ads

Friday, February 14, 2014

UTAMBUE UJIO MPYA WA MSANII MB DOG NDANI YA GAME LA MUZIKI WA BONGO

MKALI wa muziki wa kizazi
kipya nchini, Mbwana
Mohammed maarufu kama
Mb Dogg, yupo kwenye
mipango ya kuachia wimbo
wake mpya unaokwenda kwa
jina la Baby mbona
umenuna?
Mb Dogg pichani, wimbo
wake mpya wa 'Baby Mbona
Umenuna' utakuwa balaa na
unatarajiwa kumuweka tena
kileleni.
Wimbo huo umerekodiwa
katika Studio za Maccopa,
ambapo unatarajiwa
kurudisha makali na heshima
ya msanii huyo aliyewahi
kuwika katika tasnia hiyo.
Akizungumza jana jijini Dar
es Salaam, Mkurugenzi wa
Kampuni ya Qs Mhonda J
Entertainment, Joseph
Mhonda, alisema kwamba
wimbo huo ni moto wa
kuotea mbali ambao kwa
kiasi kikubwa utamuweka
juu zaidi.
Alisema kwamba Mb Dogg ni
msanii aliyejichimbia kwa
muda mrefu akiwa na
mahitaji ya kurudi kwenye
nafasi zake za juu alipokuwa
awali.
“Sisi kama Kampuni
tunaofanya kazi na Mb Dogg
tunaamini kabisa huu ni
wakati wake wa kurudi tena
kileleni ili aendeleze makali
yake ya awali.
“Baby Mbona umenuna ni
wimbo ambao kwa hakika
utadhihirisha ubora wa
mwimbaji huyu wa Latifa na
nyinginezo zilizomuweka
kileleni,” alisema.
Mb Dogg anatokea katika
kampuni hiyo kwa sasa,
akiwa sambamba na Nay wa
Mitego anayetamba na
wimbo wa Muziki Gani,
aliyeimba na Diamond.

Mwigizaji na shoga maarufu wa Nollywood Nigeria afariki ghafla akimegwa!

Mwigizaji maarufu Charles
Warren ambaye ni shoga
anayeigiza sinema katika
tasnia ya sinema ya Nollywood
nchini Nigeria amefariki ghafla
alhamisi iliyopita majira ya
usiku katika Hospitali moja
jijini Lagos nchini Nigeria.
Charles Warren alifariki ghafla
wakati akiifanya mapenzi
(akimegwa) na mwenzake
aliyetajwa kwa jina la Ajah
ambapo ghafla alianza kulalamika
maumivu ya kiuno na baadaye
maumivu hayo yakahamia
mgongoni ambapo baadaye
alipata haja kubwa mara nne
ndani ya muda wa dakika 30.
Baadaye maumivu hayo
yalihamia kifuani ambapo ilibidi
awahishwe katika hospitali ya
Safeway kwa matibabu zaidi.
Rafiki yake aitwaye Ajah ambaye
ndiye waliyekuwa wakifanya naye
mapenzi alijaribu bila mafanikio
kumfanyia masaji kifuani ili
kumpunguzia maumivu lakini
haikusaidia, Warren alifariki
dunia usiku huo huo.
RIP Charles Warren.

Monday, February 10, 2014

ROSE MUHANDO MBARONI KWA UTAPELI

STAA wa nyimbo za Injili Bongo,
Rose Muhando yamemkuta ya
kumkuta ambapo Ijumaa iliyopita
alishikiliwa na Polisi wa Kituo cha
Msimbazi jijini Dar es Salaam
kwa madai ya kuingia mitini na
shilingi milioni 6 alizolipwa kwa
ajili ya kwenda kufanya shoo ya
kiroho, Mombasa, Kenya
Novemba 3, 2013 lakini
hakutokea. Kwa mujibu wa
chanzo chetu, Rose alidakwa jijini
Dar es Salaam saa sita mchana
huku mlalamikaji wake akiwa ni
mtu aliyejulikana kwa jina la
Nathan Wami.
Nathan amewahi kuwa meneja
wa kazi za Rose Muhando. Kwa
sasa Rose anaratibiwa na
Kampuni ya Sony.
MADAI YA JALADA LA KESI
Kwa mujibu wa chanzo, jalada la
kesi hiyo lilifunguliwa Dodoma
likisomeka; DOM/RB/1129/2014
KUJIPATIA MALI KWA NJIA YA
UDANGANYIFU.
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa Rose
aliachiwa kwa dhamana akitakiwa
kurudi kituoni hapo Februari 8,
2014 huku mkononi akiwa
ameshika kiasi hicho cha fedha
kwa ajili ya kumlipa mlalamikaji
huyo.
WIKIENDA LATINGA POLISI
MSIMBAZI
Baada ya kuinyaka nyeti hiyo,
Ijumaa Wikienda lilipiga hodi
kituoni hapo na kuulizia kama ni
kweli nyota huyo wa wimbo wa
Utamu wa Yesu alishikiliwa.
“Sisi si wasemaji wakuu wa polisi,
hatuna mamlaka hayo. Hatuwezi
kusema ni kweli au si kweli,”
afande mmoja alilijibu gazeti hili.
MADAI NYUMA YA PAZIA
Wakati madai ya Rose yakiwa
hayo, nyuma ya pazia kuna
mlolongo wa matukio ya
kushangaza kati ya mwimbaji
huyo na Nathan.
Kwa mujibu wa chanzo kimoja,
Rose amekuwa akiingia kwenye
madai ya kupokea fedha za shoo
na kutokwenda lakini Nathan
akielekezewa lawama zote.
PESA APOKEE MENEJA, LAWAMA
ABEBESHWE ROSE
“Jamani mimi nataka kuwaambia
ukweli, Rose hahusiki na hiyo
tabia. Wengi wanasema ana
mchezo wa kuchukua fedha za
watu halafu haendi kwenye tukio
lakini ukweli si huo,” kilisema
chanzo hicho.
Wikienda: “Ukweli ni upi? Funguka
basi.”
Chanzo: “Ukweli ni kwamba,
Nathan amekuwa akimnyanyasa
sana Rose kwa muda wote
aliokuwa meneja wake.
“Ilifika mahali, Nathan ndiye
alikuwa akipokea pesa kutoka
kwa watu wanaomhitaji Rose bila
kuwasiliana na mwenyewe.
Wakati mwingine Rose hajulishwi
mapema.
“Siku akiambiwa, pengine
anaumwa au yupo mbali na eneo
la tukio, sasa hapo waandaaji
wanamsema Rose kwamba
amechukua fedha na kuingia
mitini,” chanzo kilizidi kuweka
wazi.
ROSE HANA CHA KUFANYA
Kwa mujibu wa chanzo, hali hiyo
imekuwa ikimsumbua sana Rose
kwani ni kweli wengi wanaamini
hivyo lakini ukweli ni kwamba
anasingiziwa tu, Rose hawezi
kupokea fedha halafu asiende
kuimba ila kwa sababu Nathan ni
meneja wake aliyemtoa kisanii
anajikuta hana la kufanya.
“Mbona kwenye matamasha ya
Pasaka na Krismasi
yanayoandaliwa na Msama
Promotion hatujawahi kusikia
Rose kaingia mitini? Ni kwa
sababu Msama mwenyewe
anawasiliana naye moja kwa
moja,” kiliendelea chanzo.
NATHAN ALIISHI NA ROSE KWA
UBABE
Ikazidi kudaiwa na chanzo chetu
kwamba katika kipindi chote,
Nathan amekuwa akiishi na Rose
kwa ubabe wa hali ya juu, jambo
ambalo lilimuathiri Rose
kisaikolojia bila kujijua.
“Kuna mengi sana, tena yale ya
ndani zaidi, sipendi kuyasema
lakini Nathan mwenyewe
anayajua, siku ikifika nitayalipua
kama atapinga,” kilisema chanzo.
ROSE MUHANDO HUYU HAPA
Ijumaa Wikienda lilimtafuta Rose
kwa lengo la kutaka kumsikia
atakachokisema juu ya madai
yote hayo kuhusu yeye na
Nathan, lakini zaidi ya yote tukio
la kuwekwa mahabusu ya
Msimbazi Polisi, msikie:
“Kusema ule ukweli mimi
namwachia Mungu, yeye anajua
ukweli uko wapi na uongo uko
wapi!”
NATHAN SASA
Baada ya hapo, gazeti hili
lilimtafuta Nathan Wami na
kumsomea mashitaka yote.
Nathan: “Hayo madai si ya kweli.
Kama kasema yeye siyo kweli.
Nimeishi na Rose karibu miaka
kumi na mbili, nilikuwa
namchukulia kama mtoto wangu.
“Nimekuwa nikiona kwenye
magazeti kwamba eti alisaidiwa
na mfuko wa kanisa wakati mimi
ndiye niliyemtoa.”
Wikienda: “Kwa hiyo madai
kwamba umekuwa ukiishi naye
kibabe, hukuwa unamtendea haki
si ya kweli?”
Nathan: “Si ya kweli hata kidogo.”
MSAMA ANAMLIPA NANI?
Gazeti hili liliwasiliana na
muandaaji wa matamasha ya
Pasaka na Krismasi, Alex Msama
kuhusu malipo ya Rose
Muhando.
Msama: “Mimi huwa namalizana
na Rose.”
Wikienda: “Kuna mwaka umewahi
kumlipa pesa halafu hakutokea
kwenye tamasha lako?”
Msama: “Hapana, hata Tamasha
la Pasaka mwaka huu atakuwepo
panapo uzima maana
tumeshamalizana.”
KUTOKA KAMPUNI YA SONY
Habari zilizopatikana kutoka
Kampuni ya Sony ambayo
inamratibu Rose kwa sasa,
zinasema kuwa wakati wa kuingia
makubaliano na nyota huyo
walikutana na masuala hayo ya
madeni lakini walipofanya
uchunguzi wakagundua mambo
ambayo hawakutaka kuyaweka
wazi lakini kimsingi
walimhurumia Rose.
“Ila mabosi wa Sony waliamua
kuwa yale madeni yaliyopita
watayalipa wao, yale ambayo
tarehe za Rose kuimba bado,
wamemwambia akaimbe ili
kumalizana na wahusika,”
kilisema chanzo hicho na kuomba
kutotajwa jina gazetini.
-GPL

