ads

Monday, March 17, 2014

MMMMH!! MWENYE MACHO AAMBIWA TAZAMA EBU NJOO UCHEKI MAMBO YA TABORA LAANA DUNIANI KWA UFUSKA HUUHAPANA DADA ZETU MMEZIDI SASA NI FULL KUONYESHA MAUNGO WAZI.

Hii ni sehemu za baadhi ya picha zilizoonesha nini kilichofanyika katika ukumbi wa Theophilo Kisanji Tabora ikiwa nimoja ya Show zilizoambatana na Shindano lakumsaka Miss & Mr.Kamna .

SERIKALI YA NIGERIA IMEKIRI MAKOSA AMBAYO YALISABABISHWA NA MKANGANYIKO KATIKA ZOEZI LA KUWAAJIRI WATU KAZI KATIKA MIJI NCHINI

Serikali ya Nigeria imekiri makosa ambayo yalisababisha mkanyagano wa watu pale walipokuwa wakihudhuria zoezi la serikali la kuwaajiri watu kazi katika miji kadhaa Nchini Nigeria.Maelfu ya watu waliokuwa na hamu kubwa ya kupata ajira, walijitokeza kwa wingi katika zoezi la mitihani ya kutafuta kazi kote Nchini humo.Walikuwa wamejitokeza katika ofisi za wizara ya uhamiaji.Watu saba waliuawa katika uwanja wa taifa mjini Abuja.Waziri wa mambo ya ndani Abba Moro, aliambia CSW kuwa utaratibu ulikosekana katika uwanja huo kiasi cha kusababisha vurumai hilo.Zaidi ya thuluthi moja ya watu walio chini ya umri wa miaka 25 hawana ajira nchini Nigeria.

Sunday, March 16, 2014

MASKINI MTOTOANUSURIKA KUCHINJWA NA BABA YAKE KISA....

Mtukioyakikatili yameendelea kushika kasi wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo mtoto aitwayeSaid Siraji/SaidJoshuaamelazwa katika Hospitali ya wilaya usiku wa kuamkia leo, baada ya kunusurika kifo katika jaribio la kuchinjwa nababayake mzazi aliyejulikana kwa jina laSalvatory.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya-Kahama; DaktaJosephFwoma amesema Siraji amefikishwa hospitalini hapo leo alfajiri baada ya kuokotwa na wasamaria wema akiwa anakimbia huko akivuja damu shingoni.Dakta Fwoma amesema baada ya kufikishwa hospitalini madaktari walimfanyia upasuaji na kumshona sehemu ya koromeo aliyochinjwa na hadi alasiri hii hali yake imeendelea vizuri hasa baada ya kuongezwa damu.Kwa mujibu wamamamzazi wa Mariamu Idd(35) amesema, Mtoto Siraji jana alichukuliwa na baba yake mzazi anayeitwa Siraji Salvatory(45) kwenda naye kwake mitaa ya Majengo kwa kuwa wazazi hao walikwisha achana siku nyingi.Mariam amesema, awali Salvatory alikuwaakimchukua Sirajimarakwa mara na kumpeleka nyumbani kwake na baadaye kumrudisha akidai kuchoshwa na huduma za matibabu kutokana na mtoto huyo kuwa na matatizo ya kiafya.Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema chanzo cha tukio hilo inasadikiwa kuwa mtuhumiwa anaugua ugonjwa wa akili.

Saturday, March 8, 2014

PICHA ZA DULLY PAMOJA NA MISS MOROGORO ZINAZOLETA UTATA HIZI HAPA.

Thursday, March 6, 2014

Picha 6 za Nicki Minaj zinazoangaliwa sana hivi sasa kwenye mtandao...!

Unaambiwa Nicki Minaj anajipanga kuja na muonekano mpya pamoja akijiandaa na kutoka na album au mixtape.Mara nyingi picha zinazotoka kwenye media zinazomuonyesha Nicki Minaj akiwa na muonekano wa Barbie kama kawaida yake. 

Lakini hizi picha alizozitoa mwenyewe ameonekana kuwa na nywele zake mwenyewe bila vitu vingine anavyojitupiaga.


HATARII..MFUNGWA AMBAKA MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI HUKO GEITA...!!!


