wakipekee kwaku like picha yake ambayo inapatikana facebook katika kurasa (page) ya

MARIDADI ONLINE 2014
(Model Competition)

Namba yake ya ushiriki ni 13
Jina Hawa twaib
pamoja tunaweza kuitangaza Tanzania.

Thursday, February 6, 2014

MABOSI WA MASHIRIKA YA UMMA WAPAANDISHWA KIZIMBANI

MABOSI wa zamani wa mashirika
ya umma, Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) na Shirika la Ndege
Tanzania (ATCL), jana walipanda
kizimbani kujibu mashitaka
yanayowakabili kutokana na
uamuzi waliofanya walipokuwa
wakiongoza mashirika hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa TBS, Joseph
Masikitiko, aliieleza mahakama
kuwa, aliyekuwa Mkurugenzi wa
shirika hilo, Charles Ekelege, alitoa
msamaha wa ada ya utawala kwa
kampuni mbili bila kufuata
taratibu.
Masikitiko alidai hayo wakati
akitoa ushahidi katika kesi ya
matumizi mabaya ya madaraka na
kulisababishia shirika hilo hasara
ya Sh milioni 68, inayomkabili
Ekelege.
Ekelege anadaiwa kusababisha
hasara hiyo baada ya kuondoa ada
ya asilimia 50 ambayo ni sawa na
Sh milioni 68, kwa Kampuni za
Jaffar Mohamed Ali na Quality
Motors bila idhini ya Bodi.
Akiongozwa na Wakili Janeth
Machulya kutoka Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa
(Takukuru), Masikitiko alidai kuwa
anazifahamu kampuni hizo kwa
kuwa zilikuwa zinafanya kazi ya
ukaguzi wa magari kutoka nje kwa
niaba ya TBS.
Alidai katika kipindi cha mwaka
2007 hadi 2009 akiwa Meneja wa
Fedha na Utawala, hajawahi
kupokea wala kushughulikia barua
za maombi ya kuondolewa kwa
ada ya utawala kutoka kampuni
hizo mbili.
Kificho
Aidha alidai hakujua kama
kampuni hizo zilipewa msamaha
wa ada, hadi alipopata ripoti ya
ukaguzi wa hesabu za nje ya
mwaka 2008 hadi 2009, na kusikia
kwenye kikao cha Baraza la
Utendaji ambalo kwa sasa ni Bodi
ya Wakurugenzi, cha Septemba 30
mwaka 2011.
Alidai katika kikao hicho yeye
akiwa mualikwa, walipata taarifa
kuwa Menejimenti ilitoa msamaha
wa ada hiyo bila kupata kibali cha
bodi hiyo, ambapo bodi iliona
walitoa msamaha huo kimakosa
na kuwaonya wasirudie tena.
Alidai taratibu za kuomba
msamaha wa ada ni kuwasilisha
barua kwa Mkurugenzi, kisha iende
kwa Mhasibu Mkuu atakayeandika
dokezo kwa Mkaguzi wa Ndani
ambaye ataangalia kama amekidhi
vigezo vya kusamehewa,
itapelekwa kwa Meneja wa Fedha
kisha Mkurugenzi ataipeleka Bodi
ya Wakurugenzi kwa ajili ya
kuidhinishwa.
Akihojiwa na Wakili Majura Magafu
anayemtetea Ekelege, Masikitiko
alidai kuwa, Bodi haikusema kama
Ekelege alifanya kosa, bali ilisema
Menejimenti ilifanya makosa kwa
kutoa msamaha huo bila kupata
kibali.
Inadaiwa kuwa Machi 28, mwaka
2008 na Agosti 7, mwaka 2009,
Ekelege alitumia madaraka vibaya
na kusamehe ada kampuni mbili
kwa asilimia 50, ambayo ni sawa
na Sh milioni 68 bila idhini ya
Baraza la Utendaji kinyume na
utaratibu wa TBS pia
alilisababishia shirika hilo hasara
ya fedha hizo.
Mataka
Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya
Kuhifadhi Magari Yanayodaiwa
Kodi, Bartholomew Kijazi,
ameieleza Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu kuwa wanalidai
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Sh milioni 206.4.
Kijazi alidai hayo jana wakati
akitoa ushahidi katika kesi ya
kutumia vibaya madaraka kwa
kutangaza zabuni na ununuzi wa
magari chakavu 26, inayomkabili
Mkurugenzi wa zamani wa shirika
hilo, David Mattaka na wenzake
wawili.
Akiongozwa na Wakili wa Serikali,
Shedrack Kimaro, Kijazi alidai
kuwa wanaidai ATCL fedha hizo
kutokana na kuhifadhi magari tisa
katika ghala lao lililopo Mbagala,
tangu 1998 hadi Novemba mwaka
jana.
Alidai kuwa Desemba 16, 2011
aliandaa ripoti ya mtiririko wa
kuingiza na kutoa magari 26 ya
kampuni ya ATCL pamoja gharama
za kuhifadhi na kukarabati, baada
ya Taasisi ya Kupambana na
Kuzuia Rushwa (Takukuru) kuomba
ripoti hiyo.
Alidai wakati huo walikuwa
wanaidai ATCL dola za Marekani
118,000 kutokana na kuhifadhi
magari hayo kwa miezi 39 kwenye
ghala lao la Mbagala, ambapo kati
ya magari hayo, magari 15
yalitolewa na mengine tisa
yamebaki kutokana na kukosekana
kwa fedha za kulipa ushuru wa
forodha.
Alifafanua kuwa kwenye ghala lao
wanatoza kila gari dola 250 kwa
mwezi na hadi kufikia Novemba
mwaka jana, walikuwa wakidai
shirika hilo dola za Marekani
129,000 ambayo ni sawa na Sh
milioni 206.4.
Alidai ATCL walihifadhi magari
hayo katika ghala lao kuepuka
gharama za bandarini ambapo kwa
siku wanatoza dola za Marekani 25
hadi 40 kulingana na ukubwa wa
gari na kwa mwezi ingekuwa dola
1,200.
Mbali na Mattaka washitakiwa
wengine ni Kaimu Ofisa Mkuu wa
Kitengo cha Fedha, Elisaph Ikomba
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Ndani, William Haji.
Washitakiwa wanadaiwa kula
njama, matumizi mabaya ya
madaraka na kuisababishia Serikali
hasara ya dola 143,442.75 za
Marekani kwa kuagiza magari 26
chakavu kwa gharama ya Dola
809,300 kutoka Kampuni ya Bin
Dalmouk Motors ya Dubai bila
kutangaza zabuni ya ushindani.
Aidha wanadaiwa kuruhusu
kununuliwa kwa magari hayo bila
mkataba wa ununuzi ambao
umewekwa saini na wahusika na
kuthibitishwa na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali na kuisababishia
Serikali hasara baada ya
kushindwa kulipia kodi na
kuchukua mkopo kwa ajili ya
kuyakomboa na kuyatunza.

Wednesday, February 5, 2014

JANGA JINGINE LAZUKA SHILOLE SIKIO LA KUFA, AKANA MAAGIZO ALIYOPEWA NA MCHUNGAJI

STAA wa mduara Bongo, Zuwena
Mohamed ‘Shilole’ amedhihirisha
kuwa ni sikio la kufa baada ya
kusema yeye ni miongoni mwa
wanawake wanaojua kuchuna
mabuzi.
Kauli hiyo imechochea vigezo vya
kumfanya Shilole aonekane
hasikii kwani wiki kadhaa
zilizopita mchungaji wa kanisa
moja lililopo Ubungo, jijini Dar
ambaye hakujulikana jina lake,
alimtaka kuishi katika sura ya
kumpendeza Mungu lakini
inaonekana amempuuza.
Akizungumza na Risasi
Mchanganyiko juzi, jijini Dar es
Salaam, Shilole alisema alitunga
wimbo wa Nachuna Buzi kwa
sababu anajua kuwa wanawake
wengi ni mafundi wa tabia hiyo
akiwemo yeye mwenyewe!
“Unajua mwanamuziki unatakiwa
kuchagua wimbo ambao
unaigusa jamii nzima kwani
mambo ya kuchuna mabuzi kwa
wanawake yapo sana, hata mimi
mwenyewe ni mtaalamu wa
kuchuna mabuzi,” alisema
Shilole.
Hata hivyo alisema japokuwa ana
tabia hiyo lakini anatambua siyo
nzuri hivyo anawasihi wanawake
wengine kuachana nayo kwani
ipo siku itawaingiza matatizoni.
Mbali na mchungaji huyo, juzi
Jumapili, Mchungaji wa Kanisa la
Anglikana, Ukonga –Mazizini, Dar,
Emmanuel Kapande alimtumia
ujumbe wa watoto wa Shule ya
Jumapili (Sunday School)
nyumbani kwake kwa lengo la
kuimba na kufanya maombi.
Watoto hao walifika nyumbani
kwa Shilole, Mwananyamala -
Manjunju, wakiwa
wameongozana na walimu wao,
Jonas Timotheo, Rehema Ezra na
Catherine Libogoma.
Ujumbe huo, ulimpelekea baraka
ya maombi nyumbani kwake na
kumshauri aishi katika mazingira
yanayompendeza Mungu.
Katika hafla hiyo, vinywaji baridi
vilichukua nafasi yake huku
Shilole akipata nafasi ya
kuzungumza na watoto hao kisha
kupiga nao picha.