AIBU SHULE YA MSINGI JIJINI DAR,WANAFUNZI WAKAA CHINI

Aibu! Shule ya Msingi Jijini
Dar, Wanafunzi wakaa chini
huku waalimu wakitumia
Khanga kama Majamvi.
Shule ya Msingi Mtambani
iliyoko Kinondoni jijini Dar es
Saalam, haina samani hali
inayosababisha wanafunzi kukaa
chini, wakati walimu
wanalazimika kutandaza khanga
wanazokalia chini ya miti.
“Shule hii ina upungufu wa
madawati, nusu ya wanafunzi
wanakaa chini, hatuna ofisi za
kutosha za walimu wale wasio
na nafasi wanakaa chini ya miti”,
alisema Mwalimu Mkuu
Emmanuel Munisi.
Aliongeza kuwa tatizo hilo
linawalazimisha wengine
kutandika khanga chini ya miti ili
kufanya kazi kwa sababu ya
ukosefu wa meza za kufanyia kazi
na kwamba mvua inaponyesha
wanalazimika kujikusanya pamoja
na wanafunzi madarasani,
alisema Munisi.
Shule ya Mtambani iko taabani
wakati serikali ilipata chenji ya
rada ya shilingi bilioni 43 ambayo
ilielezwa kuwa pamoja na
kununua vitabu mashuleni pia
itawezesha upatikanaji wa
madawati.
Serikali ya Uingereza ilirudisha
fedha hizo kuanzia mwaka jana
na kwamba jukumu la kununua
vifaa hivyo liliachwa kwa Ofisi ya
Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa, ambayo
inasimamia shule za serikali za
msingi na sekondari.
Shule hiyo ina walimu 41 na
wanafunzi 1,830 inakabiliwa na
uhaba wa madawati, viti na
meza za walimu kwa mujibu wa
Munisi. Aliiambia NIPASHE
Jumamosi kuwa mazingira
mabovu ya shule hiyo ni pamoja
na upungufu wa vyoo, ukosefu
wa sakafu madarasani badala
yake madarasa yana mahandaki
na vumbi kila wakati. Akifafanua,
alisema kuwa shule hiyo
ilianzishwa mwaka 2002 ikiwa na
wanafunzi 77 na ofisi moja
ndongo kwa ajili ya walimu. Hata
hivyo, kwa sasa ina wanafunzi
1,830 wa kike 917, wavulana 913
na walimu 41.
Alisema hakuna maji safi ya
kunywa na wanafunzi wengi
wanakabiliwa na matatizo ya njaa
yanayosababisha kudondoka
mara kwa mara.
Alieleza kuwa wastani wa
kuanguka ni kati ya watoto
watano na zaidi ambao hutibiwa
kwa kuwekewa drip za kuongeza
maji na sukari mwilini.
Madaktari wanasema tatizo ni
ukosefu wa chakula na nguvu
mwilini kwa hiyo
wanapotundikiwa drip wanapona.
Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa
Mtambani, Steven Ngonye,
akizungumzia tatizo hilo alisema
litashughulikiwa pamoja na
upatikanaji wa maji na ukarabati
wa shule hiyo.
Naye Diwani wa Kata ya
Mtambani Maji Safi Sharifu,
alisema serikali inalitambua
tatizo hilo na imetenga bajeti ya
Sh. milioni 108 kwa ajili ya
madawati na ukarabati wa
vyumba vya madarasa na
kwamba hadi sasa madawati 50
yameshapelekwa shuleni hapo.
Akifafanua zaidi alisema kuna
mpango wa kuongeza vyumba
vya madarasa mawili pamoja na
kufikisha maji safi kazi
itakayogharimu Sh. milioni 20.
CHANZO: NIPASHE

AY AFUNGUKA JUU YA YA UZUSHI WAWATU KUSU JAGUAR

Msanii wa HipHop kutoka
Tanzania, Ambwene Yesaya
amekanusha uvumi uliokuwa
umezagaa nchini Kenya wa
kumuandikia baadhi ya nyimbo
mkali wa Kioo kutoka Kenya,
Jaguar.
Katika mahojiano aliyofanyiwa
nchini Kenya alikokuwa ameenda
hivi karibuni, AY amesema hajawai
kumuandikia wimbo wowote
Jaguar na hata wimbo wao
‘Nimetoka Mbali’ kila mtu aliandika
mashairi yake.
“Jaguar ni mmoja wa marafiki
zangu. Tumefanya kazi pamoja na
hakuna ukweli wowote kuhusiana
na tetesi za mimi kumuandikia
mashairi ukizingatia amekuwepo
kwa muda mrefu kwenye gemu ya
muziki hivyo kumfanya kuwa
miongoni mwa wasanii wenye
uzoefu wa kutosha na kufanya
vizuri hata ukitazama ngoma
niliyowahi kufanya nae ya
Nimetoka Mbali, kila mmoja wetu
aliandika mashairi yake kivyake
hivyo huna haja ya kubisha kwa
uwezo mkubwa alionao na naamini
ni ushahidi tosha,” alisema.
Pia AY amepinga muziki wake
kuathiriwa na Diamond kwakuwa
kila mtu ana malengo yake katika
muziki wake.
“Kila msanii ana mipango na
mikakati yake ya kufikia malengo
aliyojiwekea, sipo kujilinganisha na
mtu yoyote, ushindani wangu ni
kwa yule anayetaka kujaribu
kutengeneza mkwanja mkubwa
kushinda wangu, huo ndio
ushindani wa kweli, hata hivyo
siwezi kuwa juu milele.”

BABU AYUBU AFUKUNGA YA MOYONI KUHUSU DIAMOND

Msanii nguli katika kuiga sauti za
watu maarufu MC Babu Ayoub
aliyewahi kutamba na wimbo wa
chaja ya kobe ameibuka na
kusema mkali wa ngololo
Diamond si mchawi.
Mkali huyu wa kibao cha chaja ya
kobe ambaye pia aliwahi
kushiriki katika wimbo wa ndiyo
mzee wa Prof.J alifunguka mbele
ya mwandishi wetu. ALisema
“Diamond si mchawi ila
anajithamini kama msanii,anajua
umuhimu wake anajitambua na
hata kama hajitambui basi
anawashauri wazuri kwa maana
ya menejiment.anajituma kwani
anajua kucheza na muda na yuko
kibiashara zaidi si kama wasanii
wengine waliowahi kuhit,jamaa
najua pia kucheza na
media ,ukimpa nafasi hafanyi
makosa.Aidha msanii huyu
anayetegemea kuja na kibao
chake kipya amedai msanii
Diamond ana haki ya kuwa hapo
alipo lakini pia itakuwa ni
fundisho kwa wasanii wengine
waliohiti na watakaohit.