MFUNGWA aliyekuwa
akitumikia kifungo cha miezi
sita katika Gereza la Butundwe
wilayani Geita amembaka
mwanafunzi wa Shule ya
Msingi Luhuha iliyoko Tarafa
ya Butundwe na kumuumiza
sehemu zake za siri, shingoni
na kwenye jicho la kulia.
Mwanafunzi huyo mwenye
umri wa miaka 15 (jina
linahifadhiwa) alitendewa
unyama huo na mfungwa
aliyejulikana kwa jina la
Godfrey Seleman (19) Februari
26, mwaka huu majira ya saa
9:00 alasiri wakati
mwanafunzi huyo alipokuwa
akichanja kuni na wanafunzi
wenzake.
Akieleza jinsi alivyofanyiwa
unyama huo, mwanafunzi
huyo alisema alipotoka shuleni
akiwa na wasichana wenzake
watano walikwenda kuchanja
kuni ndipo walipomuona
mfungwa huyo akiwa amevaa
sare, lakini baadaye alitoweka
ghafla na kurudi akiwa
amejipaka masizi usoni, akiwa
uchi kisha kuanza kumfukuza
yeye huku wenzake wengine
wakifanikiwa kukimbia huku
wakipiga kelele.
Alisema alizidiwa mbio na
mfungwa huyo ambapo
alimshika kisha kumkaba
shingoni na kumwangusha
chini na kuanza kumtendea
unyama na kumsababishia
maumivu makali sehemu zake
za siri.
“Baada ya kutendewa unyama
huo nilitoka eneo hilo ambapo
njiani nikutana na mama
mmoja nikamwelezea mkasa
ulionipata alinionea huruma
ambapo alinipeleka ofisi ya
kijiji ambako niliandikiwa
barua kuwahi polisi,
nikapelekwa hospitali ambako
walinifanyia vipimo,” alisema
binti huyo.
Aliendelea kusema kuwa
mfungwa huyo alimpiga na
kumuumiza katika jicho lake la
kulia ambalo limevimba na
kuwa bado anasikia maumivu
makali jichoni na
shingoni.Kamanda wa polisi
mkoani hapa amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo ambalo
ameliita la kinyama
lisilopaswa kutendwa na mtu
mwenye akili timamu.Alisema
mfungwa huyo mweye na
namba 244/2013 alikuwa atoke
kifungoni mwezi ujao, tayari
ametiwa mbaroni na
atafikishwa mahakamani
upelelezi utakapokamilika

Saturday, March 1, 2014

MASKINI AFANDE SELE...INASIKITISHA SANA...SOMA ZAIDI HAPA...!!!