NYAMA YA ULIMI MPE LAAZIZI WAKO

MMMH mshaanza eti nimeisha
ingia mama Chaunabe kitanga na
njia nisiye na bleki kwenye domo
langu, wahenga wanasema
kinywa cha mkubwa kinanuka
lakini maneno hayanuki. Najua
maneno yangu ya shombo
huenda hayakufurahishi wewe
ambaye kila kukicha unabadili
wanaume na kuonekana una hila.
Shutuuu dada mwanamke tabia
babu wee, mwanamke kujua
mumeo anataka nini, mwanamke
kujituma kwenye kiwanja kifupi
cha sita kwa sita.
Unasahau cha kumvutia
mwanaume unakimbilia
kuukoboa mwili nani kakuambia
weupe mali? Basi mkaa usinge
nununuliwa!
Tena leo nakazi na wewe, nani
kakuambia weusi ni laana. Basi
leo nataka nikuambie wewe usiye
na haya uliyemaliza vipodozi
mwisho wa siku uso
unakuparama kama mchawi
mzee, unalo hilo?
Siri ya weusi maana yake ni
utamu hata zambarau tamu ni
nyeusi, zabibu tamu ni nyeusi na
hata usingizi mtamu unapatikana
usiku mweusi. Huoni Mzungu
akimuonja mswahili
anachanganyikiwa.
Wewe unajikoboa Mzungu ajipake
masizi? Acha ubwege. Nimejikuta
hata nikisahau kuelezea
nilichokikusudia kwa ajili ya
malimbukeni wachache, jivunie
weusi wako babu wewe.
Tuachane na hayo ambayo kwa
kiasi nimejikuta nikipandwa na
mzuka na kuingia kwenye mada
nyingine. Kama unabisha
mwangalie jirani yako
anayetumia mkorogo ngozi kama
kuku wa mayai aliyezeeka badala
ya kupendeza anabakia kituko
mtaani.
Acha niendelee na kilicho nitoa
nyumbani, shoga leo nilitaka
kukuelezea kitu kimoja
kuhusinana na tabia za baadhi ya
wanawake kukosa lugha tamu
ndani ya nyumba zao kushindwa
kuwalisha waume zao nyama ya
ulimi. Mwanamke unakosa lugha
tamu kwa mumeo hujui kusema
asante, hujui kusema samahani,
hujui hata kumsifia mumeo!
Mumeo akikuletea kitu
unakipokea na kuamnini ni
wajibu wake kukuletea una hiyari
ya kusema asante au kukaa
kimya. Lakini nataka nikuambie
shoga kitu kinacho mtuliza
mwanaume ni pamoja na
maneno matamu. Mfano amerudi
toka kazini baada ya kumpokea
lazima umpe pole ya kazi.
“Karibu mpenzi pole na kazi,”
akikujibu asante, mwambie.
“Yaani kila muda jicho langu
lilikuwa likitazama barabarani
utarudi saa ngapi mpenzi
wangu,” hata kama ulikuwa ndani
ukiendelea na kazi zako.
Vitu hivi humfanya mwanaume
kuamini kabisa hata anapokuwa
mbali nawe bado ulimuweka
moyoni mwako, siyo anakuja
baada ya kumpokea unabakia
kama bubu haipendezi, tumia
ulimi wako kumliwaza mumeo.
Mpo katika safari ya huba mkifika
pwani lazima mpeane pole na
asante kwa kusafiri salama,
pengine wewe umewahi mwenzio
naye anakufuata pwani msaidie
naye afike pwani na baada ya
kufika mpe pole pia kumpa
asante kwa kukusafirisha vyema
katika bahari ya huba.
Usiwe uvivu wa kuomba
msamaha unapokosa, hata kosa
lenyewe liwe dogo, kumbuka
kosa ni kosa na chanzo cha moto
ni cheche. Wapo wachache lugha
tamu huzitumia kwa muuza
genge ili apunguziwe lakini kwa
mumewe vitu hivyo havionekani.
Tumia ulimi wako kujenga
nyumba yako kumfanya mumeo
aone tofauti ya mwanamke wa
nje na mkewe ambaye kila neno
tamu na zuri humwambia
mumewe. Nyama ya ulimi
ukiitumia vizuri itakufanya kila
siku penzi lako lizidi kuwa tamu,
si wajinga waliosema sauti tamu
ilimtoa nyoka pangoni na
kumtuliza simba mwenye njaa.
Yangu si mengi kwa leo, ila
kumbuka wimbo mzuri
humbembeleza mtoto akalala.

KIDUME ANASWA AKIJIUZA ( ATOA URODA WA TIGO)

AMA kweli dunia imefika
ukingoni! Ile Oparesheni Fichua
Maovu (OFM) ya Global
Publishers, bado ipo kazini
ikishirikiana na polisi ambapo
safari hii imeibuka na kigongo
cha aina yake baada ya kumnasa
‘mwanaume tata’ akijihusisha na
ukahaba, Risasi Mchanganyiko
lina mzigo kamili.
Ikiwa kwenye fumuafumua ya
magenge ya ngono maeneo ya
Kahumba mjini Morogoro hivi
karibuni, OFM kwa mwaliko wa
jeshi la polisi, ilipigwa na butwaa
baada ya kukutana uso kwa uso
na mwanaume huyo aliyekuwa
amejumuika katikati ya kundi la
madadapoa naye akifanya kama
wao.
Mbali na jamaa huyo ambaye jina
lake halikupatikana, baadaye
ilibainika kuwa kulikuwa na
wenzake wawili ambao ilikuwa
vigumu kuwatambua kufuatia
kujiremba kupita hata wanawake
wenyewe.
Kuna madai kwamba kijana huyo
aliyekadiriwa kuwa na umri wa
kati ya miaka 20 - 24 ni mtoto wa
kigogo serikalini na amekuwa
akijichanganya na madadapoa
hao kwa muda mrefu.
Mara baada ya kunaswa, kijana
huyo aliangua kilio huku akidai
kuumbuka kwani familia yake
wakiiona picha yake
hawatamwelewa.
“Naombeni tumalizane hapahapa
kwani nyumbani hawafahamu
kuwa nipo hapa muda huu. Hii ni
kesi kubwa kwangu nisaidieni,”
alisikika kijana huyo.
Hata hivyo, pamoja na kilio
hicho, polisi hawakumwelewa,
alibebwa juujuu na kuingizwa
katika karandinga kisha kutupwa
nyuma ya nondo za mahabusu
kusubiri sheria kuchukua mkondo
wake.
Wakazi wa maeneo hayo
walikuwa wakilalamika mara kwa
mara kutokana na kurundikana
kwa makahaba mahali hapo na
kusababisha uchafuzi wa
mazingira kwa kutupa ovyo
mipira ya kiume (kondom).
Katika msako huo, wanaume hao
watatu walijumuishwa na
wanawake 20 waliokamatwa
wakijihusisha na biashara
haramu ya kuuza miili.
-GPL

LAANA BINTI APIGA PICHA ZA UTUPU NA KUZIACHIA FACEBOOK LOOH!!

Amepiga picha na kuzisambaza
facebook mungu atunusuru na
haya majanga yakina dada
ambao wana piga picha za uchi
na kuweka kwenye mitandao ya
kijamii JINA analo tumia
facebook ni JESSICA KIKUMBI
TAFADHALI KURINGANA NA
MAADILI KUANGALIA PICHA
SHARITI UWE NA UMRI +18 NA

HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....!