BABY MADAHA APIGWA CHINI NA RECORD LABEL YAKE YA CANDY AND CANDY YA UKO KENYA NA KUPOKONYWA GARI, KISA NI UMALAYA

Mwanamuziki na muigizaji baby
Joseph madaha amefunguka na
kusema kuwa kweli ameamini
uchawi na kupigana juju vipo
kwenye gemu kwani mambo
yaliyomtokea hivi karibuni
haelewi hata imekauje.
Chanzo nini?
Hapo siku za nyuma baby
Madaha alipatikana na dhahama
ya kukumbwa na kashfa nzito
sana ya kujiuza kwa dau la
milioni kumi kwa jamaa mmoja
hivi mitaa ya Dar es Salaam
Jambo lilolopelekea yeye kupigwa
chini na Record label yake ya
Candy and Candy ya huko Kenya
na kupokonywa gari aina ya AUDI
TT aliyokuwa akitembelea huku
akiharibu pia uhusiano wake na
bosi wa record label hiyo – Joe
kairuki ambaye pia anadaiwa
kuwa mpenzi wake.
Je ni Kweli alijiuza?
Baby Madaha ambaye amerudi
nchini hivi karibuni tokea Nairobi
alipoenda “ku-solve” ishu yake
hiyo na label hiyo anasema yani
hata haelewi kitu gani kilitokea
siku hiyo ingawa mpaka
akaandikwa kama alienda kujiuza,
anachokumbuka ni kupigiwa simu
na mtu asiyemfahamu an
kumwambia anataka wafanye
naye kazi ya kusambaza filamu
yake mpya ya Gal Bladder
ambaye inatikisa soko kwa sasa.
Baada ya kufika hapo waliongea
vizuri na kuondoka ghafla kabla
ya kuja kusoma kesho yake kuwa
alikuwa anajiuza kitu ambacho
ansema hajui kimetoka wapi.
“Yani hata sielewi ilikuaje
nikaenda kukutana na yule jamaa,
ilikuwa ni kama muujiza hivi,
mwanzo nilisita sana ila
nikashangaa nimefika tu pale bila
kujielewa, ni vitu vya ajabu sana”
alieleza baby Madaha.
Uhusiano wake na Label hiyo
ukoje sasa?
Akizungumza na bongomovies,
baby amesema kwa sasa kila kitu
kipo sawa kwani alipoenda Kenya
waliongea vizuri na bosi wake
huyo na kumaliza tofauti zao na
sasa amerudi nchini kusambaza
filamu yake hiyo mpya ya Gal
bladder huku akijiindaa kupiga
show kwenye tour yake
aliyoiandaa jina la Top Up and
Refill itakayofanyika mwezi ujao
wa tatu.
Mwenyewe anasemaje zaidi?
Hata wafanyaje, waniroge,
wanichafue, i’m a bad gal, na
sibabaishi na vijimaneno vya
watu hata kidogo, sitoki candy
and Candy hata waloge kwa
waganga wote duniani. Kama
walifikiri nimeumbuka, wajue
watasubiri sana. Nikitoka kenya
naenda Holywood tu!

Friday, February 7, 2014

KISANUKO CHA MNUKO WA LEO AUNT EZEKIEL AKUTWA KATIKA FOLENI YA MAKAHABA JIJINI DAR

Muigizaji maarufu wa filam Tanzania anaejulikana kwajina la Aunt Ezekiel akutwa katika
foleni ya makahaba wa
kujiuza jijini dar…Akimbia
kumkwepa PAPARAZI kwa aibu asipigwe picha.
Lakini imekuwa ngumzo kwa watu wengi na wamekuwa wakijiuliza maswali me sana kwanini nyota huyo kuinekana katika eneo hilo tena akiwa katika vivazi vya utata.

MPIGIE KURA KISURA HAWA 13 MODEL COMPETITION

Mpagie kura mwadada huyu kisura aweze kuiwakilisha nchi yako kimataifa kwa uzuri wakipekee kwaku like picha yake ambayo inapatikana facebook katika kurasa (page) ya

MARIDADI ONLINE 2014
(Model Competition)

Namba yake ya ushiriki ni 13
Jina Hawa twaib
pamoja tunaweza kuitangaza Tanzania.

Thursday, February 6, 2014

MABOSI WA MASHIRIKA YA UMMA WAPAANDISHWA KIZIMBANI

MABOSI wa zamani wa mashirika
ya umma, Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) na Shirika la Ndege
Tanzania (ATCL), jana walipanda
kizimbani kujibu mashitaka
yanayowakabili kutokana na
uamuzi waliofanya walipokuwa
wakiongoza mashirika hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa TBS, Joseph
Masikitiko, aliieleza mahakama
kuwa, aliyekuwa Mkurugenzi wa
shirika hilo, Charles Ekelege, alitoa
msamaha wa ada ya utawala kwa
kampuni mbili bila kufuata
taratibu.
Masikitiko alidai hayo wakati
akitoa ushahidi katika kesi ya
matumizi mabaya ya madaraka na
kulisababishia shirika hilo hasara
ya Sh milioni 68, inayomkabili
Ekelege.
Ekelege anadaiwa kusababisha
hasara hiyo baada ya kuondoa ada
ya asilimia 50 ambayo ni sawa na
Sh milioni 68, kwa Kampuni za
Jaffar Mohamed Ali na Quality
Motors bila idhini ya Bodi.
Akiongozwa na Wakili Janeth
Machulya kutoka Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa
(Takukuru), Masikitiko alidai kuwa
anazifahamu kampuni hizo kwa
kuwa zilikuwa zinafanya kazi ya
ukaguzi wa magari kutoka nje kwa
niaba ya TBS.
Alidai katika kipindi cha mwaka
2007 hadi 2009 akiwa Meneja wa
Fedha na Utawala, hajawahi
kupokea wala kushughulikia barua
za maombi ya kuondolewa kwa
ada ya utawala kutoka kampuni
hizo mbili.
Kificho
Aidha alidai hakujua kama
kampuni hizo zilipewa msamaha
wa ada, hadi alipopata ripoti ya
ukaguzi wa hesabu za nje ya
mwaka 2008 hadi 2009, na kusikia
kwenye kikao cha Baraza la
Utendaji ambalo kwa sasa ni Bodi
ya Wakurugenzi, cha Septemba 30
mwaka 2011.
Alidai katika kikao hicho yeye
akiwa mualikwa, walipata taarifa
kuwa Menejimenti ilitoa msamaha
wa ada hiyo bila kupata kibali cha
bodi hiyo, ambapo bodi iliona
walitoa msamaha huo kimakosa
na kuwaonya wasirudie tena.
Alidai taratibu za kuomba
msamaha wa ada ni kuwasilisha
barua kwa Mkurugenzi, kisha iende
kwa Mhasibu Mkuu atakayeandika
dokezo kwa Mkaguzi wa Ndani
ambaye ataangalia kama amekidhi
vigezo vya kusamehewa,
itapelekwa kwa Meneja wa Fedha
kisha Mkurugenzi ataipeleka Bodi
ya Wakurugenzi kwa ajili ya
kuidhinishwa.
Akihojiwa na Wakili Majura Magafu
anayemtetea Ekelege, Masikitiko
alidai kuwa, Bodi haikusema kama
Ekelege alifanya kosa, bali ilisema
Menejimenti ilifanya makosa kwa
kutoa msamaha huo bila kupata
kibali.
Inadaiwa kuwa Machi 28, mwaka
2008 na Agosti 7, mwaka 2009,
Ekelege alitumia madaraka vibaya
na kusamehe ada kampuni mbili
kwa asilimia 50, ambayo ni sawa
na Sh milioni 68 bila idhini ya
Baraza la Utendaji kinyume na
utaratibu wa TBS pia
alilisababishia shirika hilo hasara
ya fedha hizo.
Mataka
Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya
Kuhifadhi Magari Yanayodaiwa
Kodi, Bartholomew Kijazi,
ameieleza Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu kuwa wanalidai
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Sh milioni 206.4.
Kijazi alidai hayo jana wakati
akitoa ushahidi katika kesi ya
kutumia vibaya madaraka kwa
kutangaza zabuni na ununuzi wa
magari chakavu 26, inayomkabili
Mkurugenzi wa zamani wa shirika
hilo, David Mattaka na wenzake
wawili.
Akiongozwa na Wakili wa Serikali,
Shedrack Kimaro, Kijazi alidai
kuwa wanaidai ATCL fedha hizo
kutokana na kuhifadhi magari tisa
katika ghala lao lililopo Mbagala,
tangu 1998 hadi Novemba mwaka
jana.
Alidai kuwa Desemba 16, 2011
aliandaa ripoti ya mtiririko wa
kuingiza na kutoa magari 26 ya
kampuni ya ATCL pamoja gharama
za kuhifadhi na kukarabati, baada
ya Taasisi ya Kupambana na
Kuzuia Rushwa (Takukuru) kuomba
ripoti hiyo.
Alidai wakati huo walikuwa
wanaidai ATCL dola za Marekani
118,000 kutokana na kuhifadhi
magari hayo kwa miezi 39 kwenye
ghala lao la Mbagala, ambapo kati
ya magari hayo, magari 15
yalitolewa na mengine tisa
yamebaki kutokana na kukosekana
kwa fedha za kulipa ushuru wa
forodha.
Alifafanua kuwa kwenye ghala lao
wanatoza kila gari dola 250 kwa
mwezi na hadi kufikia Novemba
mwaka jana, walikuwa wakidai
shirika hilo dola za Marekani
129,000 ambayo ni sawa na Sh
milioni 206.4.
Alidai ATCL walihifadhi magari
hayo katika ghala lao kuepuka
gharama za bandarini ambapo kwa
siku wanatoza dola za Marekani 25
hadi 40 kulingana na ukubwa wa
gari na kwa mwezi ingekuwa dola
1,200.
Mbali na Mattaka washitakiwa
wengine ni Kaimu Ofisa Mkuu wa
Kitengo cha Fedha, Elisaph Ikomba
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Ndani, William Haji.
Washitakiwa wanadaiwa kula
njama, matumizi mabaya ya
madaraka na kuisababishia Serikali
hasara ya dola 143,442.75 za
Marekani kwa kuagiza magari 26
chakavu kwa gharama ya Dola
809,300 kutoka Kampuni ya Bin
Dalmouk Motors ya Dubai bila
kutangaza zabuni ya ushindani.
Aidha wanadaiwa kuruhusu
kununuliwa kwa magari hayo bila
mkataba wa ununuzi ambao
umewekwa saini na wahusika na
kuthibitishwa na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali na kuisababishia
Serikali hasara baada ya
kushindwa kulipia kodi na
kuchukua mkopo kwa ajili ya
kuyakomboa na kuyatunza.