SIKU chache baada ya kuzagaa
kwa taarifa za kuachana na
mkewe mama Tunda, mfalme
wa Rhymes, Seleman Msindi
‘Afande Sele’ ameibuka na
kusimulia mambo ya
kusikitisha waliyopita katika
safari ya maisha yao.
Akizungumza na wanahabari
wetu ndani ya Ukumbi wa
Meeda, Sinza-Mori, Dar, juzi
Afande alisema hadi kufikia
hatua ya yeye kutangaza kuwa
ameachana na mama Tunda
ambaye amedumu naye kama
mume na mke kwa zaidi ya
miaka 10, alikuwa akivumilia
mambo mengi na mwisho
kuamua kuachia ngazi.
Afande Sele akiwa na familia
yake.
“Nilikuwa nikielezwa mengi
kuhusu mke wangu,
nilishapigiwa simu na
kuambiwa mke wangu
anagombaniwa na wanaume
usiku klabu lakini huwa mimi
siyo mtu wa kuishi kwa hisia,
nilivumilia nikiamini
atajirekebisha, haikuwa hivyo.
“Japo sikuwa na uthibitisho wa
moja kwa moja, lakini
nyumbani alikuwa siyo mtu
wa kutulia, amekuwa
akinizunguka hadi kwa
washkaji zangu wa karibu.
Kuna jamaa alichoshwa na
habari hizo akanifuata na
kuniambia hata kama lakini
uvumilivu wangu ulizidi,”
alisema Afande kwa hisia.
Akiendelea kushusha
masikitiko yake mbele ya
kinasa sauti cha Risasi
Jumamosi, Afande alienda
mbele zaidi kwa kusema mbali
na mkewe huyo kumsaliti kwa
wanaume tofauti wakiwema
marafiki zake, ilifika wakati
mama Tunda akawa
anachukua fedha ndani na
kwenda kutumia na wanaume.
Alisema alitumia mwanya wa
mkali huyo wa mashairi
anapokuwa amesafiri katika
shoo mbalimbali na kuachiwa
fedha za matumizi pamoja na
ujenzi wa nyumba yao mpya,
kutanulia.
“We acha tu, yaani fedha za
matumizi, ujenzi nilikuwa
namuachia lakini cha
kusikitisha ni kwamba
alizitumia kutanulia, jambo
ambalo nililizidi kunitia
umaskini na machungu
ukizingatia jamii inaniheshimu
kama msanii, mbaya zaidi
wananchi wamenitaka
nigombee ubunge Morogoro
Mjini,” alisema Afande.
Akizidi kushusha ‘vesi’, Afande
alitiririka kuwa kuna wakati
aliwahi kupewa taarifa na
rafiki yake mwingine aishie
Kurasini jijini Dar ambaye
alilamika juu ya mkewe kufika
kwa jamaa huyo na kuazima
fedha bila kuzilipa.
Kwenye aya nyingine, mkali
huyo alisema anakumbuka
jinsi alivyoishi na familia yake,
mkewe, wanaye Tunda na
Ahsante Sanaa lakini hana jinsi
kwani ameona bora kuachana
kwani umri wake una mruhusu
kuoa mke mwingine siku
ikitokea.
“Nakumbuka maisha kidogo ya
furaha na familia, mama
Tunda atabaki kuwa mama wa
watoto wangu lakini kamwe
hawezi kurudi kwangu kwani
itakuwa ni aibu juu ya aibu,”
alisema.
Afande aliachana na mama
Tunda mwishoni mwa mwaka
jana alipotimba jijini Dar
katika shughuli zake za kikazi
na kumuachia mkewe fedha za
ujenzi lakini aliporejea
nyumbani Morogoro, alikuta
mzazi mwenzake huyo
ameondoka nyumbani na
kuacha funguo, kila
alipompigia simu hakupokea.
Alipoulizwa kuhusiana na
shutuma zilizoporomoshwa na
Afande, mama Tunda
alitiririka:
“Alinipa Sh. milioni 3 za shoo
tu, tukanunua vifaa vya ujenzi
lakini siyo kwamba nilitanua
na wanaume, tena kama ni
kumfumania, mimi ndiye
nilimkuta na mwanamke
alitoka naye Fiesta Dodoma,
sikutaka tu kumsema, hizo
taarifa anazusha tu.
“Kwanza kuna mambo mengi
tu amenifanyia, alikuwa mlevi
kwani hadi wazazi wangu
walikuwa wakinishangaa sana,
sasa na mimi nikaona bora
niachane naye,” alisema mama
Tunda.

Whatsapp YAJA NA KASHESHE HIVI KARIBUNI LA KUWAUMBUA WAONGO

Kasheshe tena bonge la
kasheshe laja. Kwa kutumia
maspy wake wa kimataifa,
blog yenu mzigo imekuja na
taarifa ambayo italeta
usumbufu mkubwa katika
jamii ya watumia whatsapp
hapa Bongoland. Najua
mnajiuliza ni nini? Hata sisi
wakurugenzi, waandishi,
wafagizi wa hii blog ya
chekanakitime tuliduwaa
hivihivi kama wewe
ulivyoduwaa wakati tunasubiri
kuelezwa na spy wetu wa
kimataifa ni nini alichogundua
kuhusu watumiaji wa
Whatsapp.
Baada ya Whatsapp kuwa na
kale kamtindo kabaya ka
kuumbua watu kakusema 'Last
seen 2:00'na hivyo kuua kale
kakisingizio kuwa simu ilikuwa
imezima kwa kukosa chaji sasa
wanakuja na mpya zaidi. Kale
kakipengele katakuwa
kanataja hata ulipo, hivyo
katakuwa kakisomeka
mfano,'Last seen 2:00 Sokoni
Kariakoo'.
Sasa hii ni mbaya sana wakati
mtu kakutumia mesej...Baby
tumekusanyika hospitali
mamake rafiki yangu yu
mahututi' Huku Whatsapp
inakuonyesha 'Last seen 2:00
Coco Beach'... Kamtindo haka
kanategemea kuua mapenzi na
ndoa kadhaa ambazo mpaka
sasa zinaonekana kuwa imara
sana.