Wapenzi na wanandoa wengi hivi
leo wanapoingia kitandani tayari
kwa kuianza safari ya kupeana haki
zao za msingi hushindwa kufurahia
tendo na hasa hali hii hujitokezwa
kwa wanawake kwani mwanaume
huwa na haraka iliyopitiliza!
Mwanaume atamkumbatia na
kumbusu mwanamke kwa muda
mfupi na kabla hata hamasa ya
mapenzi ya mwanamke ahaijashika
hatama, atamwingilia na ndani ya
dakika sekunde ama dakika
zisizozidi 3, mwanamme hufika
mshindo.
Katika hali ya kusikitisha baada ya
mwanaume kujitosheleza hujongea
pembeni bila kujali mwenza wake
hajafika mwisho wa safari hali
inayosababisha mwanamke
kupoteza hamu ya tendo endapo
endapo tabia hiyo ya mwanaume
itaendelea.
Kunahatua nne muhimu ambazo
wapendanao wakizishika na
kuzitekeleza ipasavyo basi
watafanikiwa kujitosheleza kila
wanapokutana na kwa hakika
watakuwa miongoni mwa watu
wachache wanaofurahia faragha
kila wakutanapo!
Hatua ya kwanza ni
kusameheana:
Wanandoa wengi hushindwa
kupata raha ya mlo wa usiku
kutokana na kushindwa kumaliza
tofauti zao kabla ya giza
halijaingia, mgogoro wowote baina
ya wapendanao ni lazima
umalizwe kabla ya kukutana kwa
ajili ya mlo wa usiku. Hii husaidia
kuondoa kinyongo miongoni mwao
na kuwafanya mioyo yao igubikwe
na upendo ambao humfanya
ahamasike kunako majambo!
Hivyo basi endapo unataka
kufurahia mambo fulani hakikisha
unamaliza tofauti, ombaneni
msamaha na samehaneni kwa
dhati kwani kwa kufanya hivyo
kutawasaidia muwapo faragha
kufurahia kile mnachokifanya kwa
kuwa mtakuwa mmemalzia tofauti
zenu.
Hatua ya pili ni mchezo ya
mahaba:
Mashamsham hunoga na kupamba
moto kiasi cha kumfanya yoyote
aliye kwenye uwanya wa raha
kusahau kwa muda shida na
matatizo yanayomuandama pale
anapokutana an mtu anayeweza
kumpagawisha kwa michezo ya
mahaba kabla ya kuianza safari
yenyewe!
Michezo hii husaidia kuamzsha
hamasa na muhemko baina ya
wapendanao, hivyo ili wapendanao
waweze kufika mwisho wa safari
pamoja na kila mmoja alidhike na
udereva wa mwenzake
uliowafikisha safari yao lazima
watumiye muda wakutosha katika
michozo yakimahaba!
Hata hivyo kila mmoja wenu
anapaswa kuujua mwili wa
mwenza wake. Mwili wa
mwanaume ni rahisi kuuelewa
kwani una sehemu moja kuu
ambayo ni kama kiini cha
muhemko na msisimko wa
mapenzi. Sehemu hiyo ni uume.
Hivyo endapo mwanamke yoyote
atatumia muda wakutosha
kuhangaika na sehemu hiyo basi
mambo huwa safi kwa upande wa
mwanaume.
Mwili wa mwanamke una shughuli
pevu kubaini sehemu zenye
ambazo huamsha hisia za mapenzi
na ndiyo maana wanaume wengi
hushindwa kuwafikisha mwisho wa
safari wapenzi wao. Kiini cha hisia
za mapenzi kwa mwanamke ziko
kwenye kipegere G (namaanisha
critoris wadu, haya ni mambo ya
infenizimu tu). Kipegere G kipo nje
ya uke ambapo wataalamu hudai
kuwa kipo sentimita 4 kutioka
ukeni.
Wanaume wengi wanaelewa hili
lakini walio wengi wamegubikwa
na imani potofu kuwa, kwa
kuingiza kidole ukeni watafanikiwa
kuinua hamasa ya za wenza wao
kutaka kuanzisha safari jambo
ambalo si kweli, kwani wanawake
wengi hujisikia vibaya kuingizwa
vidole ukeni kutokana na ukweli
kwamba kucha zinabeba uchafu na
bakteria wengi ambao
huwasababishia kupata fangasi!
Hivyo basi, endapo wewe ni
miongoni mwa wanaume
waliokuwa wakiaminin dhana hii
nataka nikujulishe kuwa, ukitaka
kumpa msisimko uliotukuka
mwenza wako usiangaike kuingiza
kidole chote ukeni badala yake
hakikisha unatumia kidole chako
(hakikisha si kikavu) kucheza na
sehemu ya nje ya uke ambapo
utakutana na kipegere G na lips za
ndani. Hata hivyo usisahamu
kuhangaika na uke pia lakini hasa
shughulika na sehemu za nje!
MUHIMU KUJUA: Mwanaume
huahamasika kwa sekunde kadhaa
lakini mwanamke humchukua
takriban dakika 20 kuweza
kuamsha hisia zake na kumfanya
awe tayari kwa kuianza safari!
Hivyo, mwanaume mwenye busara
yaani asiye mbinafsi huakikisha
anatumia muda wakutosha
kumuuanda mwenza wake kabla ya
kuanza safari! Hivyo mwanaume
anapaswa kunza michezo ya
mahaba kwa kuzingatia hatua tatu
muhimu ambazo ni:-
Sehemu ya juu:
Wanume wengi kutokana ana
haraka zao hukimbilia sehemu ya
chini ya mwili wa mwanamke
yaani kunako na kuanza ama
kupapasa kwa kidole chake ama
ulimi na baada ya sekunde chache
huanza kumwingilia mwanamke,
lakini mwanaume mwenye kumjali
ampendaye na mwenye nia hasa
yakumfikisha kwenye kilele cha
raha huwa hana papara
huhakikisha anamhagi na kumpiga
mabusu sehemu ya juu ya mwili
wake yaani mdomoni, shingoni,
kwenye matiti, chuchu etc.
Hata hivyo, si wanawake wote
wako sawa, kuna amabo hufurahia
kutomaswa maziwa yao huku
wengine wakichukizwa kutokana na
sababu mbalimbali kwa mfano
kama mwanaume ni mtu
wamitungi ama mvuta sigara
mara nyingi kinywa chake hutoa
harufu mbaya hivyo huwa vigumu
kwa mwanamke asiyependezewa
na matumizi ya vitu hivyo
kufurahia kupigwa denda!
Kimsingi mwanamke kama kweli
unampenda mpenzi wako na
unataka ufurahie majambozi
anayokupa hakikisha unakuwa
muwazi kwa kuanza na
kumuonyesha sehemu zinazokupa
hamasa ya kufanya mapenzi, si
lazima ushike mkono wake na
kuupeleka kunako hiyo sehemu!
Hakikisha pindi mwanaume
anapokugusa sehemu
inayokusisimua unamwonyesha
wazi kuwa hapo unasikia utamu
yaani kama miguno ilikuwa haitoki
hakikisha inaanza toka, kama
pumzi zilikuwa zatoka kawaida basi
zianze toka isivyo kawaida,
nachomaanisha hapa ni kuwa
unapaswa kuonyesha umepagawa
kwa raha unayopata basi kwa
mwanaume aliye kamili hatasita
kuishughulikia kikamilifu sehemu
hiyo!
Sehemu ya chini:
Baada ya kumtomasa kiasi cha
kutosha sehemu ya juu ya
mwanamke, mwanamke huhitaji
kutomaswa sehemu ya chini na
hapa ndipo ambapo unaweza
kuhisi anataka kuingilia mana
huanza ama kujishikasiika sehemu
za chini ama hukupeleka maeneo
yake nyeti upate kumwingilia kwani
huwa amehamasika na ilim kujua
kama amaehamasika basi uke
wake huwa unamajimaji ambayo
hutoka kwa ajili ya kulainisha nyia
ya kupita bwanamkubwa yaani
uume.
Hata hivyo, ili mchezo uwe mtamu
mwanaume anapaswa kuhakikisha
anatumia dakika kadhaa kuuchezea
uke na kufuatia kinena. Hapa
ieleweke kuwa kuna wanawake
baada ya mizuka kuwapanda
hutokwa na majimaji mengi
sehemu zao za siri hivyo endapo
mwanaume ukikutana na hali hiyo
usishutuke jua mzuka imempanda
mpenzi wako tu na si vinginevyo!
Katika kuchezea sehemu zake za
siri mwanaume anapaswa kujua
kuwa kuna wanake wanapenda
chezewa kinena pekee na wengine
hupenda mwanaume atumie ulimi
ama akidole chake (kisiwe kikavu)
kuingiza ukeni huku kidole kingine
kikitomasa kinena hali
inayomsisimua mwanamke. Hivyo
mwanamke anapaswa kuwa
muwazi nini anapenda kufanyiwa!
Katika kipindi hiki mwanamke naye
anatakiwa kutoa ushirikianao wa
miguno na viuno vya hapa na pale
kuashiria anapata raha na
asisahau mptomasa mwanaume,
lakini ikumbukwe kuwa
mwanaume ana sehemu kuu moja
inayomtia wazimu ambayo ni
uume wake hivyo ni rahisi kwa
mwanaume kufika mshindo hata
kabla ya tendon a hapo ndipo
tatizo huibuka kwani wengine
baada ya tendo moja huwa
hawana uwezo wakurudia
mzunguko wa pili!
Nini mwanaume anapashwa
kufanya sasa ili kuhakikisha
hamalizi mzungoko haraka?
Anapaswa kuwa muwazi kwa
mwenza wake endapo mwenza
wake atakuwa anamshika sehemu
ambayo inamnyegesha sana na
kumfanya ajisikie kumaliza
biashara basi amueleze wazi kuwa
aiache sehemu hiyo kwa muda ili
uweze kudumu kunako
majambozi!!
Hata siku moja msifanye mahaba
kimya kimya! Simaanishi mpige
mikelele hadi iwe kero kwa
majirani na nk, elezenaneni kwa
sauti za mahaba nini kila mmoja
wenu anapenda mwenzi wake
afanyiwe na mwenza wake.
Hatua ya tatu:
Kuingiliana kimwili
Mwanaume anapaswa kuahkikisha
amasa za mapenzi za mwanamke
zimeamka kabla ya kumwingilia.
Wanaume wengi kutokana na
papara hujikuta wanawaingilia
wenza wao hata kabla
hawajahamasika na hatimaye
kumaliza tendo pasipo kuwafikisha
kileleni na hili ni tatizo la kawaida
kwa wapenzi wanaokutana kwa
mara ya kwanza na has
amwanamke akiwa na zile nataka
sitaki yani atasumbuana na
mwanaume weeeee na hatimaye
hadi dume lifanikiwe kumwingilia
kimwili inakuwa kama mbakano tu!
Hivyo basi, mwanaume unapaswa
kujua kweli mpenzi wako yuko
tayari kwa tendo la ndoa na utajua
kwa kungalia kwanza mashavu ya
uke wake kama yamekakamaa na
kuongezeka ukubwa huku kinembe
chake kikionyesha kukaza na
mwanamke akifikia hali hii basi
mwanaume huweza kuingiza
uuume wake ambao umesimama
kiurahisi kwani kuta za uke
zitakuwa na ute unaoteleza huku
uume nao ukiwa na ute unaotoka
sehemu ya mbele kabisa hali
inayowafanya wapendanao
kufurahia tendo kwani
hawataumizana!

MAPENZI MATAMU YANA HITAJI UBUNIFU KATIKA MAPENZI KUONGEZA LADHA KWA MWENZI WAKO

Ukweli ni kwamba kitu chochote
tunachokifanya katika maisha
yetu kinahitaji ubunifu ili
kukiboresha kuwa kizuri zaidi
vivyo hivyo katika mapenzi
mwanamke na mwanamume
wanahitajika kuwa wabunifu
katika mambo mbalimbali mfano
kwa mwanamke ambapo kwa
asilimia nyingi inasemekana
mwanamke akiolewa na kupata
mtoto wengi wao wanajisahau
katika mapenzi kama kupika,
usafi wa nyumba na mwili,
matumizi mabaya ya pesa,
mahaba motomoto na vitu
vingine vingi vinavyoendana na
hivyo JAMBO LA MSINGI
TUKUMBUKE KUWA WABUNIFU
naichukia sana kauli ya kusema
"Mwanamume ama mwanamke
hata umfanyie nini haridhiki" hii
ni kauli potofu na ni kujikatisha
tamaa na mwisho wa siku
kujibweteka na kumpoteza
mwenza wako MAPENZI MATAMU
YANAHITAJI UBUNIFU

HAYA NDIO MAISHA YA DIAMOND KILA SIKU ASUBUHI:

msanii huyu amekuwaakijiimalisha vyema katika mazoezi ya mwili kila anapo hamka asubuhi tazama matukio katika picha

SIAMINI NINA MWAKA KWENYE NDOA LEO NDIO NINAGUNDUA MKE WANGU ANA TATTOO YA JINA LA MWANAUME MWINGINE

Habari Wadau wa Udaku...
Leo nimeuzika sana wadau
Asubuhi wakati napata morning
Glory kwa Mke wangu
nimegundua Kwenye Titi Sehemu
ya chini ana Tatto imeandikwa "I
lov u James" kwa Maandishi
Madogo sana kama haupo makini
unaweza usiyaone...
Nimekaa nae Mwaka mzima Leo
ndio nakuja ona Nilivyojaribu
kumuuliza anakuwa mkali na
kusema ni jina la Ex Wake kabla
hajakutana na Mimi....Wadau
Hapo Mnanishaurije ? Kila
nikiona hiyo Tatoo Am Sure Mood
zitakuwa zikiniisha