Wednesday, February 5, 2014

JANGA JINGINE LAZUKA SHILOLE SIKIO LA KUFA, AKANA MAAGIZO ALIYOPEWA NA MCHUNGAJI

STAA wa mduara Bongo, Zuwena
Mohamed ‘Shilole’ amedhihirisha
kuwa ni sikio la kufa baada ya
kusema yeye ni miongoni mwa
wanawake wanaojua kuchuna
mabuzi.
Kauli hiyo imechochea vigezo vya
kumfanya Shilole aonekane
hasikii kwani wiki kadhaa
zilizopita mchungaji wa kanisa
moja lililopo Ubungo, jijini Dar
ambaye hakujulikana jina lake,
alimtaka kuishi katika sura ya
kumpendeza Mungu lakini
inaonekana amempuuza.
Akizungumza na Risasi
Mchanganyiko juzi, jijini Dar es
Salaam, Shilole alisema alitunga
wimbo wa Nachuna Buzi kwa
sababu anajua kuwa wanawake
wengi ni mafundi wa tabia hiyo
akiwemo yeye mwenyewe!
“Unajua mwanamuziki unatakiwa
kuchagua wimbo ambao
unaigusa jamii nzima kwani
mambo ya kuchuna mabuzi kwa
wanawake yapo sana, hata mimi
mwenyewe ni mtaalamu wa
kuchuna mabuzi,” alisema
Shilole.
Hata hivyo alisema japokuwa ana
tabia hiyo lakini anatambua siyo
nzuri hivyo anawasihi wanawake
wengine kuachana nayo kwani
ipo siku itawaingiza matatizoni.
Mbali na mchungaji huyo, juzi
Jumapili, Mchungaji wa Kanisa la
Anglikana, Ukonga –Mazizini, Dar,
Emmanuel Kapande alimtumia
ujumbe wa watoto wa Shule ya
Jumapili (Sunday School)
nyumbani kwake kwa lengo la
kuimba na kufanya maombi.
Watoto hao walifika nyumbani
kwa Shilole, Mwananyamala -
Manjunju, wakiwa
wameongozana na walimu wao,
Jonas Timotheo, Rehema Ezra na
Catherine Libogoma.
Ujumbe huo, ulimpelekea baraka
ya maombi nyumbani kwake na
kumshauri aishi katika mazingira
yanayompendeza Mungu.
Katika hafla hiyo, vinywaji baridi
vilichukua nafasi yake huku
Shilole akipata nafasi ya
kuzungumza na watoto hao kisha
kupiga nao picha.

NYAMA YA ULIMI MPE LAAZIZI WAKO

MMMH mshaanza eti nimeisha
ingia mama Chaunabe kitanga na
njia nisiye na bleki kwenye domo
langu, wahenga wanasema
kinywa cha mkubwa kinanuka
lakini maneno hayanuki. Najua
maneno yangu ya shombo
huenda hayakufurahishi wewe
ambaye kila kukicha unabadili
wanaume na kuonekana una hila.
Shutuuu dada mwanamke tabia
babu wee, mwanamke kujua
mumeo anataka nini, mwanamke
kujituma kwenye kiwanja kifupi
cha sita kwa sita.
Unasahau cha kumvutia
mwanaume unakimbilia
kuukoboa mwili nani kakuambia
weupe mali? Basi mkaa usinge
nununuliwa!
Tena leo nakazi na wewe, nani
kakuambia weusi ni laana. Basi
leo nataka nikuambie wewe usiye
na haya uliyemaliza vipodozi
mwisho wa siku uso
unakuparama kama mchawi
mzee, unalo hilo?
Siri ya weusi maana yake ni
utamu hata zambarau tamu ni
nyeusi, zabibu tamu ni nyeusi na
hata usingizi mtamu unapatikana
usiku mweusi. Huoni Mzungu
akimuonja mswahili
anachanganyikiwa.
Wewe unajikoboa Mzungu ajipake
masizi? Acha ubwege. Nimejikuta
hata nikisahau kuelezea
nilichokikusudia kwa ajili ya
malimbukeni wachache, jivunie
weusi wako babu wewe.
Tuachane na hayo ambayo kwa
kiasi nimejikuta nikipandwa na
mzuka na kuingia kwenye mada
nyingine. Kama unabisha
mwangalie jirani yako
anayetumia mkorogo ngozi kama
kuku wa mayai aliyezeeka badala
ya kupendeza anabakia kituko
mtaani.
Acha niendelee na kilicho nitoa
nyumbani, shoga leo nilitaka
kukuelezea kitu kimoja
kuhusinana na tabia za baadhi ya
wanawake kukosa lugha tamu
ndani ya nyumba zao kushindwa
kuwalisha waume zao nyama ya
ulimi. Mwanamke unakosa lugha
tamu kwa mumeo hujui kusema
asante, hujui kusema samahani,
hujui hata kumsifia mumeo!
Mumeo akikuletea kitu
unakipokea na kuamnini ni
wajibu wake kukuletea una hiyari
ya kusema asante au kukaa
kimya. Lakini nataka nikuambie
shoga kitu kinacho mtuliza
mwanaume ni pamoja na
maneno matamu. Mfano amerudi
toka kazini baada ya kumpokea
lazima umpe pole ya kazi.
“Karibu mpenzi pole na kazi,”
akikujibu asante, mwambie.
“Yaani kila muda jicho langu
lilikuwa likitazama barabarani
utarudi saa ngapi mpenzi
wangu,” hata kama ulikuwa ndani
ukiendelea na kazi zako.
Vitu hivi humfanya mwanaume
kuamini kabisa hata anapokuwa
mbali nawe bado ulimuweka
moyoni mwako, siyo anakuja
baada ya kumpokea unabakia
kama bubu haipendezi, tumia
ulimi wako kumliwaza mumeo.
Mpo katika safari ya huba mkifika
pwani lazima mpeane pole na
asante kwa kusafiri salama,
pengine wewe umewahi mwenzio
naye anakufuata pwani msaidie
naye afike pwani na baada ya
kufika mpe pole pia kumpa
asante kwa kukusafirisha vyema
katika bahari ya huba.
Usiwe uvivu wa kuomba
msamaha unapokosa, hata kosa
lenyewe liwe dogo, kumbuka
kosa ni kosa na chanzo cha moto
ni cheche. Wapo wachache lugha
tamu huzitumia kwa muuza
genge ili apunguziwe lakini kwa
mumewe vitu hivyo havionekani.
Tumia ulimi wako kujenga
nyumba yako kumfanya mumeo
aone tofauti ya mwanamke wa
nje na mkewe ambaye kila neno
tamu na zuri humwambia
mumewe. Nyama ya ulimi
ukiitumia vizuri itakufanya kila
siku penzi lako lizidi kuwa tamu,
si wajinga waliosema sauti tamu
ilimtoa nyoka pangoni na
kumtuliza simba mwenye njaa.
Yangu si mengi kwa leo, ila
kumbuka wimbo mzuri
humbembeleza mtoto akalala.

KIDUME ANASWA AKIJIUZA ( ATOA URODA WA TIGO)

AMA kweli dunia imefika
ukingoni! Ile Oparesheni Fichua
Maovu (OFM) ya Global
Publishers, bado ipo kazini
ikishirikiana na polisi ambapo
safari hii imeibuka na kigongo
cha aina yake baada ya kumnasa
‘mwanaume tata’ akijihusisha na
ukahaba, Risasi Mchanganyiko
lina mzigo kamili.
Ikiwa kwenye fumuafumua ya
magenge ya ngono maeneo ya
Kahumba mjini Morogoro hivi
karibuni, OFM kwa mwaliko wa
jeshi la polisi, ilipigwa na butwaa
baada ya kukutana uso kwa uso
na mwanaume huyo aliyekuwa
amejumuika katikati ya kundi la
madadapoa naye akifanya kama
wao.
Mbali na jamaa huyo ambaye jina
lake halikupatikana, baadaye
ilibainika kuwa kulikuwa na
wenzake wawili ambao ilikuwa
vigumu kuwatambua kufuatia
kujiremba kupita hata wanawake
wenyewe.
Kuna madai kwamba kijana huyo
aliyekadiriwa kuwa na umri wa
kati ya miaka 20 - 24 ni mtoto wa
kigogo serikalini na amekuwa
akijichanganya na madadapoa
hao kwa muda mrefu.
Mara baada ya kunaswa, kijana
huyo aliangua kilio huku akidai
kuumbuka kwani familia yake
wakiiona picha yake
hawatamwelewa.
“Naombeni tumalizane hapahapa
kwani nyumbani hawafahamu
kuwa nipo hapa muda huu. Hii ni
kesi kubwa kwangu nisaidieni,”
alisikika kijana huyo.
Hata hivyo, pamoja na kilio
hicho, polisi hawakumwelewa,
alibebwa juujuu na kuingizwa
katika karandinga kisha kutupwa
nyuma ya nondo za mahabusu
kusubiri sheria kuchukua mkondo
wake.
Wakazi wa maeneo hayo
walikuwa wakilalamika mara kwa
mara kutokana na kurundikana
kwa makahaba mahali hapo na
kusababisha uchafuzi wa
mazingira kwa kutupa ovyo
mipira ya kiume (kondom).
Katika msako huo, wanaume hao
watatu walijumuishwa na
wanawake 20 waliokamatwa
wakijihusisha na biashara
haramu ya kuuza miili.
-GPL

LAANA BINTI APIGA PICHA ZA UTUPU NA KUZIACHIA FACEBOOK LOOH!!