Friday, February 28, 2014

Download New Best song Anko Dunia ( Roshazy ft: Cress )

DOWN LOAD NEW BEST SONG DUNIA UTANDAWAZI by Yamala

https://www.hulkshare.com/yuskisskisiba/yamala[hulkplayer code="6gtmgsz03sao"]

MWANA DADA WEMA ATAJA SIFA ZA MWANAUME ANAYE MTAKA SOMA HAPA SIFAHIZO KAMA UNAZO

Mwanadada Wema Sepetu ambaye
pia aliwahi kuwa Miss Tanzania
2006 ambaye kwa sasa
anaendesha kampuni yake binafsi
iitwayo Endless Fame
inayojishughulisha zaidi na
utengenezaji wa Filamu
mbalimbali.
Kupitia kipindi cha Leo tena
February 28 Wema Sepetu
amekubali kutaja sifa za
mwanaume anayempenda kuwa na
mvuto kwake,swali lililoulizwa na
Watangazaji wa kipindi hicho ni
kuhusu mwanaume wa sifa gani
anayedhani anaweza kuolewa nae
ambapo Wema alijibu “Kuolewa sio
shida je huyo mwanaume
nampenda,maana naweza kuja
kuchumbiwa lakini nisimpende”
“Mimi nampenda Mwanaume
mweusi,wanaume weupe sio
kwamba sijawahi kuwa nao lakini
nakuwa sina mzuka nao”.
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake
na Diamond amekiri kwa
kusema’Kweli niko na Nasib -
Diamond na nadhani muda huu
kutakua na utulivu ndani yake,ule
utoto tuliokua tunafanya nadhani
ulikua utoto na imekua Power
Couple toka mwaka 2010 kwa hiyo
tuna ni miaka 4 sasa,kwa sasa
tumeamua kuwa serious’.
Habari kwa Hisani ya Millard Ayo
Wema Sepetu pia kaandamana na
Ant Ezekiel kwenye interview ya
kipindi hicho kinachorushwa na
Clouds Fm.

Thursday, February 27, 2014

Polisi wa Uganda wamezuia kundi la wanawake waliopanga kuandamana kupinga sheria inayopiga marufuku picha chafu.

Polisi wa Uganda wamezuia
kundi la wanawake waliopanga
kuandamana kupinga sheria
inayopiga marufuku picha
chafu.
Chini ya sheria hiyo ni marufuku
kwa wanawake kuvalia mavazi
mafupi, yenye kubana mwilini
kiasi cha kuonekana mapaja na
makalio na sheti inayoonyesha
matiti.
Wanawake hao waliopanga
kuandamana mjini Kampala
walibeba mabano kupinga sheria
mpya baadhi wakuvalia mavazi
mafupi. Baadaye walikubaliwa
kukusanyika katika uwanja nje ya
ukumbi wa kitaifa.

Wednesday, February 26, 2014

DIAMOND ASEMA HAYA JUU YA WASANII WA WA TANZANIA KUHUSU MAJUNGU

Diamond Platnumz
kiukweli, nasikitishwa sana jins
baadhi ya wasanii kutwa
wanavyolazimisha kunitengenezea
ugomvi wa kilazima pasipo kuwa na
sababu, mara wengine wakizusha
eti Nimewatusi kwenye Media,
Mara sjui Nimepost kuwakashif,
yaani ilimradi tu....kwanini
Wanamuziki wa Tanzania
Tunashindwa kubadilika... mbona
mi nahangaika na muziki wangu
kimpango wangu... Mnasema nyie
ndio mnaojua kuimba mie sijui
"sinatatizo"... Mnasema nyie ndio
wenye sauti nzuri yangu mbaya
"Sina tatizo"... sasa mbona tena
bado mnanifatilia na kutokujua
kwangu... Nafkiri ni vyema mkaanza
kutumia ujuzi wenu kukuza sanaa
ya nchi yetu na kuleta heshima na
maendeleo nchini, kuliko kupika
majungu..... Watu wanataka kazi!