VIJANA WAHIMIZWA KUJISHUGHULISHA NA KILIMO MKOANI MBEYA

SEKTA za elimu na kilimo ni
miongoni mwa zile zilizoingizwa
katika mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (BRN).
Lengo la serikali katika mpango
huo ni kuona sekta lengwa
zinapiga hatua za haraka na kuwa
na tija kwa watanzania. Ni kwa
kutambua umuhimu wa mpango
huo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,
Abbas Kandoro aliamua kufanya
ziara ya siku tatu wilayani Mbozi ili
kuona maandalizi ya utekelezaji wa
mpango wilayani hapo.
Dhana iliyopo ni kwamba mpango
huo, BRN, hauwezi kufanikiwa
iwapo hakutakuwa na maandalizi
stahiki ambayo pia kama ulivyo
mkakati wenyewe lazima nayo
yafanyika kwa haraka zaidi
sambamba na usimamizi mzuri wa
mpango mzima. Akiwa wilayani
hapa, Kandoro alijikita zaidi katika
sekta mbili hizo, elimu na kilimo
ambazo ni nguzo muhimu katika
suala zima la maendeleo kwa
wananchi wa wilaya hii.
Ukaguzi wa miundombinu ya
kilimo hususani maghala ya
chakula, matumizi sahihi ya pesa
zinazotolewa na serikali pamoja na
maabara mashuleni ni miongoni
mwa mambo aliyoyazingatia
kwenye ziara yake.
Kujiunga katika vikundi
Kandoro aliwahimiza wakulima
wilayani hapa kujiunga katika
vyama vya ushirika kwa kuwa ni
muhimu katika kuwasaidia kupiga
hatua kimaendeleo.Kwamba mbali
na ukweli kuwa umoja na nguvu,
vikundi vya ushirika vinakopesheka
kirahisi tofauti na mtu anapokuwa
mmoja mmoja.
Aliwataka wakulima kutokatishwa
tamaa na kasoro za viongozi
wachache wanaokwamisha vikundi
vyao au vyama vya ushirika
kushindwa kufikia malengo ya
kuwasaidia wanachama wake.
Alisema jambo muhimu kwa
wakulima ni kutambua kuwa
vyama vya ushirika pia vinaweza
kuwatetea hata katika kupata
maslahi stahiki kwa kuuza mazao
yao. Kupitia vyama vya ushirika,
Kandoro alisema serikali mkoani
hapa imelenga kuhakikisha mfumo
wa stakabadhi ghalani unatumika
na kuwawezesha wakulima
kuondokana na kutapeliwa na
wafanyabiashara wanaokwenda
kuwalaghai majumbani wakiwataka
kuwauzia mazao kwa bei rahisi.
Akizungumza na wanachama wa
kikundi cha wakulima wa kahawa
cha Iganda kilichopo kijijini Isansa,
Kandoro alisisitiza msimamo wa
serikali ya mkoa kuona kwamba
mkulima hauzi kahawa mbichi
badala yake aikaushe mwenyewe.
“Stakabadhi ghalani inaambatana
na uwepo wa maghala.
Ndiyo sababu tumenuia kukarabati
jumla ya maghala 54 kwa wilaya
yote ya Mbozi na kwa kuanza
tutakarabati kwanza maghala 24.
“Tunataka msimu wa kuvuna
kahawa unapoanza mfumo huu
uwe umeanza kufanya kazi. Kwa
maana hiyo kahawa itakayovunwa
itakusanywa kwa mfumo huo na
kuhifadhiwa katika maghala
haya.“Tunataka wakulima wawe na
sauti itakayowawezesha kunufaika
na jasho lao,” alisisitiza.
Mkuu huyo wa mkoa amesema
ataangalia uwezekano wa
kukisaidia kikundi hicho kupata
mashine kubwa ya kukoboa
kahawa kwa kuwa iliyopo hivi sasa
ina uwezo mdogo wa kufanya kazi,
hali inayosababisha baadhi ya
wakulima kwenda kwingineko
kukoboa kahawa yao.
Vijana na kilimo
Katika ziara hiyo, Kandoro
aliwapongeza wakazi Mbozi kwa
kuendelea kujituma katika kilimo
huku akisema kwamba ni lazima
jamii ikubali kuwa kilimo kitabaki
kuwa ajira kubwa ya watanzania
na hivyo kinachotakiwa ni serikali
kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali kuzidi kuboresha
miundombinu yake.
Mkuu huyo wa mkoa anaamini
kwamba miundombinu ikiwa bora
wakulima nao watafanya shughuli
zao kwa urahisi zaidi. “Na vijana
wanapaswa watambue kuwa si
kweli mijini kuna maisha bora.
Wengi wanadanganyika kukimbilia
huko na kuacha ajira hii.
Wanakwenda kuishi maisha
magumu mijini na kuishia
kujiingiza kwenye biashara zisizo
na tija wakati wangeweza kujiajiri
vijijini kwao kwa kulima mazao
kibiashara,” alisema.
Alisema ni vyema sasa jamii ikawa
na mtazamo kuwa vijana
wanaweza kunufaika na kilimo
wakiamua na kuwa serikali ya
mkoa itazidi kuandaa mikakati
mbalimbali ya kufanya kilimo kiwe
na tija.
“Nawapongeza kwa kuona mnazidi
kujituma. Mazao yanastawi vizuri
hali inayoonesha kwamba
mmetumia utaalamu. Tutazidi
kuleta wataalamu kila
inapowezekana ili waweze
kusaidiana nanyi,” alisema.
Kujaribu mazao mengine
Katika kijiji cha Senjele, mkuu
huyo wa mkoa alibaini kuwa ardhi
na hali ya hewa ya ukanda wa juu
wa wilaya ya Mbozi usiokubali
kilimo cha kahawa unaweza
kustawisha zao la korosho.
Hii ilikuja baada ya kushuhudia
miti ya korosho ikiwa imestawi
vyema katika viunga vya Shule ya
Sekondari ya Shikula.
“Halmashauri kwa kushirikiana na
ofisi ya kilimo mkoa angalieni
namna mnavyoweza kuhimiza
kilimo cha korosho katika ukanda
huu. Hawa hawajapanda kama
urembo hapa.Wasaidieni pia dawa
ya kupulizia hawa waliokwisha
anza. Ni zao linaloweza kuinua
uchumi wa Wanambozi
tukilihamasisha kulimwa,”
anasema.
Ufisadi na kutowajibika
Hata hivyo, Kandoro aliweza
kubaini kasoro kadhaa zinazoweza
kukwamisha matokeo ya haraka
katika sekta ya kilimo wilayani
Mbozi. Kasoro hizo ni matumizi
mabovu ya fedha za serikali katika
utekelezaji wa miradi ya
miundombinu ya kilimo pamoja na
baadhi ya wataalamu kutowajibika
ipasavyo.
Moja ya maeneo yaliyobainika
kuwepo na ufujaji wa fedha za
serikali ni katika mradi wa
umwagiliaji wa Iyula B uliopo
katika kata ya Iyula. Hapa Kandoro
alibaini kuwepo na upotevu wa
fedha kiasi cha zaidi ya Sh milioni
115.
Awali katika taarifa iliyosomwa na
ofisa kilimo na mifugo wa kata ya
Iyula, Khalid Mchomvu
alibainishwa kuwa ujenzi wa banio
la maji la mradi huo umegharimu
kiasi cha Sh 255,710,000 na
unatarajia kunufaisha jumla ya
kaya 268 zitakazolima ekari 210 za
kilimo cha umwagiliaji zikiwemo
ekari mbili zilizotengwa kwa ajili ya
vijana.
Kilichomkera mkuu wa mkoa ni
baada ya Ofisa Kilimo na Mifugo
wa Halmashauri ya Wilaya, Richard
Siliri, kueleza kuwa zinahitajika
fedha nyingine kwa ajili ya
kupasua kwa baruti jiwe kubwa
linalozuia maji kupita kwenye
mfereji pamoja na kuusakafia
mfereji huo wenye urefu wa
kilometa tisa.
Hapo ndipo mkuu wa mkoa
aliposema hakuna sababu ya
mradi huo kuombewa fedha
nyingine wakati hesabu za
kiukaguzi zinabainisha kuwa kutoka
mfuko wa maendeleo ya kilimo wa
wilaya (DADPs) walikwisha pewa
zaidi ya Sh milioni 250 na
walizotumia hadi mradi ulipofikia
ambapo ujenzi wa banio
umekamilika ni Sh milioni 134.
Fedha hizo walipewa kwa awamu
mbili ambapo awamu ya kwanza
walipewa zaidi ya Sh milioni 115
na ya pili wakapewa zaidi ya Sh
milioni 134. Akahoji ni kwa nini
taarifa ya ukaguzi inayobainisha
matumizi ya Sh milioni 134 hadi
mradi huo ulipofikia zinatofautiana
na taarifa za watendaji hao.
Akasema kuna uwezekano mkubwa
kuwa fedha hizo zilitafunwa na
wachache kwa manufaa yao.
“Nasema fedha mnazo kwa mujibu
wa taarifa za ukaguzi. Mnaweza
kukamilisha ujenzi wa mfereji na
zikabaki. Mliomba jumla ya Sh
milioni 340 kwa ajili ya utekelezaji
wa mradi na tayari mmepewa zaidi
ya Sh milioni 250 na mmetumia Sh
milioni 134 hizi nyingine ziko
wapi?” Akahoji.
Akaendelea: “Nawahakikishia
ndugu zangu wananchi kuwa
tutashirikiana kuhakikisha fedha
zenu zinajulikana zilikokwenda.
Hatuwezi kukubali miradi ya
serikali kukwama kutokana na
wajanja wachache kujinufaisha.”
Akizungumza na waandishi wa
habari, mwenyekiti wa kamati ya
usimamizi wa mradi huo, Jua
Mwamlima, alisema fedha za
mradi zilizokwishatolewa kwenye
akaunti ni zaidi ya Sh milioni 250
na zilizosalia kwenye akaunti hiyo
ni Sh 500,000 pekee.
Akasema wanachojua wanakamati
ni kuwa fedha zote zilitumika
kwenye mradi hadi ulipofikia hivi
sasa kwa kuwa nyaraka zote za
malipo zilikuwa zikiandaliwa na
kufanywa na maofisa wa ngazi ya
juu na wao kupelekewa kwa ajili ya
kutia saini pekee. Ubadhirifu
mwingine ukabainika katika kijiji
cha Msiha.
Sh milioni 100 zilizotolewa na
serikali kwa ajili ya ujenzi wa
bwawa la maji ya kutumia
majumbani pamoja na kilimo cha
umwagiliaji katika kijiji hicho
haijulikani zilipo. Kufika kwa
Kandoro kijijini hapo kulilenga
kuona namna miundombinu ya
bwawa hilo ilivyojengwa akijua
kwamba lilikwishafikia hatua nzuri
tayari kuanza kuwanufaisha
wananchi walengwa wanaokabiliwa
na uhaba wa maji kwa ajili ya
matumizi ya majumbani na pia
kwa ajili ya kilimo.
Baada ya kufika na kukuta hakuna
lolote lililofanyika ndipo mkuu
huyo wa mkoa aligeuka mbogo na
kutaka ofisi ya kilimo imueleze
ilimpeleka hapo kufanya nini
wakati hakuna miundombinu na
pia akataka kujua fedha zote
walizopewa zilifanya kazi gani.
“Sasa hapa naomba mnieleze
mmenileta kufanya nini?
Mimi nilijua kuna miundombinu
iliyokwishajengwa tayari kwani ni
muda mrefu tangu mmepewa
fedha. Je, mlinileta kuja kushangaa
mandhari ya pori hili na kusimama
simama tu kama hivi?” akahoji.
Kwa mujibu wa Kandoro, ofisi ya
kilimo wilayani hapo katika mwaka
wa fedha 2010/2011 ilipewa kiasi
cha Sh milioni 40, na mwaka wa
fedha 2012/2013 ikapewa kiasi cha
Sh milioni 60 lakini fedha hizo
hazijulikani ziliko na hakuna kazi
yoyote iliyoanza kufanyika mpaka
anafika eneo la mradi.
“Mimi nilitaraji leo nakuja kuona
miundombinu iliyolenga kusaidia
kuweka mtiririko mzuri wa maji ili
maji hayo yasaidie kulima kwa
uhakika. Hakuna kitu hapa! Wewe
mwenyewe hauna uhakika na
kilichoendelea katika Sh milioni
100 zote zilizoletwa,” akasema
Kandoro akimwambia Ofisa kilimo
na mifugo wa wilaya ya Mbozi,
Richard Sirili.
“Hii haikubaliki hata kidogo na
nasema lazima tuchukue hatua
hata polisi watu watapelekwa.
Nimeshtuka pesa ni nyingi mno.
Serikali inaleta pesa hakuna
kinachofanyika. Hatuwezi kwenda
kwa mwendo huu ndugu zangu,”
alisisitiza.
Mmoja wa wakazi wa kijiji cha
Msiha, Mawazo Mwamlenga
alisema bwawa hilo linasubiriwa
kwa hamu kubwa na wakazi wa
kijiji hicho kutokana na kukabiliana
na uhaba mkubwa wa maji kwa
ajili ya matumizi ya majumbani na
kuendeshea kilimo cha
umwagiliaji, alichosema kitaweza
kuwakomboa kuondokana na
umasikini.
Kuendelea kusuasua kwa ujenzi wa
bwawa hilo ilhali wakazi wanayo
taarifa kuwa serikali ilikwishatoa
fedha kunaonesha kama kwamba
wakazi hao wametumika kama
mtaji wa kunufaisha wajanja
wachache wasio na huruma kwao.
Katika kata ya Myovizi, Kandoro
alikutana pia na malalamiko
yanayokwamisha maendeleo ya
kilimo.
Kubwa ni mtaalamu wa kilimo
kulalamikiwa kwa kutowajibika
ipasavyo kwa wananchi aliopewa
jukumu la kuwatumikia kutokana
na utaalamu wake. Ofisa huyo,
Rehema Mwandurusa, mbali na
kudaiwa kuishi mbali na kituo
chake cha kazi wakazi wa kijiji cha
Ichesa katika kata hiyo wanasema
wamekuwa wakiishi kama hawana
mtaalamu wa kilimo hivyo
kulazimika kuendesha shughuli zao
pasipo utaalamu wowote.
Mwenyekiti wa halmashauri wa
wilaya ya Mbozi, Eliki Ambakisye
pia akakiri ofisa huyo kukaidi agizo
la kumtaka aishi eneo lake la kazi
na badala yake amekuwa akiishi
katika mji mdogo wa Mlowo uliopo
takribani kilomita kumi kutoka
eneo hilo. Akasema kwa kuishi
mbali na eneo la kazi ofisa huyo
amekuwa akifika kwa kusuasua
sana katika eneo hilo, hivyo uwepo
wake hauwasaidii wananchi
aliopewa dhamana ya
kuwatumikia.
Kufuatia malalamiko hayo,
Kandoro akamuagiza ofisa huyo
kuchagua jambo moja kati ya kazi
na kuishi anakotaka yeye ili nafasi
yake apewe mtu aliye na utayari
wa kuishi katika eneo lake la kazi
ili kuwatumikia wananchi.
Uhaba kidato cha sita
Upande wa sekta ya elimu nao
ulikuwa na yake. Cha kwanza
kilichojitokeza ni uhaba wa shule
za sekondari kwa ajili ya elimu ya
kidato cha tano na sita.Katika
eneo hilo, Kandoro alifurahishwa
na uamuzi wa wakazi wa kata ya
Myovizi kuongeza vyumba vya
madarasa na kujenga mabweni
kwa ajili ya kidato cha tano na
sita. Mkuu huyo wa mkoa aliahidi
kuchangia Sh 500,000 kwa ajili ya
ujenzi wa vyumba vya madarasa
unaoendelea.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka pia
wanafunzi wanaosoma michepuo
ya sayansi katika shule zilizo
wilayani hapo kutambua kuwa
wanalo jukumu la kuikomboa nchi
kuondokana na changamoto ya
uhaba wa walimu wa masomo ya
sayansi. Akaziagiza halmashauri
kuziwezesha shule zilizo na
maabara kwa kuzifungia umeme
wa mionzi ya jua ili kutoa fursa
kwa wanafunzi kujifunzwa kwa
vitendo wakati wowote.
Mimba mashuleni
Lakini suala la mimba kwa
wanafunzi likaonekana kuwa ni
changamoto nyingine inayopaswa
kuendelea kutafutiwa ufumbuzi.
Mkuu wa mkoa aliagiza hatua za
kisheria kuchukuliwa dhidi ya
wahusika wa mimba za wanafunzi,
ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha
wazazi wanaokwamisha kesi za
mimba kutofanyika kisheria.
Ni katika kulipa uzito jambo hili
alitoa muda wa siku saba kwa
ofisa mtendaji wa kata ya Nanyala,
Theofrida Hankungwe kuhakikisha
amewasilisha taarifa za hatua
zilizochukuliwa kwa wanafunzi
watano wa kike waliopata mimba
mwaka 2013 katika Shule ya
Sekondari ya Shikula.
Agizo hilo pia lilitolewa kwa mkuu
wa shule hiyo, Chonge Dafa
ambapo kwa pamoja viongozi hao
wanapaswa kueleza ni hatua zipi
zilichukuliwa kwa wanafunzi
waliopata mimba na pia
waliosababisha. Wanafunzi hao ni
pamoja na mmoja aliyepewa
mimba na mwanafunzi mwenzake
ambapo wote walifukuzwa shule.
“Kumekuwa na mchezo wa baadhi
ya wazazi kumaliza kesi za mimba
kiundugu kwa kupeana pesa au
mali nyingine badala ya kupeleka
kesi hizo mahali husika ili hatua za
kisheria ziweze kuchukuliwa.
Matokeo ya kumalizwa kwa kesi
hizo kienyeji imekuwa ni kuendelea
kwa wimbi la mimba mashuleni na
kusababisha watoto wa kike
kukosa haki yao ya msingi ya
kupata elimu.
“Ndugu zangu lazima tukubali
kuwa ukimwelimisha mtoto wa
kike umeelimisha familia yake
yote. Sisi akina baba mara nyingi
hatukai na watoto nyumbani. Ni
akina mama wanaoshinda nao na
kuwapa malezi ya karibu sasa
kama mama akiwa na elimu ni
wazi atailea familia yake katika
mazingira bora zaidi,” alisema.