Amepiga picha na kuzisambaza
facebook mungu atunusuru na
haya majanga yakina dada
ambao wana piga picha za uchi
na kuweka kwenye mitandao ya
kijamii JINA analo tumia
facebook ni JESSICA KIKUMBI
TAFADHALI KURINGANA NA
MAADILI KUANGALIA PICHA
SHARITI UWE NA UMRI +18 NA

HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI....!

Wapenzi na wanandoa wengi hivi
leo wanapoingia kitandani tayari
kwa kuianza safari ya kupeana haki
zao za msingi hushindwa kufurahia
tendo na hasa hali hii hujitokezwa
kwa wanawake kwani mwanaume
huwa na haraka iliyopitiliza!
Mwanaume atamkumbatia na
kumbusu mwanamke kwa muda
mfupi na kabla hata hamasa ya
mapenzi ya mwanamke ahaijashika
hatama, atamwingilia na ndani ya
dakika sekunde ama dakika
zisizozidi 3, mwanamme hufika
mshindo.
Katika hali ya kusikitisha baada ya
mwanaume kujitosheleza hujongea
pembeni bila kujali mwenza wake
hajafika mwisho wa safari hali
inayosababisha mwanamke
kupoteza hamu ya tendo endapo
endapo tabia hiyo ya mwanaume
itaendelea.
Kunahatua nne muhimu ambazo
wapendanao wakizishika na
kuzitekeleza ipasavyo basi
watafanikiwa kujitosheleza kila
wanapokutana na kwa hakika
watakuwa miongoni mwa watu
wachache wanaofurahia faragha
kila wakutanapo!
Hatua ya kwanza ni
kusameheana:
Wanandoa wengi hushindwa
kupata raha ya mlo wa usiku
kutokana na kushindwa kumaliza
tofauti zao kabla ya giza
halijaingia, mgogoro wowote baina
ya wapendanao ni lazima
umalizwe kabla ya kukutana kwa
ajili ya mlo wa usiku. Hii husaidia
kuondoa kinyongo miongoni mwao
na kuwafanya mioyo yao igubikwe
na upendo ambao humfanya
ahamasike kunako majambo!
Hivyo basi endapo unataka
kufurahia mambo fulani hakikisha
unamaliza tofauti, ombaneni
msamaha na samehaneni kwa
dhati kwani kwa kufanya hivyo
kutawasaidia muwapo faragha
kufurahia kile mnachokifanya kwa
kuwa mtakuwa mmemalzia tofauti
zenu.
Hatua ya pili ni mchezo ya
mahaba:
Mashamsham hunoga na kupamba
moto kiasi cha kumfanya yoyote
aliye kwenye uwanya wa raha
kusahau kwa muda shida na
matatizo yanayomuandama pale
anapokutana an mtu anayeweza
kumpagawisha kwa michezo ya
mahaba kabla ya kuianza safari
yenyewe!
Michezo hii husaidia kuamzsha
hamasa na muhemko baina ya
wapendanao, hivyo ili wapendanao
waweze kufika mwisho wa safari
pamoja na kila mmoja alidhike na
udereva wa mwenzake
uliowafikisha safari yao lazima
watumiye muda wakutosha katika
michozo yakimahaba!
Hata hivyo kila mmoja wenu
anapaswa kuujua mwili wa
mwenza wake. Mwili wa
mwanaume ni rahisi kuuelewa
kwani una sehemu moja kuu
ambayo ni kama kiini cha
muhemko na msisimko wa
mapenzi. Sehemu hiyo ni uume.
Hivyo endapo mwanamke yoyote
atatumia muda wakutosha
kuhangaika na sehemu hiyo basi
mambo huwa safi kwa upande wa
mwanaume.
Mwili wa mwanamke una shughuli
pevu kubaini sehemu zenye
ambazo huamsha hisia za mapenzi
na ndiyo maana wanaume wengi
hushindwa kuwafikisha mwisho wa
safari wapenzi wao. Kiini cha hisia
za mapenzi kwa mwanamke ziko
kwenye kipegere G (namaanisha
critoris wadu, haya ni mambo ya
infenizimu tu). Kipegere G kipo nje
ya uke ambapo wataalamu hudai
kuwa kipo sentimita 4 kutioka
ukeni.
Wanaume wengi wanaelewa hili
lakini walio wengi wamegubikwa
na imani potofu kuwa, kwa
kuingiza kidole ukeni watafanikiwa
kuinua hamasa ya za wenza wao
kutaka kuanzisha safari jambo
ambalo si kweli, kwani wanawake
wengi hujisikia vibaya kuingizwa
vidole ukeni kutokana na ukweli
kwamba kucha zinabeba uchafu na
bakteria wengi ambao
huwasababishia kupata fangasi!
Hivyo basi, endapo wewe ni
miongoni mwa wanaume
waliokuwa wakiaminin dhana hii
nataka nikujulishe kuwa, ukitaka
kumpa msisimko uliotukuka
mwenza wako usiangaike kuingiza
kidole chote ukeni badala yake
hakikisha unatumia kidole chako
(hakikisha si kikavu) kucheza na
sehemu ya nje ya uke ambapo
utakutana na kipegere G na lips za
ndani. Hata hivyo usisahamu
kuhangaika na uke pia lakini hasa
shughulika na sehemu za nje!
MUHIMU KUJUA: Mwanaume
huahamasika kwa sekunde kadhaa
lakini mwanamke humchukua
takriban dakika 20 kuweza
kuamsha hisia zake na kumfanya
awe tayari kwa kuianza safari!
Hivyo, mwanaume mwenye busara
yaani asiye mbinafsi huakikisha
anatumia muda wakutosha
kumuuanda mwenza wake kabla ya
kuanza safari! Hivyo mwanaume
anapaswa kunza michezo ya
mahaba kwa kuzingatia hatua tatu
muhimu ambazo ni:-
Sehemu ya juu:
Wanume wengi kutokana ana
haraka zao hukimbilia sehemu ya
chini ya mwili wa mwanamke
yaani kunako na kuanza ama
kupapasa kwa kidole chake ama
ulimi na baada ya sekunde chache
huanza kumwingilia mwanamke,
lakini mwanaume mwenye kumjali
ampendaye na mwenye nia hasa
yakumfikisha kwenye kilele cha
raha huwa hana papara
huhakikisha anamhagi na kumpiga
mabusu sehemu ya juu ya mwili
wake yaani mdomoni, shingoni,
kwenye matiti, chuchu etc.
Hata hivyo, si wanawake wote
wako sawa, kuna amabo hufurahia
kutomaswa maziwa yao huku
wengine wakichukizwa kutokana na
sababu mbalimbali kwa mfano
kama mwanaume ni mtu
wamitungi ama mvuta sigara
mara nyingi kinywa chake hutoa
harufu mbaya hivyo huwa vigumu
kwa mwanamke asiyependezewa
na matumizi ya vitu hivyo
kufurahia kupigwa denda!
Kimsingi mwanamke kama kweli
unampenda mpenzi wako na
unataka ufurahie majambozi
anayokupa hakikisha unakuwa
muwazi kwa kuanza na
kumuonyesha sehemu zinazokupa
hamasa ya kufanya mapenzi, si
lazima ushike mkono wake na
kuupeleka kunako hiyo sehemu!
Hakikisha pindi mwanaume
anapokugusa sehemu
inayokusisimua unamwonyesha
wazi kuwa hapo unasikia utamu
yaani kama miguno ilikuwa haitoki
hakikisha inaanza toka, kama
pumzi zilikuwa zatoka kawaida basi
zianze toka isivyo kawaida,
nachomaanisha hapa ni kuwa
unapaswa kuonyesha umepagawa
kwa raha unayopata basi kwa
mwanaume aliye kamili hatasita
kuishughulikia kikamilifu sehemu
hiyo!
Sehemu ya chini:
Baada ya kumtomasa kiasi cha
kutosha sehemu ya juu ya
mwanamke, mwanamke huhitaji
kutomaswa sehemu ya chini na
hapa ndipo ambapo unaweza
kuhisi anataka kuingilia mana
huanza ama kujishikasiika sehemu
za chini ama hukupeleka maeneo
yake nyeti upate kumwingilia kwani
huwa amehamasika na ilim kujua
kama amaehamasika basi uke
wake huwa unamajimaji ambayo
hutoka kwa ajili ya kulainisha nyia
ya kupita bwanamkubwa yaani
uume.
Hata hivyo, ili mchezo uwe mtamu
mwanaume anapaswa kuhakikisha
anatumia dakika kadhaa kuuchezea
uke na kufuatia kinena. Hapa
ieleweke kuwa kuna wanawake
baada ya mizuka kuwapanda
hutokwa na majimaji mengi
sehemu zao za siri hivyo endapo
mwanaume ukikutana na hali hiyo
usishutuke jua mzuka imempanda
mpenzi wako tu na si vinginevyo!
Katika kuchezea sehemu zake za
siri mwanaume anapaswa kujua
kuwa kuna wanake wanapenda
chezewa kinena pekee na wengine
hupenda mwanaume atumie ulimi
ama akidole chake (kisiwe kikavu)
kuingiza ukeni huku kidole kingine
kikitomasa kinena hali
inayomsisimua mwanamke. Hivyo
mwanamke anapaswa kuwa
muwazi nini anapenda kufanyiwa!
Katika kipindi hiki mwanamke naye
anatakiwa kutoa ushirikianao wa
miguno na viuno vya hapa na pale
kuashiria anapata raha na
asisahau mptomasa mwanaume,
lakini ikumbukwe kuwa
mwanaume ana sehemu kuu moja
inayomtia wazimu ambayo ni
uume wake hivyo ni rahisi kwa
mwanaume kufika mshindo hata
kabla ya tendon a hapo ndipo
tatizo huibuka kwani wengine
baada ya tendo moja huwa
hawana uwezo wakurudia
mzunguko wa pili!
Nini mwanaume anapashwa
kufanya sasa ili kuhakikisha
hamalizi mzungoko haraka?
Anapaswa kuwa muwazi kwa
mwenza wake endapo mwenza
wake atakuwa anamshika sehemu
ambayo inamnyegesha sana na
kumfanya ajisikie kumaliza
biashara basi amueleze wazi kuwa
aiache sehemu hiyo kwa muda ili
uweze kudumu kunako
majambozi!!
Hata siku moja msifanye mahaba
kimya kimya! Simaanishi mpige
mikelele hadi iwe kero kwa
majirani na nk, elezenaneni kwa
sauti za mahaba nini kila mmoja
wenu anapenda mwenzi wake
afanyiwe na mwenza wake.
Hatua ya tatu:
Kuingiliana kimwili
Mwanaume anapaswa kuahkikisha
amasa za mapenzi za mwanamke
zimeamka kabla ya kumwingilia.
Wanaume wengi kutokana na
papara hujikuta wanawaingilia
wenza wao hata kabla
hawajahamasika na hatimaye
kumaliza tendo pasipo kuwafikisha
kileleni na hili ni tatizo la kawaida
kwa wapenzi wanaokutana kwa
mara ya kwanza na has
amwanamke akiwa na zile nataka
sitaki yani atasumbuana na
mwanaume weeeee na hatimaye
hadi dume lifanikiwe kumwingilia
kimwili inakuwa kama mbakano tu!
Hivyo basi, mwanaume unapaswa
kujua kweli mpenzi wako yuko
tayari kwa tendo la ndoa na utajua
kwa kungalia kwanza mashavu ya
uke wake kama yamekakamaa na
kuongezeka ukubwa huku kinembe
chake kikionyesha kukaza na
mwanamke akifikia hali hii basi
mwanaume huweza kuingiza
uuume wake ambao umesimama
kiurahisi kwani kuta za uke
zitakuwa na ute unaoteleza huku
uume nao ukiwa na ute unaotoka
sehemu ya mbele kabisa hali
inayowafanya wapendanao
kufurahia tendo kwani
hawataumizana!