JE WAJUA MWANAMKE MWENYE ULIMI MREFU DUNIANI SOMA HAPA UPATE KUJUA

Pichani kushoto ni bi mdada
Chanel Tapper akionyesha urefu
wa ulimi wake
Chanel Tapper ni mwanafunzi wa
chuo cha California Marekani,
ndiye mwanamke wa kwanza
anayeshikilia rekodi ya dunia ya
kuwa na ulimi mrefu kupita
wanawake wote, inasemekana
anaulimi wenye urefu wa sentimita
9.7, baada ya kuingia katika kitabu
cha rekodi za dunia maarufu kama
Guiness , amesema anategemea
wahisani pamoja na hela
atakazopata ziweze kumuendeleza
katika kumaliza chuo na masomo
yake.

HOT PHOTOS...TANZANIAN ACTRESS LULU....!!YOU MUST SEE..

Tutumie picha zako ambazo ungependa kushare mitindo ya mavazi , swaggz na mapozi mautundu ya kinyamwezi
katika mtoko waleo leo

namba yakutuma ni
+255 (0) 655323305

BAADA YA MSANII PNC KUJITOA MTANASHATI NA KUMSINGIZIA UONGO USTAZ JUMA, ARUDI NA KUMPIGIA MAGOTI. CHEKI PICHA HAPA

Baada ya kutimuliwa
MTANASHATI msanii PNC arudi
mikono nyuma akimuomba boss
wake Ostaz Juma arudi tena
katika lebo hiyo. Picha hii
imeonekana katika account ya
facebook ya Ostaz Juma ikisema
“hahaha jamani mziki ni kazi
pnc arudi kuomba msamaha ili
aendelee kufanya kazi
mtanashati”
Na baadae mtu mzima Ostaz
akatupia video clip ikimuonyesha
PNC akiomba msamaha kwa
machungu kabisa hebu bonyez
CREDIT : DJ CHOKA

Tuesday, February 25, 2014

NISHA AMFANYIA SUPRISE MAMA YAKE HEMEDI PHD SOMA HAPA UJUE

Nisha amfanyia suprise mama
yake Hemedi PHD katika siku
ya kuzaliwa mama yake Hemedi
PHD ilikuwa kinondoni
barabarani akamwambia
hemedi kapata ajali alivyotoka
nje alikuwa kapagawa mara
waka mwimbia happy birth day
toyuuuuuuuuu...!!!
Ha ha haaa!!! Mama Hemedy
hoi tena kibaya zaidi siku hio
ilikuwa ndio siku ya
kumaliziwa Shooting ya Filamu
ya GUMZO ambayo kwa sasa
ipo mbioni kutoka,
Yani mama kutoka tu nje
akaona msongamano wa
magari watu kibao akaamini
kuwa mwanae kapata ajali
kweli kumbe ilikuwa ni katika
kumalizia kipande cha Filamu
ambapo Hemedi PHD
anatakiwa aonekane katika
ajali ya kugongwa na gari.. Du!
mama almanusura kuzimia.
Mama yake hemedi alifarijika
sana ilikuwa kipindi cha
shooting ya gumzo

Daktari FEKI akamatwa hospitali ya Muhimbili......Hili ni tukio la tatu kutokea

Hospitali ya taifa ya Muhimbili imemkamata mtu mmoja anae sadikiwa kuwa daktari feki ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akitapeli wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika hospitali hiyo ya taifa kwa namna  mbalimbali  Daktari huyo aliyejulikana kwa jina la Kitano Mustafa Kitani mwenye umri miaka 51 anadaiwa kuwa alikuwa anajitambulisha kama daktari upande wa akina mama katika hospitali ya Muhimbili.Hospitali ya taifa ya Muhimbili mbali na utaratibu wa kutumia vitambulisho kwa wafanyakazi ili kuondoa tatizo kama hili, bado tatizo hili limeendelea kujitokeza.Hospitali ya Muhimbili inawataka wafanyakazi wake wanaoshirikiana na madaktari vishoka kuacha tabia hiyo yenye athari kwa wagonjwa na taifa.Chama cha Madaktari nchini kimewataka wananchi kuwa  macho na madaktari wanaojitokeza kutaka kusaidia wagonjwa.Wakati daktari huyo akidai yeye ni daktari kitaaluma, Afisa Usalama hakubaliani nae kutokana na taarifaza kiuchunguzi kuthibitisha kuwa ni feki.Hili ni tukio la tatu kutokea katika hospitali ya Muhimbili.