WACHINA WALIO KUTWA NA MENO YA TEMBO YENYE THAMANI YA TSH.BILIONI 5.4 WAFANYA JARIBIA LA KUTUO RUSHWA ILI WAACHIWE HURU

RAIA watatu wa China
wanaokabiliwa na kesi ya kukutwa
na meno ya tembo yenye thamani
ya Sh bilioni 5.4, wanadaiwa
kujaribu kutoa rushwa ya Sh
milioni 30.2 kwa askari ili
wasifunguliwe mashitaka.
Wakili Mwandamizi wa Serikali,
Faraja Nchimbi alidai hayo jana
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu wakati akiwasomea
washitakiwa maelezo ya awali.
Alidai Novemba 2 mwaka jana
katika eneo la Kifaru Mikocheni B,
washitakiwa walikamatwa na
askari wakiwa na vipande 706 vya
meno ya tembo pamoja na ganda
la risasi.
Nchimbi alidai washitakiwa hao,
walikiri kumiliki vitu hivyo bila
kibali na kudai watawapa askari
hao na baadhi ya wananchi
waliokuwa katika eneo la tukio Sh
milioni 30.2 ili wasifunguliwe
mashitaka.
Hata hivyo, askari hao, Mrakibu
wa Polisi (ASP) Heri Mugaye,
Sajenti Gerwin, askari wa
Wanyamapori Simon Saye na
wananchi waliokuwa eneo la tukio,
walikataa kupokea fedha hizo na
kuwafikisha kituo cha Polisi na
kuwafungulia mashitaka.
Aliendelea kudai kuwa katika
maelezo ya onyo waliyotoa kituo
cha Polisi, washitakiwa hao walikiri
kukutwa na nyara hizo na risasi
bila kuwa na kibali cha umiliki
kutoka mamlaka husika.
Hata hivyo, jana baada ya
kusomewa maelezo ya awali,
washitakiwa hao waliokuwa
wanatafsiriwa na mkalimani,
walikana maelezo hayo, lakini
walikiri majina, uraia na umri wao.
Washitakiwa katika kesi hiyo ni
Huang Gin (50), Xu Fujie (22) na
Chen Jinzhan (31), walifikishwa
mahakamani hapo Novemba 8
mwaka jana, wakikabiliwa na
shitaka moja, kabla ya kuongezewa
mashitaka mawili.
Awali, Wakili Mwandamizi wa
Serikali, Tumaini Kweka,
aliwasomea upya washitakiwa
mashitaka yao baada ya kufanya
marekebisho kwa kuongeza
mashitaka mawili .
Alidai kuwa Novemba 2, mwaka
jana katika mtaa wa Kifaru
Mikocheni B, washitakiwa
walikamatwa wakiwa na vipande
706 vya meno ya tembo vyenye
uzito wa kilo 1,889 vyote vikiwa na
thamani hiyo, mali ya Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi
wa Wanyamapori.
Alidai katika mashitaka mengine,
wanadaiwa kutaka kutoa rushwa
ya Sh milioni 30.2 kwa askari Polisi
na askari wa Wanyamapori ili
wasifunguliwe mashitaka ya
kukutwa na nyara na ganda la
risasi bila kuwa na kibali.
Katika mashitaka mengine,
washitakiwa wanadaiwa siku hiyo
hiyo walikutwa na ganda la risasi
bila kuwa na kibali cha kumiliki
silaha. Washitakiwa hao walikana
mashitaka yao na kurudishwa
rumande hadi Februari 17 mwaka
huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

UWANJA WA AZAM RUKSA KUTUMIKA KIMATAIFA KIMICHEZO

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF)
limekubali Uwanja wa Azam uliopo
Chamazi kutumika kuchezea
michuano ya kimataifa. Kwa
mujibu wa taarifa iliyopo kwenye
mtandao wa Azam, CAF imekubali
uwanja huo kutumika kupitia
taarifa ya barua pepe iliyotumwa
juzi na Naibu Mkurugenzi wa
Mashindano Khaled Nassar.
Taarifa hiyo inasema, Uwanja wa
Azam umepita vigezo vyote
vinavyohitajika na CAF kuandaa
michuano ya kimataifa utaanza
kutumika katika mechi za Kombe
la Shirikisho ambayo Azam FC
wanashiriki.
Naye Ofisa Habari wa Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) Boniface
Wambura amethibitisha kuwa
Uwanja wa Azam umekubaliwa
kutumika katika michezo ya
kimataifa kwa klabu kuanzia
msimu huu.
"Ni kweli Uwanja wa Azam
umepata kibali cha kutumika
katika michezo ya kimataifa na
utaanza kutumika msimu huu
unakuwa uwanja wa kwanza
unaomilikiwa na klabu Afrika
Mashariki kuruhusiwa kuandaa
mashindano makubwa ya klabu,”
alisema Wambura.
Khaled ameandika katika taarifa
yake ya barua pepe kwenda TFF na
Azam FC kuwa CAF ilimtuma
mkaguzi wake toka Zimbabwe,
Wilfried Mukuna kuja kukagua
uwanja huo na Mukuna
aliwasilisha ripoti CAF iliyopelekea
shirikisho hilo kutoa kibali kwa
Azam FC na TFF kuruhusiwa
kuutumia uwanja huo kwa mechi
zinazoandaliwa na CAF.
Uongozi wa Azam FC umetoa
shukrani kwa mkaguzi wa CAF
Mukuna, Uongozi wa TFF chini ya
Rais Jamal Malinzi na uongozi wa
CAF Cairo Misri hasa Nassar kwa
kuwezesha zoezi hilo kufanyika kwa
uwazi na uweledi wa hali ya juu.
"Pia Azam FC inapenda
kuwataarifu wapenzi wake kuwa
kuanzia msimu huu mechi zake za
CAF zitachezwa Azam Complex
Chamazi," ilisema taarifa ya Azam.