MAPENZI MATAMU YANA HITAJI UBUNIFU KATIKA MAPENZI KUONGEZA LADHA KWA MWENZI WAKO

Ukweli ni kwamba kitu chochote
tunachokifanya katika maisha
yetu kinahitaji ubunifu ili
kukiboresha kuwa kizuri zaidi
vivyo hivyo katika mapenzi
mwanamke na mwanamume
wanahitajika kuwa wabunifu
katika mambo mbalimbali mfano
kwa mwanamke ambapo kwa
asilimia nyingi inasemekana
mwanamke akiolewa na kupata
mtoto wengi wao wanajisahau
katika mapenzi kama kupika,
usafi wa nyumba na mwili,
matumizi mabaya ya pesa,
mahaba motomoto na vitu
vingine vingi vinavyoendana na
hivyo JAMBO LA MSINGI
TUKUMBUKE KUWA WABUNIFU
naichukia sana kauli ya kusema
"Mwanamume ama mwanamke
hata umfanyie nini haridhiki" hii
ni kauli potofu na ni kujikatisha
tamaa na mwisho wa siku
kujibweteka na kumpoteza
mwenza wako MAPENZI MATAMU
YANAHITAJI UBUNIFU

HAYA NDIO MAISHA YA DIAMOND KILA SIKU ASUBUHI:

msanii huyu amekuwaakijiimalisha vyema katika mazoezi ya mwili kila anapo hamka asubuhi tazama matukio katika picha

SIAMINI NINA MWAKA KWENYE NDOA LEO NDIO NINAGUNDUA MKE WANGU ANA TATTOO YA JINA LA MWANAUME MWINGINE

Habari Wadau wa Udaku...
Leo nimeuzika sana wadau
Asubuhi wakati napata morning
Glory kwa Mke wangu
nimegundua Kwenye Titi Sehemu
ya chini ana Tatto imeandikwa "I
lov u James" kwa Maandishi
Madogo sana kama haupo makini
unaweza usiyaone...
Nimekaa nae Mwaka mzima Leo
ndio nakuja ona Nilivyojaribu
kumuuliza anakuwa mkali na
kusema ni jina la Ex Wake kabla
hajakutana na Mimi....Wadau
Hapo Mnanishaurije ? Kila
nikiona hiyo Tatoo Am Sure Mood
zitakuwa zikiniisha