Monday, February 24, 2014

MWANA DADA MREMBO AFIA GEST JIJINI ARUSHA

MREMBO mmoja ambaye alihu-
dumu kwenye nyumba ya kulala
wageni na baa (jina tunalo)
iliyopo Tengeru, wilayani
Arumeru, mkoani Arusha,
Blandina Michael (33) amekutwa
amekufa kwenye moja ya vyumba
vya nyumba hiyo huku chanzo
cha tukio hilo kikihusishwa na
vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu
mmiliki wa nyumba ya wageni
moja ambaye pia anajihusisha na
biashara za madini (jina tunalo)
kwamba alimtoa kafara
mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa,
kila mwaka mtu mmoja katika
biashara zake hupoteza maisha
ghafla.
Hata hivyo, mfanyabiashara huyo
alipoongea na Uwazi juzikati
alikanusha vikali tuhuma hizo na
kueleza kuwa yeye ni muumini
mzuri wa imani yake.
‘’Hao watu wanapotosha sana,
unajua kuna mwaka mwanaume
mmoja alikufa ghafla kwenye
nyumba yangu ya kulala wageni,
alikuja na mpenzi wake ila
alimeza Viagra ambazo hata
polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na
mimi tukio hilo wanaliunganisha
na hili kwamba nawatoa kafara,”
alisema.
Kifo cha Blandina kilitokea ndani
ya chumba huku mtu mmoja
anayedaiwa kuwa mpenzi wake
aliyejulikana kwa jina moja la
Timo, mkazi wa eneo hilo
akihojiwa na polisi.
Marehemu Blandina ambaye ni
mzaliwa wa mkoa wa Tanga,
anaelezwa na bosi wake huyo
kwamba alikuwa kama mtoto wa
familia yake kwa vile alimwamini
sana. Alifanya kazi hapo kwa
miaka 8 na hakuwa na tatilo la
kiafya.
Bosi huyo alisema mwili wa
marehemu uligundulika baada ya
mfanyakazi mwenzake wa kiume
kumpigia simu saa 2 asubuhi
ambapo simu yake ilikuwa ikiita
bila kupokelewa ndipo alipoamua
kwenda kumgongea katika
chumba hicho.
Alisema baada ya kufika
alishangaa kukuta mlango wa
chumba chake uko wazi na
alipochungulia alibaini kwamba
Blandina alikuwa amefariki dunia.
Hata hivyo, polisi baada ya kufika
na kuufanyia uchunguzi wa awali
mwili huo hawakugundua
kuwepo kwa jeraha lolote
linaloashiria kuuawa, ingawa
mwili huo ulipelekwa kufanyiwa
uchunguzi wa kitaalam katika
Hospitali ya Mkoa ya Mount
Meru.

COVER YA FILAMU YA MPONZA DR.CHENI

Msanii wa filamu hapa nchini
anayefahamika kwa jina la Dr.
amejikuta katika wakati mgumu
baada ya bodi ya filamu Tanzania
kuzuia filamu yake mpya inayoitwa
'Nimekubali Kuolewa' kwa madai
ya cover iliyotumika katika kasha
la filamu hiyo inachochea ushoga.
Kufuatia madai hayo msanii huyo
amesema kuwa
bodi hiyo haikumtendea haki kwa
kuwa filamu yake ina lengo zuri la
kupinga ushoga na sio kuchochea.
Ameela bodi hiyo haikuangalia
maudhui na badala yake
imeangalia zaidi cover la filamu
hiyo
“Eti ushoga wangu uko kwenye
kujiremba sana, wamenionea,
lengo letu ni kukemea na kupinga
vikali vitendo vya ushoga na ndoa
za jinsia moja, huwezi kuelimisha
bila kuonesha madhara yake kwa
vitendo kama ilivyo kwenye filamu
hiyo. Amesema Dk Cheni.
Msanii huyu amekumbwa na hali
hiyo ikiwa ni muendelezo wa bodi
ya filamu kuzuia filamu ambazo
inazitilia mashaka.
Hata hivyo bodi hii imekuwa
ikilalamikiwa na baadhi ya wasanii
wakidai haitendi haki.