Monday, February 3, 2014

KEEP SWAGG 'Z

JINA:Master P anatokea pande za bunda ni mkali wa media pia ni chief wa Talent camp
NDANI YA SWAGGZ LEO
Katupia kitu cha Black yellow pia na kofia iliyo endana na t shirt
UJUMBE WA LEO
,"Nawapenda sana watu wote but Maiaha hayakutafuti Ila yanatafuwa"

AUWA KWA TUHUMA ZA KUZUIA MVUA KUNYESHA

WATU wawili wa familia moja
wameuawa wilayani Maswa
mkoani Simiyu, kwa kupigwa na
wananchi waliojichukulia sheria
mikononi, wakiwatuhumu kuzuia
mvua kunyesha hivyo kusababisha
ukame kwenye eneo lao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Simiyu, Charles Mkumbo alitaja
waliouawa ni Gilya Chile (70) na
mjukuu wake, Nyangu Nyambalya
(30).
Polisi inashikilia watu wanane
akiwemo Kamanda wa
Sungusungu, Sosoma Masamuda
(50), Ligwa Malimi wakituhumiwa
kuhusika na mauaji hayo.
Wengine ni Emanuel Kasmiri (42),
Michael Sospeter (18), Toto
Emanuel (28), Nyanzobe Ntinga
(26) Tabu Zengo (31) na Joyce Kija
(30). Baada ya uchunguzi wa polisi
kukamilika, watafikishwa
mahakamani kujibu mashitaka.
Mauaji hayo yalifanyika usiku wa
kuamkia juzi katika kijiji hicho,
Kata ya Mwanhonoli wilayani
Maswa.
Inadaiwa sungusungu wa kijiji
hicho waliitana usiku na kuafikia
katika kikao chao kwenda
kuwaamsha babu na mjukuu wake
waeleze sababu za kuzuia mvua
kunyesha.
"Usiku huo walinzi hao wa jadi
waliwakamata watuhumiwa hao
waliokuwa wamelala nyumba
tofauti wakawahoji kwa nyakati na
maeneo tofauti na kuwataka
watoe maelezo ya kutosha ya
sababu ya wao kuzuia mvua
isinyeshe mpaka mazao kuanza
kukauka katika mashamba ya
wakulima wa kijiji hicho,’’ alisema
kamanda.
Inadaiwa sungusungu
hawakuridhishwa na maelezo
ndipo walianza kuwasulubu kwa
kipigo na kuwasababishia mauti
kabla ya kuteketeza miili yao.
Kamanda alisema, uchunguzi wa
awali wa polisi umebaini kabla ya
vifo vyao, watuhumiwa walikuwa
wakitamba kwenye vilabu vya
pombe kuwa wanatoka kwenye
familia ya kitemi hivyo wana
uwezo wa kuleta mvua au kuizuia
isinyeshe.
Kwa mujibu wa kamanda, tambo
hizo zilifanyika kipindi ambacho
kijiji hicho kilikumbwa na ukame.
Inadaiwa watu hao walishauri
wananchi wa kijiji hicho
wawachangie gunia moja la
mahindi au mtama kila kaya
walete mvua.

KUFURU, JAMAA AAMUA KUFUNGA NDOA NA MBWA

Mnamo siku ya Jumatatu historia
iliwekwa katika kanisa la Our
Lady huko Presidio Francisco
jimboni California nchini
Marekani.
Mtu mmoja aitwaye Paul Horner
pichani mwenye umri wa miaka
35 akiwa amevalia suti yake
nadhifu alifunga ndoa na mbwa
wake mwaminifu aitwaye Mac.
Mchungaji aliyefungisha ndoa
hiyo Father McHale alionyesha
kufurahishwa kwake na kitendo
cha yeye kufungisha ndoa hiyo ya
kihistoria nchini Marekani.

Saturday, February 1, 2014

VIONGOZI WA DINI, VIJANA VIJANA WAHASISHA UVUMILIVU NA UMOJA KATIKA KAUNTI YA KWALE

Wakati Keya Kazungu alipofanya
ziara ya kurudi katika mji wa
nyumbani kwenye Kaunti ya Kwale
kwa ajili ya mapumziko ya
Krisimasi, aliona mabadiliko ya
kipekee.
Mwezi Januari 2011 wakati
alipoondoka kwenda kusoma Chuo
kikuu cha Nairobi, alisema vijana
wa jirani kutoka dini mbalimbali
yalijichanganya pasipo shida,
wakizungumza wakati wa jioni.
Wakati aliporudi, Kazungu,
mwenye umri wa miaka 25,
alisema aligundua kwamba
marafiki zake walikusanyika kwa
mujibu wa mashirikisho ya dini
zao.
Pasipo kutambua mvutano wa
kidini ulioshamiri, Kazungu,
Mkristu, alisema aliungana na
kikundi cha rafiki zake Waislamu.
"Nilifurahi kuwaona kwani
hatukuwa tumeonana kwa kipindi
cha karibia miaka miwili," Kazungu
aliiambia Sabahi. "Nilitarajia
wangekuwa na furaha pia, hata
hivyo, rafiki zangu walikuwa
tofauti. Kwa dakika kadhaa kikundi
kilitawanyika kwenda eneo
lingine."
Hassan Mwalulu, mwenye umri wa
miaka 24, mkaazi Mwislamu wa
Kwale, alithibitisha kwamba
shughuli za kijamii ziliathiriwa na
mvutano wa kidini katika eneo
hilo.
"Vijana ambao walikuwa wakicheza
pamoja bila kujali dini zao kwa
sasa wanaenenda tofauti,"
aliiambia Sabahi.
"Vilabu vya ndani vya mpira wa
miguu vimeundwa kwenye
mwelekeo wa kidini," alisema,
akiongezea kwamba miezi
michache iliyopita mashindano ya
ndani ya michezo yalikuwa na
maovu ya mtindo wa kidini na wa
kimadhehebu.
"Ni jambo la kawaida kusikia timu
ikisema kwamba 'tutawaonyesha
hawa Wakristo namna mpira wa
miguu unavyochezwa' au
'tutawashinda hawa Waislamu,'"
alisema. "Michezo kama ya mpira
wa miguu inajulikana kwa
kuzidisha mambo mengi ikiwa ni
pamoja na dini, lakini siyo Kwale."
Kubadilisha mwelekeo huo, vikundi
visivyo rasmi na watu binafsi
wanahamasisha shughuli za
mwingiliano baina ya dini katika
kaunti hii, Mwalulu alisema.
"Waliandaa zoezi la kusafisha mji
mara mbili na mashindano ya
[mpira wa miguu] ambapo
wachezaji kutoka imani mbalimbali
wanachanganyika kuunda timu,"
alisema, akiongeza kwamba
jitihada zinaonyesha matunda
taratibu wakati mvutano
unapungua.
Zaidi ya hayo, alisema, vijana
wanakutana katika mikutano
mbalimbali ili kujadili masuala
yanayoiathiri kaunti na jinsi
yanavyoweza kushughulikiwa
vizuri.
"Tumeishi kwa pamoja kwa [muda]
mrefu ili kuruhusu baadhi ya
masuala kutugawanya," alisema.
"Nina marafiki Wakristo ambao
niliwaalika kupata pamoja chai na
vitafunwa nyumbani kwangu au
sehemu ya kulia chakula. na wao
walifanya hivyo hivyo. mvutano
huu wa dini ni suala la kupita.
Tunajitolea kurudisha undugu."
Mauaji ya wahubiri wa dini
yaharibu uhusiano
Hussein Khalid, mkurugenzi
mtendaji wa Haki Africa, asasi
isiyo ya kiserikali ambayo
inatangaza haki za kijamii na
kiuchumi kwa Wakenya wote,
aliiambia Sabahi kwamba mauaji
yasiyo na ufumbuzi ya wahubiri wa
Kiislamu na kikristo yalikuwa
yanaharibu uhusiano.
Khalid alisema serikali inaweza
kupunguza mvutano wa kidini kwa
kuchunguza na kuwashtaki
watuhumiwa wa mauaji ya
mapadri wawili wa Kikatoliki na
wahubiri saba wa Kiislamu katika
mkoa wa Pwani tangu 2012.
Ukosefu wa mashtaka umeongeza
mvutano katika dini mbili, ambazo
matokeo yake wafuasi wake
wamekuwa wakituhumiana wao
kwa wao, Khalid aliiambia Sabahi.
"Tunahisi kwamba vikosi vya ulinzi
vinahusika na mauaji ya watu
wanaotuhumiwa kuwa na
uhusiano na magaidi lakini
wanasababisha matatizo zaidi kwa
jamii ambazo zimekuwa zikiishi
pamoja kwa miaka mingi,"
alisema.
Kamishna wa kaunti ya Kwale
Evans Achoki alikanusha tuhuma
kwamba serikali ilikuwa inahusika
na mauaji nje ya mahakama ya
watuhumiwa wa ugaidi.
"Sote tumeshangazwa na mauaji
lakini uchunguzi unaendelea,"
aliiambia Sabahi. "Hatutoi nafasi
yoyote. Baadhi ya magaidi
wanaweza kuwa wanawalenga
wahubiri katika mpango wa
kuchochea mivutano ya kidini."
Mwenyekiti wa Baraza la Wahubiri
wa Dini mbalimbali wa Pwani
Padri Wilybard Lagho alikiri
kulikuwa na kuongezeka kutengana
na kutovumiliana baina ya imani
tofauti.
Uhusiano kati ya Waislamu na
Wakristo katika mkoa wa Pwani
umetetereka, aliiambia Sabahi.
Msingi wa kuondoa kutokuwa na
uvumilivu wa kidini ni kuendelea
kuonyesha umoja miongoni mwa
viongozi wa dini, alisema,
akiongeza kwamba watumishi
kutoka imani zote wanafanya kila
wawezalo kuboresha uhusiano.
Licha ya kufanya kazi tofauti na
jamii zao, ushirikiano kati ya
Waislamu na Wakristo unahusisha
kuonekana pamoja katika
mikutano inayofanyika katika
ukumbi wa mji na barabarani
kuhubiri amani na umoja , alisema
Lagho.
"Hatuelewi kiwango cha kutokuwa
na uvumilivu, lakini pamoja na
maulamaa wa Kiislamu
tunaonekana kwa utulivu na
uvumilivu pamoja na imani zetu
zinazohusika. Tunaamini kwamba
kutokuwa na uvumilivu wa dini
hakutapunguza vurugu za kisekta,"
alisema Lagho.
Lagho alisema Wakristo
wanahamasishwa kujichanganya
na kufanya biashara pamoja na
Waislamu.
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la
Ushauri la Waislamu Kenya Sheikh
Juma Ngao alisema Maulamaa wa
Kiislamu wataendelea kutetea njia
zisizosababisha vurugu kwa
kutatua mambo.
"Dini zote zinamhitaji kila mmoja
kwa ajili ya ustawi wa dini na nchi
kwa ujumla," aliiambia Sabahi.
"Kuna njia ambazo zinahitaji
kutumika … Bila kujali mtu alikosa
kiasi gani, sio haki kufanya hivyo
kwa mtu wa imani tofauti."
Ngao alisema maimamu kutoka
katika misikiti mbalimbali
wamekubali kusisitiza mada hiyo
ya umoja na uvumilivu wakati wa
mahubiri yao.
"Kuwepo kwa amani ndiyo
kulikuifikisha nchi umbali huu na
tunawajibika kuudumisha,"
alisema.