VIJANA WAHIMIZWA KUJISHUGHULISHA NA KILIMO MKOANI MBEYA

SEKTA za elimu na kilimo ni
miongoni mwa zile zilizoingizwa
katika mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (BRN).
Lengo la serikali katika mpango
huo ni kuona sekta lengwa
zinapiga hatua za haraka na kuwa
na tija kwa watanzania. Ni kwa
kutambua umuhimu wa mpango
huo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,
Abbas Kandoro aliamua kufanya
ziara ya siku tatu wilayani Mbozi ili
kuona maandalizi ya utekelezaji wa
mpango wilayani hapo.
Dhana iliyopo ni kwamba mpango
huo, BRN, hauwezi kufanikiwa
iwapo hakutakuwa na maandalizi
stahiki ambayo pia kama ulivyo
mkakati wenyewe lazima nayo
yafanyika kwa haraka zaidi
sambamba na usimamizi mzuri wa
mpango mzima. Akiwa wilayani
hapa, Kandoro alijikita zaidi katika
sekta mbili hizo, elimu na kilimo
ambazo ni nguzo muhimu katika
suala zima la maendeleo kwa
wananchi wa wilaya hii.
Ukaguzi wa miundombinu ya
kilimo hususani maghala ya
chakula, matumizi sahihi ya pesa
zinazotolewa na serikali pamoja na
maabara mashuleni ni miongoni
mwa mambo aliyoyazingatia
kwenye ziara yake.
Kujiunga katika vikundi
Kandoro aliwahimiza wakulima
wilayani hapa kujiunga katika
vyama vya ushirika kwa kuwa ni
muhimu katika kuwasaidia kupiga
hatua kimaendeleo.Kwamba mbali
na ukweli kuwa umoja na nguvu,
vikundi vya ushirika vinakopesheka
kirahisi tofauti na mtu anapokuwa
mmoja mmoja.
Aliwataka wakulima kutokatishwa
tamaa na kasoro za viongozi
wachache wanaokwamisha vikundi
vyao au vyama vya ushirika
kushindwa kufikia malengo ya
kuwasaidia wanachama wake.
Alisema jambo muhimu kwa
wakulima ni kutambua kuwa
vyama vya ushirika pia vinaweza
kuwatetea hata katika kupata
maslahi stahiki kwa kuuza mazao
yao. Kupitia vyama vya ushirika,
Kandoro alisema serikali mkoani
hapa imelenga kuhakikisha mfumo
wa stakabadhi ghalani unatumika
na kuwawezesha wakulima
kuondokana na kutapeliwa na
wafanyabiashara wanaokwenda
kuwalaghai majumbani wakiwataka
kuwauzia mazao kwa bei rahisi.
Akizungumza na wanachama wa
kikundi cha wakulima wa kahawa
cha Iganda kilichopo kijijini Isansa,
Kandoro alisisitiza msimamo wa
serikali ya mkoa kuona kwamba
mkulima hauzi kahawa mbichi
badala yake aikaushe mwenyewe.
“Stakabadhi ghalani inaambatana
na uwepo wa maghala.
Ndiyo sababu tumenuia kukarabati
jumla ya maghala 54 kwa wilaya
yote ya Mbozi na kwa kuanza
tutakarabati kwanza maghala 24.
“Tunataka msimu wa kuvuna
kahawa unapoanza mfumo huu
uwe umeanza kufanya kazi. Kwa
maana hiyo kahawa itakayovunwa
itakusanywa kwa mfumo huo na
kuhifadhiwa katika maghala
haya.“Tunataka wakulima wawe na
sauti itakayowawezesha kunufaika
na jasho lao,” alisisitiza.
Mkuu huyo wa mkoa amesema
ataangalia uwezekano wa
kukisaidia kikundi hicho kupata
mashine kubwa ya kukoboa
kahawa kwa kuwa iliyopo hivi sasa
ina uwezo mdogo wa kufanya kazi,
hali inayosababisha baadhi ya
wakulima kwenda kwingineko
kukoboa kahawa yao.
Vijana na kilimo
Katika ziara hiyo, Kandoro
aliwapongeza wakazi Mbozi kwa
kuendelea kujituma katika kilimo
huku akisema kwamba ni lazima
jamii ikubali kuwa kilimo kitabaki
kuwa ajira kubwa ya watanzania
na hivyo kinachotakiwa ni serikali
kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali kuzidi kuboresha
miundombinu yake.
Mkuu huyo wa mkoa anaamini
kwamba miundombinu ikiwa bora
wakulima nao watafanya shughuli
zao kwa urahisi zaidi. “Na vijana
wanapaswa watambue kuwa si
kweli mijini kuna maisha bora.
Wengi wanadanganyika kukimbilia
huko na kuacha ajira hii.
Wanakwenda kuishi maisha
magumu mijini na kuishia
kujiingiza kwenye biashara zisizo
na tija wakati wangeweza kujiajiri
vijijini kwao kwa kulima mazao
kibiashara,” alisema.
Alisema ni vyema sasa jamii ikawa
na mtazamo kuwa vijana
wanaweza kunufaika na kilimo
wakiamua na kuwa serikali ya
mkoa itazidi kuandaa mikakati
mbalimbali ya kufanya kilimo kiwe
na tija.
“Nawapongeza kwa kuona mnazidi
kujituma. Mazao yanastawi vizuri
hali inayoonesha kwamba
mmetumia utaalamu. Tutazidi
kuleta wataalamu kila
inapowezekana ili waweze
kusaidiana nanyi,” alisema.
Kujaribu mazao mengine
Katika kijiji cha Senjele, mkuu
huyo wa mkoa alibaini kuwa ardhi
na hali ya hewa ya ukanda wa juu
wa wilaya ya Mbozi usiokubali
kilimo cha kahawa unaweza
kustawisha zao la korosho.
Hii ilikuja baada ya kushuhudia
miti ya korosho ikiwa imestawi
vyema katika viunga vya Shule ya
Sekondari ya Shikula.
“Halmashauri kwa kushirikiana na
ofisi ya kilimo mkoa angalieni
namna mnavyoweza kuhimiza
kilimo cha korosho katika ukanda
huu. Hawa hawajapanda kama
urembo hapa.Wasaidieni pia dawa
ya kupulizia hawa waliokwisha
anza. Ni zao linaloweza kuinua
uchumi wa Wanambozi
tukilihamasisha kulimwa,”
anasema.
Ufisadi na kutowajibika
Hata hivyo, Kandoro aliweza
kubaini kasoro kadhaa zinazoweza
kukwamisha matokeo ya haraka
katika sekta ya kilimo wilayani
Mbozi. Kasoro hizo ni matumizi
mabovu ya fedha za serikali katika
utekelezaji wa miradi ya
miundombinu ya kilimo pamoja na
baadhi ya wataalamu kutowajibika
ipasavyo.
Moja ya maeneo yaliyobainika
kuwepo na ufujaji wa fedha za
serikali ni katika mradi wa
umwagiliaji wa Iyula B uliopo
katika kata ya Iyula. Hapa Kandoro
alibaini kuwepo na upotevu wa
fedha kiasi cha zaidi ya Sh milioni
115.
Awali katika taarifa iliyosomwa na
ofisa kilimo na mifugo wa kata ya
Iyula, Khalid Mchomvu
alibainishwa kuwa ujenzi wa banio
la maji la mradi huo umegharimu
kiasi cha Sh 255,710,000 na
unatarajia kunufaisha jumla ya
kaya 268 zitakazolima ekari 210 za
kilimo cha umwagiliaji zikiwemo
ekari mbili zilizotengwa kwa ajili ya
vijana.
Kilichomkera mkuu wa mkoa ni
baada ya Ofisa Kilimo na Mifugo
wa Halmashauri ya Wilaya, Richard
Siliri, kueleza kuwa zinahitajika
fedha nyingine kwa ajili ya
kupasua kwa baruti jiwe kubwa
linalozuia maji kupita kwenye
mfereji pamoja na kuusakafia
mfereji huo wenye urefu wa
kilometa tisa.
Hapo ndipo mkuu wa mkoa
aliposema hakuna sababu ya
mradi huo kuombewa fedha
nyingine wakati hesabu za
kiukaguzi zinabainisha kuwa kutoka
mfuko wa maendeleo ya kilimo wa
wilaya (DADPs) walikwisha pewa
zaidi ya Sh milioni 250 na
walizotumia hadi mradi ulipofikia
ambapo ujenzi wa banio
umekamilika ni Sh milioni 134.
Fedha hizo walipewa kwa awamu
mbili ambapo awamu ya kwanza
walipewa zaidi ya Sh milioni 115
na ya pili wakapewa zaidi ya Sh
milioni 134. Akahoji ni kwa nini
taarifa ya ukaguzi inayobainisha
matumizi ya Sh milioni 134 hadi
mradi huo ulipofikia zinatofautiana
na taarifa za watendaji hao.
Akasema kuna uwezekano mkubwa
kuwa fedha hizo zilitafunwa na
wachache kwa manufaa yao.
“Nasema fedha mnazo kwa mujibu
wa taarifa za ukaguzi. Mnaweza
kukamilisha ujenzi wa mfereji na
zikabaki. Mliomba jumla ya Sh
milioni 340 kwa ajili ya utekelezaji
wa mradi na tayari mmepewa zaidi
ya Sh milioni 250 na mmetumia Sh
milioni 134 hizi nyingine ziko
wapi?” Akahoji.
Akaendelea: “Nawahakikishia
ndugu zangu wananchi kuwa
tutashirikiana kuhakikisha fedha
zenu zinajulikana zilikokwenda.
Hatuwezi kukubali miradi ya
serikali kukwama kutokana na
wajanja wachache kujinufaisha.”
Akizungumza na waandishi wa
habari, mwenyekiti wa kamati ya
usimamizi wa mradi huo, Jua
Mwamlima, alisema fedha za
mradi zilizokwishatolewa kwenye
akaunti ni zaidi ya Sh milioni 250
na zilizosalia kwenye akaunti hiyo
ni Sh 500,000 pekee.
Akasema wanachojua wanakamati
ni kuwa fedha zote zilitumika
kwenye mradi hadi ulipofikia hivi
sasa kwa kuwa nyaraka zote za
malipo zilikuwa zikiandaliwa na
kufanywa na maofisa wa ngazi ya
juu na wao kupelekewa kwa ajili ya
kutia saini pekee. Ubadhirifu
mwingine ukabainika katika kijiji
cha Msiha.
Sh milioni 100 zilizotolewa na
serikali kwa ajili ya ujenzi wa
bwawa la maji ya kutumia
majumbani pamoja na kilimo cha
umwagiliaji katika kijiji hicho
haijulikani zilipo. Kufika kwa
Kandoro kijijini hapo kulilenga
kuona namna miundombinu ya
bwawa hilo ilivyojengwa akijua
kwamba lilikwishafikia hatua nzuri
tayari kuanza kuwanufaisha
wananchi walengwa wanaokabiliwa
na uhaba wa maji kwa ajili ya
matumizi ya majumbani na pia
kwa ajili ya kilimo.
Baada ya kufika na kukuta hakuna
lolote lililofanyika ndipo mkuu
huyo wa mkoa aligeuka mbogo na
kutaka ofisi ya kilimo imueleze
ilimpeleka hapo kufanya nini
wakati hakuna miundombinu na
pia akataka kujua fedha zote
walizopewa zilifanya kazi gani.
“Sasa hapa naomba mnieleze
mmenileta kufanya nini?
Mimi nilijua kuna miundombinu
iliyokwishajengwa tayari kwani ni
muda mrefu tangu mmepewa
fedha. Je, mlinileta kuja kushangaa
mandhari ya pori hili na kusimama
simama tu kama hivi?” akahoji.
Kwa mujibu wa Kandoro, ofisi ya
kilimo wilayani hapo katika mwaka
wa fedha 2010/2011 ilipewa kiasi
cha Sh milioni 40, na mwaka wa
fedha 2012/2013 ikapewa kiasi cha
Sh milioni 60 lakini fedha hizo
hazijulikani ziliko na hakuna kazi
yoyote iliyoanza kufanyika mpaka
anafika eneo la mradi.
“Mimi nilitaraji leo nakuja kuona
miundombinu iliyolenga kusaidia
kuweka mtiririko mzuri wa maji ili
maji hayo yasaidie kulima kwa
uhakika. Hakuna kitu hapa! Wewe
mwenyewe hauna uhakika na
kilichoendelea katika Sh milioni
100 zote zilizoletwa,” akasema
Kandoro akimwambia Ofisa kilimo
na mifugo wa wilaya ya Mbozi,
Richard Sirili.
“Hii haikubaliki hata kidogo na
nasema lazima tuchukue hatua
hata polisi watu watapelekwa.
Nimeshtuka pesa ni nyingi mno.
Serikali inaleta pesa hakuna
kinachofanyika. Hatuwezi kwenda
kwa mwendo huu ndugu zangu,”
alisisitiza.
Mmoja wa wakazi wa kijiji cha
Msiha, Mawazo Mwamlenga
alisema bwawa hilo linasubiriwa
kwa hamu kubwa na wakazi wa
kijiji hicho kutokana na kukabiliana
na uhaba mkubwa wa maji kwa
ajili ya matumizi ya majumbani na
kuendeshea kilimo cha
umwagiliaji, alichosema kitaweza
kuwakomboa kuondokana na
umasikini.
Kuendelea kusuasua kwa ujenzi wa
bwawa hilo ilhali wakazi wanayo
taarifa kuwa serikali ilikwishatoa
fedha kunaonesha kama kwamba
wakazi hao wametumika kama
mtaji wa kunufaisha wajanja
wachache wasio na huruma kwao.
Katika kata ya Myovizi, Kandoro
alikutana pia na malalamiko
yanayokwamisha maendeleo ya
kilimo.
Kubwa ni mtaalamu wa kilimo
kulalamikiwa kwa kutowajibika
ipasavyo kwa wananchi aliopewa
jukumu la kuwatumikia kutokana
na utaalamu wake. Ofisa huyo,
Rehema Mwandurusa, mbali na
kudaiwa kuishi mbali na kituo
chake cha kazi wakazi wa kijiji cha
Ichesa katika kata hiyo wanasema
wamekuwa wakiishi kama hawana
mtaalamu wa kilimo hivyo
kulazimika kuendesha shughuli zao
pasipo utaalamu wowote.
Mwenyekiti wa halmashauri wa
wilaya ya Mbozi, Eliki Ambakisye
pia akakiri ofisa huyo kukaidi agizo
la kumtaka aishi eneo lake la kazi
na badala yake amekuwa akiishi
katika mji mdogo wa Mlowo uliopo
takribani kilomita kumi kutoka
eneo hilo. Akasema kwa kuishi
mbali na eneo la kazi ofisa huyo
amekuwa akifika kwa kusuasua
sana katika eneo hilo, hivyo uwepo
wake hauwasaidii wananchi
aliopewa dhamana ya
kuwatumikia.
Kufuatia malalamiko hayo,
Kandoro akamuagiza ofisa huyo
kuchagua jambo moja kati ya kazi
na kuishi anakotaka yeye ili nafasi
yake apewe mtu aliye na utayari
wa kuishi katika eneo lake la kazi
ili kuwatumikia wananchi.
Uhaba kidato cha sita
Upande wa sekta ya elimu nao
ulikuwa na yake. Cha kwanza
kilichojitokeza ni uhaba wa shule
za sekondari kwa ajili ya elimu ya
kidato cha tano na sita.Katika
eneo hilo, Kandoro alifurahishwa
na uamuzi wa wakazi wa kata ya
Myovizi kuongeza vyumba vya
madarasa na kujenga mabweni
kwa ajili ya kidato cha tano na
sita. Mkuu huyo wa mkoa aliahidi
kuchangia Sh 500,000 kwa ajili ya
ujenzi wa vyumba vya madarasa
unaoendelea.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka pia
wanafunzi wanaosoma michepuo
ya sayansi katika shule zilizo
wilayani hapo kutambua kuwa
wanalo jukumu la kuikomboa nchi
kuondokana na changamoto ya
uhaba wa walimu wa masomo ya
sayansi. Akaziagiza halmashauri
kuziwezesha shule zilizo na
maabara kwa kuzifungia umeme
wa mionzi ya jua ili kutoa fursa
kwa wanafunzi kujifunzwa kwa
vitendo wakati wowote.
Mimba mashuleni
Lakini suala la mimba kwa
wanafunzi likaonekana kuwa ni
changamoto nyingine inayopaswa
kuendelea kutafutiwa ufumbuzi.
Mkuu wa mkoa aliagiza hatua za
kisheria kuchukuliwa dhidi ya
wahusika wa mimba za wanafunzi,
ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha
wazazi wanaokwamisha kesi za
mimba kutofanyika kisheria.
Ni katika kulipa uzito jambo hili
alitoa muda wa siku saba kwa
ofisa mtendaji wa kata ya Nanyala,
Theofrida Hankungwe kuhakikisha
amewasilisha taarifa za hatua
zilizochukuliwa kwa wanafunzi
watano wa kike waliopata mimba
mwaka 2013 katika Shule ya
Sekondari ya Shikula.
Agizo hilo pia lilitolewa kwa mkuu
wa shule hiyo, Chonge Dafa
ambapo kwa pamoja viongozi hao
wanapaswa kueleza ni hatua zipi
zilichukuliwa kwa wanafunzi
waliopata mimba na pia
waliosababisha. Wanafunzi hao ni
pamoja na mmoja aliyepewa
mimba na mwanafunzi mwenzake
ambapo wote walifukuzwa shule.
“Kumekuwa na mchezo wa baadhi
ya wazazi kumaliza kesi za mimba
kiundugu kwa kupeana pesa au
mali nyingine badala ya kupeleka
kesi hizo mahali husika ili hatua za
kisheria ziweze kuchukuliwa.
Matokeo ya kumalizwa kwa kesi
hizo kienyeji imekuwa ni kuendelea
kwa wimbi la mimba mashuleni na
kusababisha watoto wa kike
kukosa haki yao ya msingi ya
kupata elimu.
“Ndugu zangu lazima tukubali
kuwa ukimwelimisha mtoto wa
kike umeelimisha familia yake
yote. Sisi akina baba mara nyingi
hatukai na watoto nyumbani. Ni
akina mama wanaoshinda nao na
kuwapa malezi ya karibu sasa
kama mama akiwa na elimu ni
wazi atailea familia yake katika
mazingira bora zaidi,” alisema.