WAUZA NGUO ZA NDANI MITUMBA WAIZIDI UJANJA TBS JIJINI MBEYA

WAFANYABIASHARA wa nguo
za ndani zilizo hafifu maarufu
kama mitumba jijini Mbeya,
jana waliwazidi ujanja
maofisa wa Shirika la
Viwango Tanzania (TBS) kwa
kuficha nguo hizo wakati wa
operesheni ya kuzikusanya na
kuwakamata wauzaji.
Wafanyabiashara hao
walioonekana kupewa taarifa
ya nini kitafanyika kabla
walificha nguo hizo hatari kwa
afya za wavaaji na baada ya
kumalizika kwa uparesheni
wakazirejesha sokoni na
kuendelea kuziuza kama
kawaida huku wakijigamba
kuwa Serikali haiwawezi.
Awali maofisa wa TBS
walioambatana na askari wa
Jeshi la Polisi na waandishi
wa habari, waliendesha
operesheni ya kukamata nguo
za ndani hususani chupi,
sidiria na soksi katika masoko
ya Sido na Mwanjelwa lakini
hawakufanikiwa kukamata
hata nguo moja katika
masoko hayo yaliyo maarufu
kwa uuzaji wa nguo za
mitumba ikiwemo zilizokuwa
zikitafutwa.
Ajabu ni kuwa
wafanyabiashara hao
walionesha kuwa na taarifa ya
kufanyika kwa operesheni na
kila kona ya masoko hayo
walisikika wakizungumza kuwa
maofisa wa TBS na polisi
wako katika eneo lao
wakifanya operesheni ya
kukamata nguo hizo.
“Umewaona ndio hao
wamekuja kwa ajili ya
kukamata zile nguo. Lakini
wanatafuta tu ukorofi kama
wanataka kukamata nguo za
mitumba si wakamate tu na
mashati basi.
“Kwa nini watilie mkazo
kwenye nguo za ndani pekee?”
Walisikika wafanyabiashara
katika baadhi ya vibanda vya
masoko hayo mawili wakihoji
hali iliyoonesha kuwa hawana
elimu ya kutosha juu ya
athari za kuvaliwa kwa nguo
hizo.
Mahali pekee walikofanikiwa
maofisa hao ni katika Soko la
Mbalizi ambako walifanikiwa
kumkamata mfanyabiashara
mmoja Lusekelo Adam akiwa
anauza soksi za mtumba na
kumfikisha ofisi ya Kamanda
wa Polisi mkoani Mbeya na
kisha kuteketeza soksi hizo
ambazo muuzaji alisema
zilikuwa na thamani ya Sh
200,000.
Akizungumza mara baada ya
kumalizika kwa operesheni
hiyo Ofisa Viwango na
Mkaguzi wa TBS, Paul
Manyirifa alikiri zoezi hilo
kufanyika kwa
wafanyabiashara walio
wadogo na kusema shirika
linaamini wapo
wafanyabiashara wakubwa
ambao ndio huziingiza kwa
njia za panya na kuwataka
wajisalimishe.
Kwa upande wake
Mwanasheria wa shirika hilo,
Baptista Bitao alisema
adhabu kwa mtu yeyote
anayeuza nguo hizo ni kati ya
Sh milioni 50 hadi 100 lakini
pia Mkurugenzi Mkuu wa
shirika ana mamlaka ya kutoa
adhabu isiyopungua Sh
milioni 20.
Naye Kamanda wa Polisi
mkoani hapa Ahmed Msangi
aliahidi kuendelea kutoa
ushirikiano wa kina kukamata
nguo hizo akisema lengo ni
kuona Watanzania hawawi
watu wa kupokea vitu
vitakavyolisababishia hasara
Taifa lao kwa kuingia
gharama ya kutibu maradhi
yatokanayo na nguo hizo.

Friday, January 31, 2014

KOCHA WA MANCHESTER DAVID MOYES AJIVUNIA KUWA NA NGUVU MPYA UWANJANI BAADA YA USAJILI WA JUAN MATA KULEJEA

KOCHA wa Manchester
United, David Moyes
amesema usajili wa Juan
Mata na kurejea kwa Robin
van Persie na Wayne Rooney
kumerudisha morali Old
Trafford.
Van Persie amerejea uwanjani
baada ya kukosa mechi 11
kutokana na kuwa majeruhi
na kufunga katika ushindi wa
mabao 2-0 dhidi ya Cardiff,
huku Mata akifanya kazi nzuri
baada ya kusajiliwa kwenye
dirisha dogo kwa pauni
milioni 37.1 akitokea Chelsea.
"Morali yangu imerudi, kwa
sababu najua kwamba
wachezaji wazuri wamerudi,"
alisema Moyes.
"Lakini bado nataka kushinda
na kucheza vizuri zaidi kwa
hiyo usidhani kwa sababu
nimeshinda leo (juzi) ndio
sababu ya kufurahi".
"Nina furaha kwa pointi tatu
nilizopata lakini wapi, nataka
kwenda na malengo ya wapi
nataka timu yangu icheze,
bado nahisi nina kazi kubwa
ya kufanya".
Ushindi huo umeifanya
Manchester United izidishe
ushindani katika kuwania
nafasi ya nne dhidi ya Everton
na Tottenham, lakini bado
wana tofauti ya pointi sita
dhidi ya timu inayoshika
nafasi ya nne Liverpool baada
ya kikosi hicho cha Brendan
Rodgers kuifunga Everton.
Na Moyes alikiri kwamba ujio
wa Mata, ambaye alicheza
vizuri licha ya kufanyiwa
mabadiliko kunampa namna
ya kupanga timu yake.
Katika mechi dhidi ya Van
Persie alifunga bao la kwanza
kabla Ashley Young hajafunga
bao la pili na la ushindi.
United imepoteza mechi nne
kati ya sita za mwisho
ikifanya vibaya kwenye Ligi na
kwenye makombe mbalimbali.
"Juan alifanya vizuri sana
ametengeneza nafasi nzuri
sana katika dakika 30 za
mwanzo," aliongeza Moyes.
"Tutamtumia na yeye
atatutumia, nilitaka kuwaona
yeye na Robin pamoja usiku
huu (juzi)," alisema.

JOSEPH OWINO ATAMBA KUVAA TIMU YA JKI OLJOLO

MLINZI wa Simba, Joseph
Owino amefurahishwa
kurejeshwa kwenye kikosi cha
timu hiyo na yupo tayari
kuivaa timu ya JKT Oljoro ya
Arusha kesho. Owino
alitofautiana na Kocha Mkuu,
Zdravko Logarusic kwa kile
ambacho kocha alidai kuwa
mchezaji huyo wa kimataifa
wa Uganda, alikuwa hajitumi
katika mazoezi.
Kutokana na hali hiyo,
aliamua kumpeleka Owino
kufanya mazoezi na timu B
kwa maelekezo maalumu.
Owino ambaye kwa sasa
amerejeshwa kundini baada
ya kuomba msamaha,
alisema atafuata maelekezo
ya kocha kama anavyotaka na
kusisitiza kuwa hatoruhusu
kutokuelewana tena kujirudia.
“Mimi ni kama binadamu
wengine na katika hali ya
kawaida watu hutofautiana na
hivyo nafurahi tumemaliza
tofauti zetu na tutafanya kazi
poa,” alisema Owino jana Dar
es Salaam.
Akizungumzia hali hiyo,
Msemaji wa Klabu ya Simba,
Asha Muhaji alisema ni
utaratibu wa kawaida kwa
kocha kuwarejesha wachezaji
kwenye timu B hasa pale
mchezaji anapotofautiana na
kocha.
“Kwa kiasi fulani naweza
kusema kuwa hakukuwa na
lolote baya kubwa ila ni hali
ya kawaida kwa watu
kutofautiana ila kizuri ni
kwamba wameshamaliza
tofauti zao na kwa sasa kila
kitu sawa,” alisema Muhaji.
Kwa upande wake, Kocha
Logarusic alisema anataka
kuona nidhamu ikichukua
mkondo wake katika klabu
hiyo hasa kwa wachezaji
kujituma na kufuata
maelekezo yake.
Katika mchezo huo wa kesho
kati ya Simba na maafande
hao wa Arusha, utakuwa ni
wa pili kwa kocha huyo katika
ligi na kisha timu itakwenda
Morogoro kuivaa Mtibwa
Sugar, Februari 5, mwaka
huu.

TANZANIA YAZIDI KUNG'ARA KIMATAIFA KWAKUWA NA MIRADI MIKUBWA YA KIMAENDELEO

TANZANIA imeendelea kupata
miradi mikubwa ya
maendeleo ya kimataifa,
ambapo sasa imeibuka kuwa
mshindi kimataifa na
kukubaliwa kuanzisha mradi
mkubwa wa Kanda ya Kati wa
Uchukuzi. Mradi huo
utakaohusisha miundombinu
ya reli, barabara na bandari
unatarajiwa kuanza
kutekelezwa wakati wowote
nchini.
Akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam jana,
Waziri wa Uchukuzi, Dk
Harrison Mwakyembe,
alisema mradi huo ulishinda
miradi 51 ya nchi zingine za
Afrika katika mkutano wa
Uchumi wa Dunia (WEF)
uliofanyika Januari 22 jijini
Davos, Uswisi.
Kabla ya ushindi huo, mradi
huo uliingia kwenye miradi 16
bora kati ya 51 ya Afrika na
kushindanishwa katika
mkutano huo uliohudhuriwa
na nchi kubwa kiuchumi,
kampuni za kimataifa na
mashirika makubwa ya fedha
duniani.
“Kwa kweli ilikuwa neema na
furaha kubwa kwa Tanzania
kupewa heshima hii, kwani
miradi mingine 16
iliyowasilishwa katika
mkutano huo nayo ilikuwa na
sifa nzuri, lakini mradi huu
wa Kanda ya Kati ambao
takribani asilimia 95 ya
utekelezwaji wake itanufaisha
Tanzania, ulionekana bora
zaidi,” alisema Dk
Mwakyembe.
Kutokana na ushindi huo, Dk
Mwakyembe alimwomba
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
aunde Tume maalumu ya
kitaifa, itakayosimamia na
kushughulikia kikamilifu
utekelezaji wa mradi huo, ili
uwe wa mfano Afrika na
duniani kote.
Sifa zilizochangia mradi huo
kutangazwa mshindi kati ya
miradi bora 16 ya Afrika na
aliyekuwa Waziri Mkuu wa
Uingereza, Gordon Brown, ni
pamoja na mikakati
iliyowekwa na Serikali ya
Tanzania chini ya Mpango wa
Matokeo Makubwa Sasa
(BRN) ya kuendeleza Ukanda
wa Kati wa Uchukuzi.
Nyingine ni dhamira ya dhati
ya Serikali ya Tanzania
iliyoonekana, pamoja na
mfumo iliyojiwekea katika
utekelezaji wa mradi huo
unaolenga kupanua bandari
za Tanzania na kufungua zaidi
milango ya kiuchumi kwa nchi
jirani.
Alipopewa nafasi ya
kuzungumza baada ya mradi
huo kutangazwa kushinda
katika mkutano huo,
Mwakyembe alishukuru
washiriki wa kila pembe ya
dunia, kwa kuiamini Tanzania
na kuelezea mikakati ya
utekelezaji wa mradi huo
ambapo hata hivyo
alibainisha upungufu wa
fedha uliopo.
Alisema baada ya kuelezea
changamoto zilizopo katika
hotuba yake, Brown
alimtaarifu kuwa mwaka huu
viongozi wakuu wa nchi
duniani, watakutana Abuja,
Nigeria, kupokea tathmini ya
utekelezaji wa mradi huo
ambapo pia itafanyika warsha
ya maandalizi ya utekelezaji
wa mradi mwanzoni mwa
Aprili nchini.
“Tuna mpango wa kumwomba
Rais Jakaya Kikwete awe
mgeni rasmi katika ufunguzi
wa warsha hii, ili
tuuthibitishie ulimwengu
utayari wa Tanzania kuleta
mapinduzi katika sekta ya
uchukuzi,” alisisitiza Dk
Mwakyembe.
Aidha, alisema kupitia warsha
hiyo, Tanzania imejipanga
kuionesha dunia kuwa na
mipango mizuri na ndiyo
maana akaombwa Waziri
Mkuu aunde Tume
itakayofanya kazi kwa saa 24
kusimamia utekelezaji wa
mradi huo.
Alisema alipendekeza tume
hiyo ya watu wanane ihusishe
wataalamu kutoka wizara za
Uchukuzi, Ujenzi, Fedha,
Shirika la Reli Tanzania (TRL)
na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mradi huo kwa Tanzania
utagusa Bandari ya Dar es
Salaam, maeneo ya
Mashariki, Magharibi na
Kaskazini mwa nchi na
utahusisha nchi za Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC),
Rwanda na Burundi.
Miradi mingine Mradi huo
mkubwa ni kielelezo kingine
cha heshima ya Tanzania
kimataifa, ambapo mwaka
jana wakati wa ziara ya Rais
wa Marekani nchini, Barrack
Obama, nchi ilipata heshima
nyingine ya kutekeleza mradi
mkubwa wa umeme
unaojulikana kama ‘Power
Africa’, utakaoinufaisha nchi
na kuwa kitovu cha uzalishaji
wa nishati hiyo.
Katika mradi huo
unaowezeshwa na Marekani
kwa kushirikisha Serikali na
sekta binafsi, una lengo la
kuiwezesha nchi kuongeza
kiwango cha uzalishaji
sambamba na kupata umeme
wa uhakika, utakoongeza
ajira. Serikali ya Marekani
ilitoa dola bilioni 7 kusaidia
kupatikana megawati 10,000
za nishati hiyo, huku sekta
binafsi ikitoa dola bilioni 9.
Moja ya kampuni kubwa
zinazohusika na mpango huo
ni General Electric (GE),
ambayo imekuwa mstari wa
mbele kuhakikisha mradi
unaendelea kwa kuahidi kutoa
megawati 5,000 kwa gharama
za kawaida kwa Tanzania na
Ghana.

Rihanna and Shakira Sizzle in "Can’t Remember to Forget You" Video

Shakira's back and she's belly
dancing on walls again, this time
with Rihanna by her side. The pop
stars unveiled the stunningly
beautiful visuals for their
collaboration, "Can't Remember to
Forget You" and it's got us all
talking.
"It's very reggae and it has a lot
of the vintage feel at the same
time," The Voice coach told VEVO
News about her post-break up
confessional. "That's why I
thought that Rihanna would be the
perfect feature in this song; her
voice in this song is just unreal
because she is reggae. I don't
think I've ever heard a female
singer deliver her lines in a reggae
song with such authenticity, you
know?"
The video, which features the pop
divas lamenting about their
"selective memory" as they dance
their way through a mansion and
its outdoor pool, was directed by
Joseph Kahn, who worked with Rih
Rih and Eminem for "Love the Way
You Lie."
The song is the lead single from
Shakira's self-titled, 10th studio
album, expected Mar. 25 with
more collaborations including Ne-
Yo, "who's out of this world," she
said.
Audio for the "Can't Remember to
Forget You" was released Jan. 13,
and it has so far climbed to No.
28 on the Billboard charts.
Combine the rapidly rising chart
success with the popularity of the
single's Spanish language version
and an Instagram post of her
baby boy that garnered 2.1 million
likes, Shakira has made a return
to Billboard 's Social 50 chart,
which ranks "the most popular
artists on YouTube, Vevo,
Facebook, Twitter, SoundCloud,
Wikipedia, Myspace and
Instagram." It's her first time atop
the chart since this time last
year.
This is her first album since 2010's
Sale el Sol .
"I love proving to myself with
every album that I can still do it,"
Shakira admitted, after saying that
she "always suffers" through the
creative process. But she's
"extremely happy" with how her
album came out. "It's always
nerve-racking, it's always the
same feeling, the same butterflies
in your stomach. You never know
how your body of work is going to
be received ... [but] at the end of
the day, I feel like I have an album
that I wanted to have."

MBOWE NAWENZAKE ASHIKILIWA NA JESH LA POLISI KWAMAHOJIANO MKOANI MBEYA

Chenyekiti wa Chadema Mh.
Freeman Mbowe na wabunge wawili
wa chama hicho Mh. Halima Mdee
na Peter Msigwa wameshikiliwa na
kuhojiwa kwa muda na Jeshi la
polisi mkoani Iringa kwa madai ya
kuzidisha muda katika mkutano
wao wa jana.

PICHA ZA YALIYOJIRI KWENYE MAZISHI YA MZEE DUDE

ALIYEKUWA MUIGIZAJI MCHEKESHAJI KWENYE KIPINDI CHA TV "FUTUHI"KILICHOKUWA KIKIRUSHWA NA STAR TV YA JIJINI MWANZA,MAREHEMU MZEE OMARY MAJUTO@DUDE AMEZIKWA RASMI JANA JIONI JIJINI MWANZA,
HIZI NI BAADHI YA PICHA ZA YALIYOJIRI KWENYE MAZISHI HAYO JANA JIONI,

MAZOEA YA WADADA WENGI WA SASA KUTOKA BILA KUVAA KUFULI YAMUUMBUA MCHEZA TENISI MAARUFU NCHINI MAREKANI NA DUNIANI SERENA WILLIAMS, AZIANIKA NYETI ZAKE MBELE KADAMNASI,

PICHA YA KIHASARA HASARA YA MCHEZA TENISI MAARUFU NCHINI MAREKANI NA DUNIANI KWA UJUMLA SERENA WILLIAMS ZIMEVUJA MTANDAONI,
KWA HARAKA HARAKA IMESHINDWA KUELEWEKA KUWA NI MAKUSUDI AMA NI BAHATI MBAYA KWA YEYE KUONEKANA KUTOKA AKIWA BILA KUFULI,PICHA INAYOMUONYESHA WAZI SEHEMU ZAKE NYETI,
HALI HII IMEKUWA NI KAWAIDA KWA WASANII NA WATU MAARUFU HASA WA JINSIA YA KIKE KUKUTWA NA KAMERA ZA MAPAPARAZI SEHEMU TOFAUTI DUNIANI WAKIWA BILA KUFULI JAMBO LINALOONYESHA KUWA HALI HIYO YA KUTOVAA KUFULI KWA WADADA SASA HIVI NI FASHION.

PICHA,YALIYOJIRI KWENYE MAZISHI YA MPIGA TUMBA MAHIRI NCHINI TANZANIA MASOUD MOHAMED"MCD",

MWANAMUZIKI {MPIGA TUMBA} MAARUFU NCHINI TANZANIA MASOUD MOHAMED "MCD"AMEZIKWA RASMI JANA WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO ALIKOKUTWA NA UMAUTI,MAREHEMU MCD ALIZIKWA JANA MAJIRA YA SAA SABA MCHANA KWENYE MAKABURI YA NJORO,WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO,MAREHEMU  ALIFARIKI DUNIA JUZI JUMATATU MAJIRA YA SAA NNE USIKU KATIKA HOSPITALI YA KCMC{KILIMANJARO},IKIWA NI MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALINI HAPO KWA MATIBABU BAADA YA HALI YAKE KUWA MBAYA,HIZI NI BAADHI YA PICHA ZA MAZISHI YA MAREHEMU MCD JANA MKOANI KILIMANJARO,

Wednesday, January 15, 2014

Tuesday, November 26, 2013

UKUBALI USIKUBALI?? HUU NI UTAFITI ULIOFANYWA TOKA...

UKUBALI USIKUBALI?? HUU NI UTAFITI ULIOFANYWA TOKA...: KUNA WASANII WAMETANJWA HUMU KIUKWELI ,HAPO NDO TUKADIRIKI KUSEMA HUU UTAFITI HATUKUBALIANI NAO HAUKO SAWA KABISA.SOMA

Wednesday, November 20, 2013

CHEKI VIDEO MPYA KUTOKA KWA SHILOLE "NAKOMAA NA JI...

CHEKI VIDEO MPYA KUTOKA KWA SHILOLE "NAKOMAA NA JI...: Dakika zako 4 unaweza kuzitumia kuungana na AyoTV sasa hivi kutazama video mpya ya mwimbaji Shilole iitwayo ‘Nakomaa na jiji’ iliyofan...

SIRI YAFICHUKA!!!!!!!!! HUYU NDIYO MGANGA WA STAA ...

SIRI YAFICHUKA!!!!!!!!! HUYU NDIYO MGANGA WA STAA ...: Pennie na Diamond ambao wanadaiwa kumtumia Dk Kamdege kufanikisha mambo yao.   Dk Kamdege kutoka Tabora ambae inasemekana amekuwa kwe...

Hot Newz Daily: EXCLUSIVE: SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA NAY ...

Hot Newz Daily: EXCLUSIVE: SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA NAY ...: Kuwa wa kwanza kusiikiliza hapa ngoma mpya kutoka kwa Nay wa Mitego "Nakula Ujana". Ngoma imefanyika pale MJ Records bit ikinyon...