WACHINA WALIO KUTWA NA MENO YA TEMBO YENYE THAMANI YA TSH.BILIONI 5.4 WAFANYA JARIBIA LA KUTUO RUSHWA ILI WAACHIWE HURU

RAIA watatu wa China
wanaokabiliwa na kesi ya kukutwa
na meno ya tembo yenye thamani
ya Sh bilioni 5.4, wanadaiwa
kujaribu kutoa rushwa ya Sh
milioni 30.2 kwa askari ili
wasifunguliwe mashitaka.
Wakili Mwandamizi wa Serikali,
Faraja Nchimbi alidai hayo jana
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu wakati akiwasomea
washitakiwa maelezo ya awali.
Alidai Novemba 2 mwaka jana
katika eneo la Kifaru Mikocheni B,
washitakiwa walikamatwa na
askari wakiwa na vipande 706 vya
meno ya tembo pamoja na ganda
la risasi.
Nchimbi alidai washitakiwa hao,
walikiri kumiliki vitu hivyo bila
kibali na kudai watawapa askari
hao na baadhi ya wananchi
waliokuwa katika eneo la tukio Sh
milioni 30.2 ili wasifunguliwe
mashitaka.
Hata hivyo, askari hao, Mrakibu
wa Polisi (ASP) Heri Mugaye,
Sajenti Gerwin, askari wa
Wanyamapori Simon Saye na
wananchi waliokuwa eneo la tukio,
walikataa kupokea fedha hizo na
kuwafikisha kituo cha Polisi na
kuwafungulia mashitaka.
Aliendelea kudai kuwa katika
maelezo ya onyo waliyotoa kituo
cha Polisi, washitakiwa hao walikiri
kukutwa na nyara hizo na risasi
bila kuwa na kibali cha umiliki
kutoka mamlaka husika.
Hata hivyo, jana baada ya
kusomewa maelezo ya awali,
washitakiwa hao waliokuwa
wanatafsiriwa na mkalimani,
walikana maelezo hayo, lakini
walikiri majina, uraia na umri wao.
Washitakiwa katika kesi hiyo ni
Huang Gin (50), Xu Fujie (22) na
Chen Jinzhan (31), walifikishwa
mahakamani hapo Novemba 8
mwaka jana, wakikabiliwa na
shitaka moja, kabla ya kuongezewa
mashitaka mawili.
Awali, Wakili Mwandamizi wa
Serikali, Tumaini Kweka,
aliwasomea upya washitakiwa
mashitaka yao baada ya kufanya
marekebisho kwa kuongeza
mashitaka mawili .
Alidai kuwa Novemba 2, mwaka
jana katika mtaa wa Kifaru
Mikocheni B, washitakiwa
walikamatwa wakiwa na vipande
706 vya meno ya tembo vyenye
uzito wa kilo 1,889 vyote vikiwa na
thamani hiyo, mali ya Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi
wa Wanyamapori.
Alidai katika mashitaka mengine,
wanadaiwa kutaka kutoa rushwa
ya Sh milioni 30.2 kwa askari Polisi
na askari wa Wanyamapori ili
wasifunguliwe mashitaka ya
kukutwa na nyara na ganda la
risasi bila kuwa na kibali.
Katika mashitaka mengine,
washitakiwa wanadaiwa siku hiyo
hiyo walikutwa na ganda la risasi
bila kuwa na kibali cha kumiliki
silaha. Washitakiwa hao walikana
mashitaka yao na kurudishwa
rumande hadi Februari 17 mwaka
huu kesi hiyo itakapotajwa tena.